Mkuu
Quraan ni somo lenye fani zaidi ya moja
Mfano mdogo
Aya ulizozituma,Ni aya kamili katika Quraan,ila hazifanyi kazi kihukmu,
Tazama mtiririko huu Chief
1)Kuna aya husomwa na hufanya kazi kihukmu
2)Kuna aya husomwa,lkn hazifanyi kazi kisheria
3)Kuna aya haipo ndani ya Quraan(haisomwi)lkn inafanya kazi kisheria
4)Kuna aya haipo ndani ya Quraan(Imefutwa)na haifanyi kazi kisheria
Na haya yote
Yalitokea zama za Mtume wa Allah sala na salamu ziwe juu yake kwa amri ya Mola
Unaweza kuuliza
Kwann zinafutwa?!
Jawabu
Quraan ilishuka taratibu ndani ya miaka 23 kwa matukio mbalimbali na ukumbusho au maonyo na makemeo,Ushukaji wake,kulingana na hali za watu kwa wakati husika.
mfano
Pombe iliharamishwa ndani ya awamu tatu.
Awamu ya kwanza
Ni Hii
يَسْأَلونَكَ عَنِ الْخَمْرِ وَالْمَيْسِرِ قُلْ فِيهِمَا إِثْمٌ كَبِيرٌ وَمَنَافِعُ لِلنَّاسِ [البقرة:219]
Wanakuuliza kuhusu Pombe na Kamari,Waambie,ndani ya Pombe na Kamari kuna madhambi makubwa na manufaa kwa watu
Aya hii,haikuja moja kwa moja kuharamisha,Bali ilikuja kutoa tahadhari tu
Aya ya pili
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لا تَقْرَبُوا الصَّلاةَ وَأَنْتُمْ سُكَارَى [النساء:43].
Enyi Walioamini,msiikaribie swala hali ya kuwa mmelewa(mmekunywa Pombe)
Aya hii
Ikaja kuharamisha kipindi tu cha Swala,mbali na swala,baadhi walikuwa wanaendelea kunywa
Aya ya tatu
يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّمَا الْخَمْرُ وَالْمَيْسِرُ وَالْأَنْصَابُ وَالْأَزْلامُ رِجْسٌ مِنْ عَمَلِ الشَّيْطَانِ فَاجْتَنِبُوهُ لَعَلَّكُمْ تُفْلِحُونَ [المائدة:90].
Enyi mlioamini,Hakika mambo yalivyo,Pombe na Kamari na Na Ibada ya Masanamu na Ramli,ni shari/chukizo katika miongoni mwa matendo ya Shetani,Basi jiepusheni nayo,ili mpate kufaulu
Aya hii ya tatu
Imekuja moja kwa moja Kuharamisha,zikabaki aya mbili za mwanzo,kuwa ni zenye kusomwa tu bila kufanyiwa kazi kisheria
Huu ni mfano tu Mkuu
Turudi nyuma
Aya ulizozituma,zimebaki kusomwa tu bila kufanyiwa kazi kisheria
aya iliyokuja na kufuta hukmu za aya mbili ulizozituma ni hii kwa mtu asie kuwa na Mke ni hii au Mume(akafanya dhambi ya zinaa)
الزَّانِيَةُ وَالزَّانِي فَاجْلِدُوا كُلَّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا مِائَةَ جَلْدَةٍ [سورة النور: 2
Mzinifu Mwanamke na Mzinifu Mwanaume,Wapigeni viboko kila mmoja miongoni mwao,viboko mia moja....
Ama aya kuhusu kupigwa mawe mpaka kufa,ni kwa wale ambao wameoa au kuolewa
Aya hii imefutwa kusomwa,imebaki Hukmu
aya ni hii
الشَّيْخُ وَالشَّيْخَةُ فَارْجُمُوهُمَا الْبَتَّةَ نَكَالًا مِنَ اللَّهِ وَاللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
Mtu mzima mzifu(Mwanaume alieoa) na Mtu mzima mzinifu(Mwanamke alieolewa),Wapigeni mawe moja kwa moja(mpaka kufa),Adhabu itokayo kwa Allah,Na Allah ni mwenye nguvu mwenye hukmu
Ikadhabiti hili kutoka kwa Mtume wa Allah,kwa kuwaadhibu wazinifu kwa aina zao
Mkuu
Nataraji utakuwa umenielewa angalau kwa uchache
Shukran sana
Nakaribisha masahihisho kwa ndg zangu
na kama kuna swali,naomba liulizwe,in sha Allah tutajaribu kulijibu ikiwa tuna elimu nalo
Sent using
Jamii Forums mobile app