Zilipendwa na visa vyake..

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,434
7,055
Muziki wa zamani ulikuwa na burudani ya aina yake. Mbali ya utunzi mahiri na uimbaji hodari, nyimbo nyingi zilitungwa kuelezea visa na mikasa iliyowahi kuwakuta wasanii husika.

Kupitia uzi huu tutakumbushana nyimbo mbalimbali ambazo zinasimulia visa hivyo vilivyowasibu ndugu zetu hawa. Lol!

Kwa heshima ya Jabali la Muziki, Marijani Rajab (RIP), nitafungua njia kwa kuelezea yaliyomkuta mpaka akatunga wimbo wake maarufu uitwao Aisha kama nilivyokuta ikisimuliwa na wadau fulani.

Ilikuwa hivi;

'Marijani alitembelea Mwanza, akakutana na kipusa Aisha. Binti mzuri, mtanashati wakati huo anatingisha Jiji la Mwanza.

Jabali la muziki akakolea, ikabidi binti akamuahidi Jabali kuonana nae Dar es Salaam.. Wakapanga siku ya kukutana pale Keys Hotel, barabara ya Uhuru, karibu na Mnazi Mmoja. Wakati huo Keys Hotel ndio ilikuwa Hotel janja na ya wajanja..

Siku ya ahadi Jabali akafika mapema kumsubiri.. Alisubiri mpaka usiku hakutokea. Kesho yake akasema abahatishe wapi.. Ndio akaamua kumtungia wimbo huo.

Huyo dada anaishi Marekani sasa hivi na anakadiriwa kuwa na umri wa takribani miaka 60'.

Wimbo wenyewe ni huu hapa chini;


Unakumbuka kisa gani cha kweli ambacho kilitungiwa wimbo?
 
SASA NIMEHAMIA MTAA WA SABA, TOKA PALE NILIPOKUWA NIKIKAA ZAMANI..ILE NYUMBA SIO NYUMBA ILIKUWA NA MIKOSI
 
NAJUUUTA, NI KINDA LANGU LENYE RANGI YA CHUNGWA, MARINGO YAKE NA MWENDO VINANICHOSHA, NACHOKA KABISA

KINACHONISHINDA NYUMBANI KWAO WAMEZIDIA UKALI, NIFANYE NINI ILI WAPATE TULIA NACHOKA KABISA
 
NAJUUUTA, NI KINDA LANGU LENYE RANGI YA CHUNGWA, MARINGO YAKE NA MWENDO VINANICHOSHA, NACHOKA KABISA

KINACHONISHINDA NYUMBANI KWAO WAMEZIDIA UKALI, NIFANYE NINI ILI WAPATE TULIA NACHOKA KABISA
Jose usiandike mashairi tu. Kama una kisa chake kilichopelekea ukatungwa wimbo huo tuletee japo kidogo.

Ndio lengo la thread hii.

PS: Rangi ya Chungwa ni miongoni mwa classic songs!
 
Jose usiandike mashairi tu. Kama una kisa chake kilichopelekea ukatungwa wimbo huo tuletee japo kidogo.

Ndio lengo la thread hii.

PS: Rangi ya Chungwa ni miongoni mwa classic songs!
MKUU NIMEANDIKA HIVYO KWA SABABU BAADHI YA MASHAIRI YAMENITOKEA MIMI...(NAHUSIANISHA KIDOGO)

NB: SAMAHANI KAMA NIMEHARIBU LENGO LA UZI WAKO
 
MKUU NIMEANDIKA HIVYO KWA SABABU BAADHI YA MASHAIRI YAMENITOKEA MIMI...(NAHUSIANISHA KIDOGO)

NB: SAMAHANI KAMA NIMEHARIBU LENGO LA UZI WAKO
Sawa mkuu. Ni kweli umepishana kidogo na lengo la uzi ila pole sana kwa yaliyokusibu.
 
Namsaka mbaya wangu: by Marijani Rajabu.

Nilikuwa nikichonganishwa na Mpenzi wangu bila kujua kuna ki dudu mtu, nilipohisi kuna mtu anatia fitina, niliamua kumsaka mpaka nikaja kugundua ni rafiki yake wa karibu, Ndipo nilimtongoza kimyakimya akakubali. Siku nikampeleka gesti baada ya kumpigisha kilaji cha kutosha, nilipiga shoo ya kufa mtu, kisha nikamuandia sms Mupenzi, kwamba kila siku tunagombana kwa sababu ya huyu nilienae hapa gesti fulani na nikampa namba ya chumba. Alipokuja aliingia chumbani niliacha mlango wazi,.
Niliwaacha nyasi zikiwaka moto na mambo wakisawazisha.
 

Huu wimbo wa Maseke ya Meme (pembe za kondoo) ulibamba kunako baada ya kifo cha Bavon Marie-Marie (agosti 5, 1970). Bavon Marie ndie alikuwa mtunzi wa kibao hiki. Katika wimbo huu Bavon (ambaye alikuwa mdogo wa Franco, au Luambo Luanzo Makiadi) iliaminika kuwa alitabiria kifo chake. Hadithi zilizagaa kuwa alirogwa na kaka yake ambaye hakupendezewa na mdogo wake kuingia kwenye muziki. Nakumbuka enzi hizo ndio nipo kidato cha pili na masikitiko yalikuwa makubwa sana. Ilikuwa si miaka mingi imepita baada ya kifo cha mwanamuziki mwingine aliyetingisha anga za Tanganyika, Salum Abdallah.
 
Namsaka mbaya wangu: by Marijani Rajabu.

Nilikuwa nikichonganishwa na Mpenzi wangu bila kujua kuna ki dudu mtu, nilipohisi kuna mtu anatia fitina, niliamua kumsaka mpaka nikaja kugundua ni rafiki yake wa karibu, Ndipo nilimtongoza kimyakimya akakubali. Siku nikampeleka gesti baada ya kumpigisha kilaji cha kutosha, nilipiga shoo ya kufa mtu, kisha nikamuandia sms Mupenzi, kwamba kila siku tunagombana kwa sababu ya huyu nilienae hapa gesti fulani na nikampa namba ya chumba. Alipokuja aliingia chumbani niliacha mlango wazi,.
Niliwaacha nyasi zikiwaka moto na mambo wakisawazisha.
Hivi ni kwamba hamjaelewa lengo la uzi au mnafanya makusudi tu?

Ila kisa chako kimenichekesha sana. Wewe ni kauzu zaidi ya dagaa
 
Marijan Rajab alikuwa bright sana ila ilikuwa ngumu kwa wengi kumwelewa, Kuna mwaka sikumbuki ni waziri gani aliwasilisha bungeni kusudio la kuandika kitabu juu yake ikiwa ni hatua ya kuenzi kazi zake, personally huwa namchukulia kama mwalimu aliyefundisha wengi pasipo yeye kujijua.
 
Muziki wa zamani ulikuwa na burudani ya aina yake. Mbali ya utunzi mahiri na uimbaji hodari, nyimbo nyingi zilitungwa kuelezea visa na mikasa iliyowahi kuwakuta wasanii husika.

Kupitia uzi huu tutakumbushana nyimbo mbalimbali ambazo zinasimulia visa hivyo vilivyowasibu ndugu zetu hawa. Lol!

Kwa heshima ya Jabali la Muziki, Marijani Rajab (RIP), nitafungua njia kwa kuelezea yaliyomkuta mpaka akatunga wimbo wake maarufu uitwao Aisha kama nilivyokuta ikisimuliwa na wadau fulani.

Ilikuwa hivi;

'Marijani alitembelea Mwanza, akakutana na kipusa Aisha. Binti mzuri, mtanashati wakati huo anatingisha Jiji la Mwanza.

Jabali la muziki akakolea, ikabidi binti akamuahidi Jabali kuonana nae Dar es Salaam.. Wakapanga siku ya kukutana pale Keys Hotel, barabara ya Uhuru, karibu na Mnazi Mmoja. Wakati huo Keys Hotel ndio ilikuwa Hotel janja na ya wajanja..

Siku ya ahadi Jabali akafika mapema kumsubiri.. Alisubiri mpaka usiku hakutokea. Kesho yake akasema abahatishe wapi.. Ndio akaamua kumtungia wimbo huo.

Huyo dada anaishi Marekani sasa hivi na anakadiriwa kuwa na umri wa takribani miaka 60'.

Wimbo wenyewe ni huu hapa chini;


Unakumbuka kisa gani cha kweli ambacho kilitungiwa wimbo?



Umenikumbusha miaka ya 1990 kuna msikilizaji mmoja wa redio aliambiwa achague wimbo achezewe kusindikiza salaam zake, akamwambia mtangazaji apigiwe Revola revola Revola, ifahamike hili lilikuwa ni tangazo la biashara ya sabuni
 
Huu wimbo wa Maseke ya Meme (pembe za kondoo) ulibamba kunako baada ya kifo cha Bavon Marie-Marie (agosti 5, 1970). Bavon Marie ndie alikuwa mtunzi wa kibao hiki. Katika wimbo huu Bavon (ambaye alikuwa mdogo wa Franco, au Luambo Luanzo Makiadi) iliaminika kuwa alitabiria kifo chake. Hadithi zilizagaa kuwa alirogwa na kaka yake ambaye hakupendezewa na mdogo wake kuingia kwenye muziki. Nakumbuka enzi hizo ndio nipo kidato cha pili na masikitiko yalikuwa makubwa sana. Ilikuwa si miaka mingi imepita baada ya kifo cha mwanamuziki mwingine aliyetingisha anga za Tanganyika, Salum Abdallah.
Asante sana kwa kumbukizi murua mkuu.
 
Kuna hidaya mmoja pale chuganian alizua tafrani kwa mCongolese mmoja
Akaapa lazima arudi kumsaka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom