acha chuki binafsi mkuu iyo posho una ushahidi anachukua, mbona rahisi kujua anazo stahli ni zile za mwanzo alipojiuzuru ubunge hizi 230 zinazotaka kusainiwa ndo atapeleka aliposema. HUYU NDO MZALENDO WA KWELI.
Atazipelekaje bila kuzichukua?
Hili swali hata mi najiuliza sana. Au zikitoka hazina zitaenda zenyewe huko Ocean Road??
Pili ikitokea huko Ocean Road wakaandaa list ya waliochangia, hizo hela zitahesabika zimetoka wapi? Hazina au kwa Zitto??
Hata kabla chama cha ACT-Wazalendo hakijaanza kufanya ziara rasmi katika mkoa wa Lindi, Kiongozi mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe kutuma salamu kwa vya siasa vilivyopo katika mkoa huu. Hasa wilayani Nachingwea, Wilaya ambayo inatajwa kuwa ni miongoni mwa ngome imara za Chama Cha Mapinduzi, wakati CUF wakifuatia kwa umaarufu katika wilaya hiyo.![]()
Chama hicho kimeweka rekodi ya kipekee katika ukanda huu Baada ya kuingiza wanachama takribani 300 ndani ya dakika 45 katika mtaa wa Kilimani hewa mjini Nachingwea ambapo Zitto aliingia mjini hamo kimyakimya kwa ajili ya kushiriki mazishi ya baba mzazi wa mwandishi wa habari wa kampuni ya Mwananchi, Peter Nyanje.
Zitto alidhihirisha kukubalika na wananchi baada ya wananchi hao kubaini alikuwa ndiye.
Zitto ambaye muda mwingi alikuwa ametulia na kujiweka katika kundi la watu wa kawaida.
Mnyetishaji huyo wa habari hii ambaye hakutaka jina lake liandikwe Mtandaoni, Alisema eneo ambalo lilitia fora ni kijiji cha Mtua."bro(kaka) yule jamaa anakubalika,pale Mtua amesababisha bendera za CHADEMA kushushwa pale Mtua,wala hakuwaamrisha bali tulishangaa wanamshangilia kwenda kushusha bendera ya CHADEMA,na wengi wao walikuwa vijana,"alisema.
By Zitto,
Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.
Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.
Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.
Source: His facebook page.
Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.
mkuu umemeaanisha ulichokisema au ni kejeli umetoa!?