Zitto amefeli Leadership Qualities

Zitto amefeli Leadership Qualities

Tunataka chama kinachofuata na kuheahimu na kuilinda katiba na kuepuka kulindana ata pindi mtu wa karibu na mwenye ushawishi vip kwa watu ila akivurugaa anapigwa chini na maisha yanaendelea
chadema wameonyesha mfano mzuri hawakujari umaarufu wa zitto au watu wangapi wanamfuata nyuma ila kwa sababu kavunja katiba basi atupishe
hichi ndo chama cha kukipa nchi
 
Ngumu kumeza duh! ni vyema wanachama wa Chadema wakaamua kufikiria kuwa ndani ya miaka 7 hadi 10 inayokuja kutokana na hali hii ya kutuhumiana wenyewe kwa wenyewe hadi kufikia huko hali itakuaje?

Nilitegemea maamuzi yaliyochukuliwa jana yangetoka Chama kingine...............na sio CHADEMA.

Mkuu haya mambo ya Zitto yana historia ndefu sana na pengine wengi mnawaza matokeo yake sasa kwavile hamjafatilia siasa hizi muda mrefu. Zipo hayupo active kwenye shughuli za chama muda mrefu sana na ofisi yake kuu ni Facebook na Twita......
 
Naomba kuuliza je kwa hiyo hana tena ubunge? au kuna hatua za kufanya ili apoteze rasmi ubunge?. Kama zipo zifanywe haraka tuone muvi itaendeleaje
 
Zitto alikua naibu katibu mkuu wa chama sasa alitaka nafasi gani tena ili alidhike
Ifike kipindi binadamu tuwe tunalidhika na tulichonacho
Ata shetani alikua ivo ivo kajawa na Tamaa anatakaa high power more than the Almighty
Ndo kama zitto sasa mwisho wa siku anakosa vyote na kuanza kutengeneza utawala wake ambao hakika hauta dumu for last longer
CHADEMA chini ya Mwenyekitu Mboye je?? Chama kinashuka au ndo kinapanda
Ukiangalia Uongozi wa mboye umekua na mafanikio sana na kufanya chama kimekua na mvuto kwa wananchi kwa kawaida tunaona tunatoka kwenye point moja tunaenda nyingine sasa anapotokea mtu ndani ya chama anakua anahalibu badala ya yeye kua ndo mwenye uchungu wa kukijenga chama ili baadae aje afaidi matunda ya misukosuko yake na safari ndefu
Uamuzi wa chama ni mzuri kabisa wamemtoa ili wao waendelee na safari wakiwa na lengo moja ambalo litaleta manufaa kwa wananchi
VIVA CHADEMA VIVA
 
Pole kaka, Ndio Siasa Zilivyo, Najua ulivyoumia kaka

Lakini nadhani ni muda muafaka kwa Zitto kwenda chama kingine, kwa sababu kama wenzie "hawamtaki" kwa sababu yoyote ile kwa nini alazimishe kuwa nao

kuuumia for what?? tunarudisha nyuma mapambano ya kuiondoa CCM\
unless uje useme zitto anaipaisha CCM...just sad for chadema na mstakabali wake

afadhali yeye hawajamuua
 
wachaga walishaamua kumng'oa zito baada ya yeye nakundi lake kutaka katiba ya chama ifanyiwe marekebisho pia safu ya juu ya viongoz ibadirishwe...!,mbaya zaid wanasiasa wakibongo wana tabia ya kukomoana bila kujali madhara ya pande zote...!uwepo wa zito chadema ulikuwa na umuhim wake,hivyo kukurupuka kumng'oa huenda pia kukaleta madhara makubwa sana kwa chama kuliko watu wanavyo dhania,km kumegeka kwa wafuas,siri za chama kuwa pasipo huska km na yeye ataamua kukomoa,jino kwa jino,akuanzae mmalize... N.k
nafikiri mawazo yako ni sahihi ila kitendo walichofanya cdm kimewanyongonyesha watu ambao walishaanza kuamini upinzani.hapa ndio upinzani unapoonekana kama wasanii tu
 
Cdm ilisha baki safi wote wanaopiga kelele
humu Kumtetea zito ni mafisiem jamani mfuateni act
 
zitto alikua naibu katibu mkuu wa chama sasa alitaka nafasi gani tena ili alidhike
ifike kipindi binadamu tuwe tunalidhika na tulichonacho
ata shetani alikua ivo ivo kajawa na tamaa anatakaa high power more than the almighty
ndo kama zitto sasa mwisho wa siku anakosa vyote na kuanza kutengeneza utawala wake ambao hakika hauta dumu for last longer
chadema chini ya mwenyekitu mboye je?? Chama kinashuka au ndo kinapanda
ukiangalia uongozi wa mboye umekua na mafanikio sana na kufanya chama kimekua na mvuto kwa wananchi kwa kawaida tunaona tunatoka kwenye point moja tunaenda nyingine sasa anapotokea mtu ndani ya chama anakua anahalibu badala ya yeye kua ndo mwenye uchungu wa kukijenga chama ili baadae aje afaidi matunda ya misukosuko yake na safari ndefu
uamuzi wa chama ni mzuri kabisa wamemtoa ili wao waendelee na safari wakiwa na lengo moja ambalo litaleta manufaa kwa wananchi
viva chadema viva

chagalism ndani ya chadema
 
WOTE MNAOMKOSOA ZITTO HAPA UMRI WENU NAONA NI MDOGO NA MNAONGEA BILA YA KUFANYA RESEARCH, NA MLIIDANDIA HII MELI MWAKA 2010, WAKATI PALE MWANGA WA NURU ULIPOTUFIKIA CHADEMA, MNASAHAU NI ZITTO, NA WENZAKE WAKONGWE NDANI YA CHAMA NDIO WALOKISAIDIA CHAMA KUONEKANA NI CHAMA CHENYE WATU MAKINI, NA WENYE MAWAZO YA KIMAGEUZI, LEO HII MBOWE KATEKWA AKILI NA WAKUJA AMBAO HATA HAWANA MIAKA 10 NDANI YA CHADEMA,. MTOA POST HUJAFANYA RESEARCH YA KUTOSHA, NAHISI HIKI KITU KINACHOITWA "DURANTE BENE PLACITO NOSTRO" KINAUTESA UONGOZI WA JUU. SITAKI KUAMINI KUWA CHAMA KITAKUFA, NA SITAKI KUAMINI UTAKUA MWISHO WA ZITTO, HII VITA YA KUMZIMA ZITTO NI MIPANGO YA MAFISADI, WA CCM WAKISHIRIKIANA NA WAJINGA WACHACHE TENA WAKUJA NDANI YA CHAMA, AMBAO WAMEPEWA MADARAKA NOW WAMEKUA WANAKIBURI KIASI WANAWEZA KUMVUA YOYOTE UANACHAMA, KAMA KINA KIBATALA, MALLYA, LISSU, MABERE MARANDO, GODBLESS LEMA, NA WENGINEO WANGEKUWA WASAFI NA WAADILIFU kwanini walihama vyama vyao na kuja kujiunga na chadema, na kama ni mikakati yao ni kuiua chadema, NASEMA WASHINDWE, TENA WASHINDWE KABISA NA WALEGEE, MWISHO napenda kumpa pole ZZRK, kumptia moyo kuwa haya ndio maisha ya siasa, kwani umetufanyia mengi, mazuri japo BINADAMU MWEPESI KUSAHAU NDIO NATURE YAKE, ila pia hatujakamilikazzk kama binadamu anamapungu yake. HAKI YA KWELI IPO KWA MUNGU DUNIA NI DHULUMATI. PUMZIKA KWA AMANI RASTA MAN CHACHA WANGWE, JANA TAREHE 10 ZITTO KAFUTWA UANACHAMA NA WANACHAMA WALIOJIUNGA CHADEMA 2004. WAKATI ZITTO ANA ZAIDI YA MIKA 20 CDM.
WAKATI ZITTO ANA ZAIDI YA MIKA 20 CDM.[/QUOTE] zitto anamiaka 20 na chadema hii kali. Kwa hiyo chuo kikuu alijiunga na miaka 17? maana 2015 atakuwa ana miaka 37. 37 ukitoa 20 unapta 17. N yeye mwenyewe alikiri Mbowe ndiye alieyemfuata akiwa chuo Kikuaa ili ajiunge CAHADEMA kweli wafuasi wa zittomna safari ndefu ya kujenga hoja
 
kama ccm hamwezi maamuzi magumu sisi tunaweza kila siku lowassa anawajambisha ila kumtimua hamwezi kazi kumchafua na kumtukana tu
chadema ni mpango wa mungu
woga wenu woga wa kijinga aibu kubwa hamtaki kuambiwa ukweli udini ukabila ukanda umewajaaa,mtakosa kura kwa uzembe wenu,cdm bila zitto hakina mvuto.zitto,kitila wangemsaidia sana mbowe ambaye hana uwezo hata wa kujenga hoja ni mwanasiasa wa kurudia rudia maneno.
 
Mi nauliza kama keshapoteza ubunge wake rasmi au bado kuna hatua za kumwarifu spika ili ampige marufuku kumwona bungeni? Kama bado kuna hatua zaidi basi wazikamilishe haraka ili tuone muvi litaendeleaje
 
woga wenu woga wa kijinga aibu kubwa hamtaki kuambiwa ukweli udini ukabila ukanda umewajaaa,mtakosa kura kwa uzembe wenu,cdm bila zitto hakina mvuto.zitto,kitila wangemsaidia sana mbowe ambaye hana uwezo hata wa kujenga hoja ni mwanasiasa wa kurudia rudia maneno.

Ndio anarudia rudia maneno lakin chama kinasonga mbele zitto kasimamishwa mda sana kwenye chama na huyo mkumbo ila angalia uchaguzi mdogo chadema imefanya nini bila hao wasaliti wako
Chadema kuna watu makini sana zaidi ya zitto na tuna vijana wapo wengi sana wasomi na wenye uwezo mkubwa sana
Na siku zote dhambi ya usaliti haitaweza kuwaacha na huko wanapoenda napo watafanyana ivo ivo
CHADEMA NI MPANGO WA MUNGU
 
Hiyo red; hivi ungekuwa wewe ndiye Mwanasheria Mkuu wa Chadema then baada ya uamuzi wa jana wa Mahakama ukaulizwa na waandishi wa habari juu hatma ya Zito nani ya Chama, ungefanyaje? Ungekaa kimya tu? Tungekuona una kiburi! Tundu Lissu ndiye msemaji rasmi wa Chama juu ya masuala yote ya kisheria na kwa kweli ametimiza wajibu wake kikamilifu. Tatizo lenu mnataka mijitu isiyotimiza wajibu na mioga kuchukua maamuzi hali iliyotufikisha hapa tulipo kama taifa.

Well said dudus!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom