by zitto,
juzi nilipokuwa jijini mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.
Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi shule ya buhangija na hospitali ya saratani ya ocean road. Buhangija nilitembelea mwezi aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.
Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na miss. Tanzania briggite alfred ambaye anajenga bweni pale. Ocean road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu hajjat shida salum.
Source: His facebook page.
Huyu zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.
Kama ungesoma vizuri post yake (ZZK) ungegundua kuwa hakusema kuwa atakataa. Alisema ataitumia katika kusaidi wahitaji kama vile kuchangia ujenzi wa mabweni katika hospitali ya ocean road! Matusi/maneno ya kashfa na kejeli hayakujengi mwana JF; badala yake yanakufanya uonekane kuwa u-mvivu wa kufikiri. Badilika!Posho hizo ni kwa mujibu wa sheria so atapokea maana ni mafao kwa mujibu wa sheria awadanganye wajinga, zile za posho alisema hatapokea mara atapelekea kwenye NGO yake huko Kigoma, muulizeni ziko wapi? NGO yake ilipokea ngapi? Mnafiki sana huyu
acha kujivua ufahamu.
kumbe ndo maana tunapishana mkuu, wewe unajua analipwa kiharamu sawa, ila jua alistaafu kwa kujiuzuruLowasa analipwa isivyo halali na huo nao ni ufisadi.Kwani alistaafu lini
ingekuwa mnafata katiba mpaka sasa hadi mbowe ashfukuzwa kwa mujibu wa katiba maana kaivunja na kujiongezea mda. ko barua ya ZZK aliandikiwa lini na naniZito alifukuzwa kwa mujibu Wa katiba ya CDM
kwani penshani anapewa nani, je huyu mbunge wa mwanza aliefariki (r.i.p) is no longer MP ko familia yake haistahili pensheni hahahahhahaBut my understanding is ZZK is no longer an MP, anapeweje pension
Kama hachukui hiyo 'ziada' atawezaje 'kuipeleka' huko anakodai ataipeleka (bila kuichukua)?
Amesema malipo ya ziada hatachukua...atachukua stahili yake...na hapo hapo akasema ziada atapeleka Ocean Road na huko Kigoma kujenga bweni. Siyo habari ya kusema hana ziada...amesema ziada ataitoa msaada, na wakati huo huo akiwa amesema hataichukua. Soma uelewe.Kwa hiyo kama mtu hana ziada anakuwa hana kitu kabisa!!!???
Zitto, anasema atachukua zile anazostahili kwa mujibu wa sheria , sasa yeye ambazo hastahili ni ngapi? Vipi kuhusu posho ya kukaa ambayoalisema aliacha kuchukua , mbona aliendelea kuchukua ?
Matusi/maneno ya kashfa na kejeli hayakujengi mwana JF; badala yake yanakufanya uonekane kuwa u-mvivu wa kufikiri. Badilika!
Amesema malipo ya ziada hatachukua...atachukua stahili yake...na hapo hapo akasema ziada atapeleka Ocean Road na huko Kigoma kujenga bweni. Siyo habari ya kusema hana ziada...amesema ziada ataitoa msaada, na wakati huo huo akiwa amesema hataichukua. Soma uelewe.
Muulize HUYO ZZK katumia pesa ngapi za Mbowe alipokuwa pale UDSM na kugombea ubunge Kigoma kaskazini na katumia vifaa vingapi vya chadema kama helcopter na vinginevyo. Halafu google upate taarifa za Mbowe kafanya nini HAI bila kufilisi shirika lolote la UMMA kama nalivyofanya yeye kuishinikiza NNSF kuingia mkataba na kampuni yake
By Zitto,
.............
Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.
......................
Source: His facebook page.
Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.
Ziada inatokana na matumizi yake sio uelewa wako au wangu anaweza pewa shilingi mia tu akatumia sabini thelathini ikabaki na hiyo akaiita ziada akatoka huko alikotaja . . . .. .ziada ya mtu anaijua mwenyewe. . . .
Aseme anazostahili kwa mujibu wa sheria ni ngapi? Mbona yeye analipwa wakati alifukuzwa kwenye chama chake na kuukosa Ubunge ? Mbona mpaka leo akina Danny Makanga na Erasto Tumbo , tangu walipofukuzwa UDP hawajawahi kulipwa mafao yao ? yeye analipwakwa utaratibu upi?
Soma uelewe, acha kujitoa ufahamu Zitto hazungumzii ziada ya matumizi yake. Anazungumzia ziada kwenye mafao. Amesema ziada ya kile anachostahili, siyo ziada ya matumizi yake. Fuatilia suala hili kwa kumaanisha utaelewa. Kabla ya kufanya hivyo, usinijibu. Kama ungekuwa unafuatilia masuala haya japo kwa kusikia tu mtaani, usingeshindwa kulielewa hili. napoteza muda kujadiliana na mtu aliyeamua kujifanya kipofu huku macho anayo.