Ziara ya dr. Bilal (Mbeya) yadoda

alichoifanya secta ya elimu ya juu hakitasahuliwa, wakati huo alitoa mikopo na hela za kujikimu kwa wanafunzi wa zanzibar huku akiacha wa bara wnaandamana na kuhaha ovyo[/QUOTE]
Hapo kwenye red, unajua kama una nia mbaya utabaki na nia hiyo wewe tu, kama angekuw ambaguzi mbona ndiye ana rejkodi ya kuw awqaziri kiongozi wa kwanza kurejea kufundisha chuo kikuu na akaamua kufundisha Dodoma? Kwani Zanzibar hakuna vyuo? Tena, ziara yake Mbeya haikuwa ya mikutano ya hadhara mbona hilo hamtaki kulifahamu, aliyeweka picha ana maana yake lakini Dr Bilal alifanya kazi aliyotakiwa kuifanya Mbeya kwa mafanikio na kumaliza na kurejea kusimamia shughuli nyingine za serikali ikulu kama ambavyo anafanya hata sasa
 
ndo huyu bwana ..yaani ana midude miwili anaenda nayo kila mahali sasa sijui analalaje nao..wazeee hawa bwana

Kiongozi kuwa na busara na heshima nadhani hufai kuwa mtanzania kama unazarau wazee? Kijana huna nizamu hata kidogo mheshimu kwa umri wake na mafanikio ambayo amekuzidi
 
Ujua kuwa kichaa kunaanza taratibu, kama mtu alifatilia taarifa na alikuwapo Mbeya kabla Makamu hajaenda huko safari yake ilitangazwa rasmi nini majukumu yake. Hakuwa na mikutano ya hadhara wala ziara hiyo haikuwa ya maandamano kama CDM mlivyozoea. Ni wakati sasa kabla mtu hujaamka na hoja finyu utafakari kabla ya kuandika maana hapa Pinda kaenda Kagera mmeanza oooh anaenda kufuta cheche za CDM, CDM ni chama cha upinzani na hao ni viongozi kazi yao ni kutazama maendeleo na sio kupiga maneno. MY TAKE: Nawashukuru wananchi wa Mbeya kubakia wakifanya kazi zao za maendeleo maana maendleo hayaji kwa maandamano ama mikutano ya hadhara bali kufanya kazi kwa saa nyingi na kujituma.

You are just confusing us!
 
huyu mzee mi namuoneaga huruma tu sijui kwa nini ...yaani mara mia shein ....yani yuko kibwege ***** tu
 
Mr. Oyoyoo jana nilishindwa kukujibu ujumbe wako kutokana na mgao wa umeme. Ziara ya Makamu Wa Rais Dr. Mohamed Gharib Bilal ilitanganzwa mtaa kwa mtaa katika jiji la Mbeya kwa muda wa siku mbili asubuhi na mchana, tangazo lilikuwa linawataka wananchi wajitokeze kwa wingi kumpokea mheshimiwa huyo katika uwanja wa ndege bila kukosa. Katika uwanja wa ndege ambao mimi nilienda kumpokea kwa kutumwa na ofisi nikiwa na gari ya ofisi. kwa hiyo ninachokisema na ninachokiandika ni cha kweli. Sina muda wa kuandika uongo na ukizingatia mimi ni graduate. Kwa mfano kama ziara hiyo ingekuwa ni ya Dr. Slaa kuja Mbeya kufungua Ofisi ya CDM Mkoa watu katika uwanja wa ndege wangekanyagana. Tuache ushabiki, tujadili uhalisia.
 
Hapo ni bada ya kutangaza kwa siku mbili ujio wake na magari tofauti kwenye kona za jiji
Nilikuwepo mjini mimi,matangazo ya siku ya kuja yaliendelea mpaka muda mfupi kabla ya jamaa kufika
Ana haki ya kulakiwa na hao waliojitokeza baada ya gharama kubwa ya kumtangaza,ila nawaambia wanajamvi kama ni kulinganisha nani anakubalika zaidi kati ya CCM na CHADEMA subirini siku SLAA atakapoingia Mbeya
 
Hao kwenye picha kila mmoja kalipwa kiasi gani,
maana nasikia kwa hapa kwetu ni kuanzia 40000,
embu tupashe!
 
Ujua kuwa kichaa kunaanza taratibu, kama mtu alifatilia taarifa na alikuwapo Mbeya kabla Makamu hajaenda huko safari yake ilitangazwa rasmi nini majukumu yake. Hakuwa na mikutano ya hadhara wala ziara hiyo haikuwa ya maandamano kama CDM mlivyozoea. Ni wakati sasa kabla mtu hujaamka na hoja finyu utafakari kabla ya kuandika maana hapa Pinda kaenda Kagera mmeanza oooh anaenda kufuta cheche za CDM, CDM ni chama cha upinzani na hao ni viongozi kazi yao ni kutazama maendeleo na sio kupiga maneno. MY TAKE: Nawashukuru wananchi wa Mbeya kubakia wakifanya kazi zao za maendeleo maana maendleo hayaji kwa maandamano ama mikutano ya hadhara bali kufanya kazi kwa saa nyingi na kujituma.
kama ccm wanacmamia hilo mbona maendeleo hatuna?
KK
 
Back
Top Bottom