Zitto amefeli Leadership Qualities

Zitto amefeli Leadership Qualities

Chadema imejifunga goli dakika za majeruhi, CCM itapeta tu uchaguzi October

CCM itapeta kwa lipi? Hizi propaganda nyepesi nyepesi peleka Lumumba. CCM wamekosa mbinu. Thinktank hawapo tena CCM. Wamebaki wabashiri tu wa aina ya Sheikh Yahya.

Eti mashabiki wa ZZK ni magamba...Mjinga tu ndio atatishwa na ZZK kuondoka CDM.
 
Huyu mheshimiwa kufukuzwa uanachama katika CDM sio kwamba ndo mwisho wa safari yake katika siasa cha kufanya akae atulie na kufanya uamuzi sahihi ni nini cha kufanya ili kuendeleza kujenga nchi yetu kwa sababu huyu jamaa ni msaada mkubwa sana katika nchi yetu make aliweza kuibua mambo mengi sana ambayo ni maovu yaliyofanywa na baadhi ya viongozi.

mwisho,, harakati sio chadema tu broo zitto cha msingi angalia mbele tu usigeuke nyuma kiangalia upumbavu wao huo
 
ZZK ataomba rufaa ya kesi yake hawezi kuyaacha mahela yake ya ubunge.
 
Sasa ndugu,kosa la 'wakuja'' akina sisi ni lipi kwenye sakata hili.Kwenye taasisi mtu akijiunga si anakuwa na haki sawa na aliowakuta?
Au akina Mwigamba na Kitila nao ni wakongwe CHADEMA?

Kosa la msingi la Zitto,Mwigamba na Kitila ni kuandaa mkakati wa kuuondoa uongozi wa juu kinyemela,bila kufuata taratibu za chama.Kwa kosa ambapo walitumia majina feki kama MM,MM1,MM2 na MM3 WALIKIRI NA KUOMBA MSAMAHA.

Lakini sio kila mtu akiomba msamaha hupewa! Sasa kwa kosa hili utawalaumu vipi hao kina Lissu,Kibatala etc?

Wao wanafuata katiba ya chama.
WOTE MNAOMKOSOA ZITTO HAPA UMRI WENU NAONA NI MDOGO NA MNAONGEA BILA YA KUFANYA RESEARCH, NA MLIIDANDIA HII MELI MWAKA 2010, WAKATI PALE MWANGA WA NURU ULIPOTUFIKIA CHADEMA, MNASAHAU NI ZITTO, NA WENZAKE WAKONGWE NDANI YA CHAMA NDIO WALOKISAIDIA CHAMA KUONEKANA NI CHAMA CHENYE WATU MAKINI, NA WENYE MAWAZO YA KIMAGEUZI, LEO HII MBOWE KATEKWA AKILI NA WAKUJA AMBAO HATA HAWANA MIAKA 10 NDANI YA CHADEMA.
 
Zito alikuwa kuwadi mbaya sana ndani ya CDM na huko anakokwenda itakuwa hivyo hivyo yeye anaangalia 'hongo' TU
 
Zito si mvumilivu na ni mbinafsi. Kama wanamchukia asingepewa nafasi ya uongozi ndani ya CDM. Useme wamemvumilia wameshindwa na yeye alifikiri cdm haiwezi kuwepo bila yeye. Itampa nafasi kujitafakari upya ili abadilike.
 
Watu tuache unafiki.

Hapa kinachowaumiza pro-Zitto ni timing tu,hamna jingine.

Yeye alitaka kutangaza hatma yake ambayo sote tunaijua,ya kwenda kwenye Alliance yao mwisho wa mwezi maana uchaguzi wa Alliace ni May.

Sasa hapa ni kwamba kawahishiwa na kuondolewa kaheshima cha ''Kuhama'' na kuvishwa ''Kufukuzwa/timuliwa". Otherwise destiny yake inajulikana.

Tunatakiwa kumtakia mafanikio katika Alliance badala ya kuanza kumlilia mtu ambaye hajapotea, anayeenda kwenye gheto lake.

Kila la kheri kamanda ila yale mambo ya kisirisiri achana nayo, hayalipi. Tutasikitika kama utaanzisha mkakati wa siri kujiita synonym kama MM tena ili umpindue labda katibu au mwingineo.
 
Zito si mvumilivu na ni mbinafsi. Kama wanamchukia asingepewa nafasi ya uongozi ndani ya CDM. Useme wamemvumilia wameshindwa na yeye alifikiri cdm haiwezi kuwepo bila yeye. Itampa nafasi kujitafakari upya ili abadilike.

Ukweli mtupu!!
 
Ikafie mbele huko,chadema ina vijana wengi wasomi kwa sasa kila kona ya nchi
 
Kazi sio siasa pekee jamani,kuna kaz nyingi tu za kufanya na mtu akaishi
 
Tangu mwanzo wa mgogoro tulishauri kuwa kwa kiongozi kijana kama ZZK ilikuwa ni muhimu kuwa na washauri wenye mtazamo chanya badala ya wasaka tonge. Ninaamini bado ana nafasi ya kufanya mabadiliko na akabakia kuwa a young political icon kwa siasa zetu.

afwe: ni kweli kabisa!!!
ZZK ni kijana ambae uwezo wake ni mkubwa!! lakini Tabia moja ya WTZ hawana washauri wa kumshauli!!!!! ukikosa washauli utajikuta ukiingizwa kwenye mikasa itakayo gharimu maisha!!!
ZITO anaweza kulekebisha kila kitu bado ni kijana!!!!!
 
Umakini wowote wa taasisi ni kusimamia miongozo yake hasa KATIBA. CDM haijamfukuza Zitto bali amejifukuza yeye kikatiba. Anaijua vizuri Katiba YA Chama na ameshiriki kwenye marekebisho yake. Ajipange kuomba upya uanachama au aanzishe chama chake .

Chama alishaanzisha ACT!
 
Kwa stahili hili hii ya ubabe,Chadema bado sana kuchukua nchi.Bado chama hakijakomaa kidemokrasia.


Acha kuweka akili likizo wewe,ubabe wa Chadema uko wapi hapo,ni heri kuishi na mchawi kuliko msaliti
 
Umakini wowote wa taasisi ni kusimamia miongozo yake hasa KATIBA. CDM haijamfukuza Zitto bali amejifukuza yeye kikatiba. Anaijua vizuri Katiba YA Chama na ameshiriki kwenye marekebisho yake. Ajipange kuomba upya uanachama au aanzishe chama chake .

mmh kabla ya zitto kwenda mahakamani CDM hawakusimamia katiba!! yaani katiba inasimamia kwa vitu vya ku favor upande huu na inavunjwa kwa vitu ambavyo havi ku fevi
 
Kichuguu,

mkuu tatizo ni kwamba SHERIA HUWA HAINA MSAMAHA!!!

ndo maaana hata wakati wa MAO kule china Waliokikuza cha na viongozi waandamizi walinyongwa!! maaana sheria haina msamaha....
LENIN kule RUSIA kuna viongozi vigogo wa chama walinyongwa na ambao walikikuza chama na ambao walihusika kwenye mapinduzi!!
sheria haina msamaha...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom