CosaNostra
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 382
- 139
Mbona hakukataa zile 3bln za wenye migodi ya madini kule kanda ya ziwa?
By Zitto,
Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.
Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.
Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.
Source: His facebook page.
Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.
Huko kwenye vyama vyenu, Nani mwenye uwezo wa kujitolea na kufanya Kama zzk.
Mbowe alisema gari la serekali silitaki na bado analitumia Hadi kubebea magendo kenya, lakini yeye kufanya hivyo ni sawa
act inauza kadi, tshirt na michango ya kila mwezi ya wanachama,kwani act wana shida ya pesa? Tafakari chukua hatua
Wangefanya hivyo hivyo wabunge wote tungepiga hatua.
......... viva Zitto zuberi kabwe.
Mbona hakukataa zile 3bln za wenye migodi ya madini kule kanda ya ziwa?
alizohongwa na ccm ni zaidi ya 238 mara 4 kwa hiyo asiwa danganye watu hyo yuda nyepesi ayatwallah aka supreme leader
Msaliti, msalitii ,msaliti,msaliti,msaliti,yuda,yuda,yuda
Maana yake atazichukua. Kutoa ocean rd etc mbona hata wengine nao watachangia hivyo hivyo? Sanaaa
Ukimfata zitto utapotea
ni unafiki kukataa posho kwa mkono mmoja na kupokea kwa mkono mwingine ,huyu anatumia NGO yake kupokea posho na rushwa kwa mgongo wa ufadhili kumbe anatumia katika chama chake cha act
Husuda chuki binafsi choyo na uvivu wa kufikiri ndio tatizo lenuMpendazoe HAJALIPWA mafao yake hadi leo!Dr Ndembela Ngungangwa hadi anafariki hakulipwa mafao yake!
Zitto analipwa mafao yake yote daaah
Zito ndio mwanasiasa pekee anayetenda anachokiongea,wengine wote hasa yule mwenye makengeza kwake ni pesa mbele maslahi ya wananchi baadaye