Zilipendwa za redio RTD

Zilipendwa za redio RTD

Dingi alikuwaaga mnoko, saa 3 usiku anafunga mlango watu wote walale, ukichelewa nje utajutia. Hivyo alama yetu ya kukaribia saa 3 ni music unaowekwa wa kuashiria kuanza kwa kipindi cha MAJIRA saa 2.45 usiku, ukisikia music huo utakimbia ufe ili kuwahi geti lisifungwe kabla yako kuingia.
 
Dingi alikuwaaga mnoko, saa 3 usiku anafunga mlango watu wote walale, ukichelewa nje utajutia. Hivyo alama yetu ya kukaribia saa 3 ni music unaowekwa wa kuashiria kuanza kwa kipindi cha MAJIRA saa 2.45 usiku, ukisikia music huo utakimbia ufe ili kuwahi geti lisifungwe kabla yako kuingia.
Ma jira kilikuwa kizuri sana

Fuatiwa na mazungumzo baada ya habari

Teh
 
Chei chei shangazi,mama na mwana,kombora-saa 11 asubuhi.

Duh! Enzi hizo home hakuna tv ni Kaseti na redio ya mkulima,Kaseti una isikiliza weekend tena kama baba kanunua betri mpya,
Ila maisha yalikua mazuri kipindi hicho sikosi kipindi cha watoto wetu na kipindi cha mama na mwana, Siwezi kumsahau Debora mwenda (shangazi) alivyo kuwa makini kutu hadithia hizo hadithi episode baada ya episode,
Mungu ambariki huko Alipo.
 
Na kipindi cha Afya kinaanza na wimbo wa "Kuleni Kuku mayai mboga samaki maziwa,kuleni chakula bora cha kujenga muili na kujenga nyumba safi pa kulala pawe bora"

Pia Mshamu alikuwa noma,halafu mzee Mundu mbishi kupindukia full mfumo dume! kuna akina Sijali ,Havijawa! Siwema binti mtayaona hadi raha!

Charles Hillary, mambo mpwito mpwito, mama Sarah Dumba - mama na mwana enzi hizo - RTD
 
Kulikua na TANGAZO LA DAWANOL
"Mgongo wangu waniuma maumivu teeleee, dawa ya maumivu dawa yenye nguvu dawa ni dawanol,

Tangazo la IPP : "Ah! mama Mariam vipi?"....."Hizi nguo dadaangu, nimetumia kila aina ya sabuni lakini bado tu hazitakati!!" "Si utumie Komesha?" Kulikua na sabuni iliitwa Komesha,

Sintamsahau Michael katembo alikuwa na kipindi kinaitwa "Mbiu ya mikoa"
Hapo zinapigwa ngoma asilia za kila mkoa.
 
Ilipoanza sabasaba " wanashinyanga ngw'eji gwashiga gw'ilegebishe ugulema wa kisasa balemi ngw'angaleli kwanza amalale mgab'eje"


Huu wimbo nimepiga watoto wa wazaramo sana maana walikuwa wananitania sana maana ndo nilikuwa nimeingia jiji nikitokea bara na kiswhili cha kisukuma


Aki ya Nani watani wangu mlipo kunyweni ,kuleni nakuja kulipa

Teh
 
Ilipoanza sabasaba " wanashinyanga ngw'eji gwashiga gw'ilegebishe ugulema wa kisasa balemi ngw'angaleli kwanza amalale mgab'eje"


Huu wimbo nimepiga watoto wa wazaramo sana maana walikuwa wananitania sana maana ndo nilikuwa nimeingia jiji nikitokea bara na kiswhili cha kisukuma


Aki ya Nani watani wangu mlipo kunyweni ,kuleni nakuja kulipa

Teh
Hahahaa! Mkuu hiyo ilikua ni mwaka 1987 ilipofanyika sabasaba kitaifa mkoani Shinyanga mgeni rasmi akiwa president Ali Hassan Mwinyi.
 
Kulikua na TANGAZO LA DAWANOL
"Mgongo wangu waniuma maumivu teeleee, dawa ya maumivu dawa yenye nguvu dawa ni dawanol,

Tangazo la IPP : "Ah! mama Mariam vipi?"....."Hizi nguo dadaangu, nimetumia kila aina ya sabuni lakini bado tu hazitakati!!" "Si utumie Komesha?" Kulikua na sabuni iliitwa Komesha,

Sintamsahau Michael katembo alikuwa na kipindi kinaitwa "Mbiu ya mikoa"
Hapo zinapigwa ngoma asilia za kila mkoa.
Komesha nimezitumia sana

Tumbo tamimu risasi

Teh
 
Hahahaa! Mkuu hiyo ilikua ni mwaka 1987 ilipofanyika sabasaba kitaifa mkoani Shinyanga mgeni rasmi akiwa president Ali Hassan Mwinyi.
Waliniacha hoi waendesha malori ya kubeba pamba yaliyokuwa yakijulikana DAF

Yaani ndugu walisondeka mpaka juu na maboi wako hukohuko juu gali inanesa upande upande

Kweli yalikuwa maonyesho si mchezo

Teh
 
Bima yako,IPP hewani,Jenga na Mecco,Mtaalamu wetu,ushirika,Shirika la Posta na Simu,Sukita,nimekumbuka hivyo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom