Butola
JF-Expert Member
- Jan 19, 2010
- 2,290
- 763
Cheo cha makamu wa rais hakiwezi kufutwa yeye ni rais wa akiba. Kumbuka ikitokea rais aliko madarakani ameshindwa kufanya kazi na kuachia ngazi makamu wa rais ndiye anakuwa rais na kumalizia kipindi cha miaka mitano. Hii ni kwa mujibu ya katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ibara ya 37.5
Haijalishi katiba ya sasa inasemaje lakini je kuna umuhimu kweli wa kuweka cheo kikubwa hivi lakini kisicho na mamlaka yoyote ya kiutendaji na kuishia kukatakata tu vitambaa?hapana mkuu!!
Ndio maana Dr. Shein aliamua kuachana na Umakamu wa Rais na kugombea Urais wa Zanzibar japo ki-protocol ni cheo kidogo kuliko cha Makamu wa Rais, hiki cheo kwa namna kilivyo sasa kinamfanya Makamu wa Rais autumie muda wake mwingi ofisini kusoma magazeti tu.