Zitto akataa posho ya mil. 238

Zitto akataa posho ya mil. 238

Kina Mbowe, Lema, Mnyika, kuchukuwa milioni 230 kila mmoja na kukaa kimya siyo wanafiki?

Si kila anayefanya mambo ya muhimu katika jamii kama kutoa misaada anaita media ili apate coverage ya kumpatia max za wananchi, ukifuatilia habari za chinichini utakuta wengine pia wanafanya makubwa bila kujitangaza.
Nilifikiri jamaa yako hatapokea kabisa, kumbe atapokea ila anaelekeza atakachofanyia, ukimfatilia mpaka mwisho si ajabu ukakuta wala hatofanya kama alivyotangaza
 
  • Thanks
Reactions: Pai
Mtu anieleze kifungu kinachosema mbunge atajiuzulu ubunge kwa kukufukuzwa uanachama na chama chake-Ila kipo kinachosema atakoma kuwa mbunge najua bado kuna watakaoshindwa kuelewa hapa
 
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.


Huyo Zitto mwnyew ameiga na bado hajapatia Nassari yy aliuza gari la kibunge akanunua ambulance mbili. Mtoa mada uache ushabiki wa uco na maana
 
Kwan tafsiri ya kupokea ziada ya 230 ni ipi?? Kwamba ikitokea wamzidisha ndipo anapokea au hyo ndiyo ziada kwa maana tayar alishachukua chake??
 
Kina Mbowe, Lema, Mnyika, kuchukuwa milioni 230 kila mmoja na kukaa kimya siyo wanafiki?
Kuna hela wanalipwa wabunge, wafanyakazi wa umma isiyokuwa katika sheria na stahili na hasa ya kiinua mgongo?
 
Ndo maana hakuna maendeleo fedha nyingi ni posho tuuu.
Kwa nini walipwe mahela mengi namna hiyo?

Kwa nini hayo mahela yasitumiwe kwenye mambo mengine yaliyo muhimu zaidi kuliko matumbo ya hao wabunge?
 
Usanii wa kiwango cha chini kabisa huo. Uliwahi kukataa posho bungeni kumbe lengo lako lilikuwa kuwaingiza wapinzani wengine mkenge. Cha ajabu ulitangaza kukataa posho kumbe nyuma ya pazia ukiwa katika kamati yako ya pac ulikuwa unachukuwa posho mara mbili.

Pia ulikuwa na ile jeuri ya fedha ulizokuwa unatumiwa Ujerumani na wanaokupa kazi ya kuharibu upinzani. Cha ajabu kabisa unakuja na porojo na ulaghai ule ule kwa watu walewale kwa matumaini kuwa utaaminika? You can fool some people some time but you will never fool all the people all the time. Aibu yako na yaliyokukuta Tunduma ni mwanzo tu wa yatakayokukuta mbele ya safari.
 
Kina Mbowe, Lema, Mnyika, kuchukuwa milioni 230 kila mmoja na kukaa kimya siyo wanafiki?

Na akina Pinda, Lowasa, Riz1, January, Mwigulu .................. same boat!! I love this country!!
 
huwa siamini kabisa kauli za Zitto ni za kinafiki
 
Last edited by a moderator:
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.


Zitto halishafukuzwa na CDM kwa makosa mbalimbali,kapoteza haki zake zote
 
Kwan tafsiri ya kupokea ziada ya 230 ni ipi?? Kwamba ikitokea wamzidisha ndipo anapokea au hyo ndiyo ziada kwa maana tayar alishachukua chake??

Hiyo kama ipo kihalali ataipokea ya kwake, ila kama ipo inayozidi hapo ndio itaenda Ocean Road
 
Hapo hujaelewa jambo moja;
1. Atapokea

2. Inayozidi zaidi atachangia bweni na hospital

Hajasema hatapokea.

Kwani wabunge wengine hawatatoa misaada kwa jamii? Je, uzalendo ni upi hapo? Tusidanganyane tafadhali
 
sasa hayo mamilioni ya nini wakati yeye sio mbuge.........tunamjua huyo anasura mbili
 
... Pesa Zipo Kihalali Hizo Siyo Za Wizi, Zitto Amezoea Za Kimyakimya Yaani Za Wizi
 
... Mbna Mwandiga Imemshinda? Kama Kweli Yeye Mzalendo Atuletee Maendeleo Hapa Mwandiga, Si Bora Angezipokea Then Akanunua Ambulance Kwaajili Ya Kina Mama Wa Kalinzi. Huyu Jinga Kweli.
 
Back
Top Bottom