Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huu wakupelekeana zawadi kila mtu aone umetowa nini umepewa nini, ni umwanjomwanjo. Enzi zetu, ilkuwa hakuna huu upuuzi, maoana kwisha, anaekultea zawadi anakuletea kwako na si kwenye maholi. Mwenye gunia debe la karanaga, mwenye debe la maharage, mwenye gunia la dagaa, mwenye mkeka mwenye mbuzi, mwenye msala, mwenye jamvi, Haya. Anakuletea nyumbani na unaziona hapo hapo na unajuwa nani kakuletea nini. Hakuna sijui zimefungwa makaratasi sijui nini, ngoja tu kuna siku watu watapelekewa vichwa vya watu ndio mchezo utakwisha!
kuna maharusi walipokuja kufungua zawadi zao wakakuta kuna zawadi moja ina hirizi ambayo kwa maelezo yao ilikuwa inapumua, wakaita watu na kuipeleka kwa mchungaji, wakafanya maombi na kuishia kuichoma moto. Maharusi raha ya ndoa imepotea tena. Kwasasa wanajaribu kuangalia mkanda wa video wakati wa zawadi ili wajue nani aliyetoa ile zawadi.
Haya jamani wale masingle kuweni makini na zawadi za harusi siku ya harusi yako.
Haha... Miaka gani hiyo. We kumbe mzee kweli.. Loh!
Hakuna uzee wala ujana hapo, wewe uletewe uma, vijiko, visu vya kulia wakati kila siku unapika bada, inahusu nini? si bora mtu akuletee zawadi ya n'gonda. Tena nyumbani, sio kwenye hall, ujuwe haswa imeletwa na nani?
Mie Harusi yangu Mzee Ndesamburo alileta mbuzi 6 nyumbani, huyu Mzee wenu wa Magwanda. Hizo ndio zawadi. Msishangae! Marehem baba'ke Gozi langu walikuwa ni marafiki wakubwa na huyu mzee wetu.