Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Status
Not open for further replies.
sawa hawa majamaa wanatutenga sana wakristo sasa funga yenu as tusile mnatusumbua
 
Kwaio kama ni 90% wanawanyima wakristo uhuru kama ndo hivo watangaze serikali ya mapinduzi Ina dini.
Hizi sheria hazikuanza leo wala jana,ni sheria ambazo wengi wamezikuta.Wakristu wa zanzibar miaka nenda miaka rudi wanaziheshimu hizi sheria,nazungumzia wa wazawa wa Zanzibar.

Matatizo makubwa wanayoyapata Wazanzibari nyakati hizi ni kutoka kwa wakristo wageni wahamiaji wanaohamia Zanzibar,Wakrito wageni wanaohamia Zanzibar katika nyakati hizi ufahamu wao mdogo kuhusu itikadi na utamaduni wa wenyeji wa Zanzibar.

Wakati fulani Wanzibari wailslamu walikuwa wanasherehekea Xmas na wenzao Wakristu,Na wazanzibari wakristu walikuwa wanahudhuria shuhuli za kisilamu zinazaofanywa na wenzao waislamu,ndio maana ukaja msemo "zanzibar njema atakae aje",ilkuwa kama pepo ilioko duniani..

Masikitiko makubwa,Wakati huo hauko tena Wazanzibari ambao wako kama milioni moja laki tano(1,500.000),asilimia tisini na tano (95%)ni wailamu,wameanza kuogopa,kutoka na fikra za wenzao wakristo zinazoletwa na wakristo wasio wenyeji wa zanzibar ambao wanaitikadi kali za kidini...

Wanzibari wameanza kuwa woga,wameanza kuwa na siasa kali za kidini,hili jambo jipya zanzibar, na kwa wazanibari,kumbuka Ukristo ulianzia Zanzibar ndio ukafika Tanganyika,,wazanzbari inabidi waunge mkono mashekhe wenye siasa kali za kidini(extremisim) kutokana na woga wao,Woga unaosababishwa na mtu kama alieleta hii mada(huu uzi)...

Askofu Hafidh ni mmoja wa maskofu mzawa wa zanzibar,aliunga mkono sana Zanzibar iwe na mamlaka kamili,kwa kuogopa siasa kali wanazokuja nazo wakristo wenzano kutoka Tanganyika. Kwanini hatuwaachi tu wazanzibari wakaamua wanachokitaka kutokana na mila tamaduni zao,kwanini iwe issue....tafakari
 
Fuoni Lodge watu wanakula na kunywa tuu kama kawa Ramadhani inawahusu waislamu waliofunga tuu wengine acheni tufanye yetu
 
Fuoni Lodge watu wanakula na kunywa tuu kama kawa Ramadhani inawahusu waislamu waliofunga tuu wengine acheni tufanye yetu

Ukidakwa wanakupeleka 'Chuo cha Mafunzo'[emoji12][emoji12]
 
🙂 🙂 mtu anayeishi z'bar kama siyo mtu wa dini ni sawa na kuishi jangwani tu, hizo sheria zao ziishie huko huko, huku kwetu kuna msemo "mdomo wangu usinipangie muda wa kula"
 
Hakuna Mwenye haki zaidi ya mwenzake TANZANIA haina DINI, ila watu wake ndiyo wanadini, acha nifanye yangu ambayo sivunji sheria za NCHI yangu,,,,,,,,, tukianza hivyo mwishowe lazima wanaokuja huku ZENJI wawe waislamu tu,,,,,,
Tanzania haina dini ila ZANZIBAR WANA DINI.. waacheni na mambo yao bhana kila kitu mnataka muwapangie?? Acheni uku.ma wenu... Ss wabara tuna matatizo sana.. sasa Zanzibar wewe kwenu?? Hata hao wakristo ni wahamiaji kule tena kutoka bara.. hasa askari ndio wamejaza ila wenyewe ni waislamu zaidi.. Usiingilie mipaka yao.. ndio maana hata magufuli akienda huko huwa mpole maana hana mamlaka kamili ndani ya zanzibar hasa ya kisheria na utawala... ndio maana wao wana jaji mkuu wao.. wana spika wao na rais wao...
 
hawa watu wanakuaga kama wendawazimu kipindi cha mfungi Muda wa kufungua ukifika anakula chochote popote
Mkuu kufunga ina umuhimu sana katika mwili wako,wakristo walio wakristo wa kweli na wao wanafunga,umeshawahi kwenda hospitali ukambiwa usile kwa masaa fulani,ndio upate matibabu..

Unajua kwanini unaambiwa usile kabla ya matibabu.....,kama hujui fanya research ingia kwenye Google utapata jibu...
 
Sasa kama kila dini kuheshimu dini nyingine, kwanini waislamu nao wasile kama wakristo ili kuheshimu ukristo, mbona wao wanakula hadharani wakati ya kwaresma? Huyu kiongozi atakua na vyeti feki.
Kabla ya kuwaambia waislam wasile kipindi cha kwa resma,anza kwanza kuwaambia wakristo wenzio kama wasabato,kkkt wote wafunge.
Ukifanikiwa hilo ndo uwataje waislam
 
Lakini ni suala ambalo lipo wazi kabisa hata waziri mkuu mstaafu Pinda Kayanza aliwahi kulitolea ufafanuzi, zaidi ya 90% ya wakazi wote ni waislamu..so hapa tunatekeleza tu 'wengi wape'...sidhani kama ni udini!
Mbona Waislam ni asilimia ndogo Marekani lakini wanadai wanataka haki zao

Uislam ni udicteta halisi
 
Hivi wewe ukiwa umefunga nami nakula chakula changu hadharani inakuuma nini....!!?? Hivi ina maana wakristo huwa hatufungi?? Mbona tunaishi na nyie vizuri...
Hata kama mfanyakazi wako wa ndani kama siyo muislam mpe uhuru ale kwa muda wake... Wewe uliyefunga uko na Mungu wako... Kumnyima uhuru mwenzio kisa umefunga hain maana... Na mfungo wako ni batiri...
Hajakatazwa mtu kula bali usile hadharani, kula ndani kwako
 
Asiekubaliana na hilo asiende Zanzibar mpaka mfungo uishe...OVERrrrr
 



Chanzo: Habari Leo
=====================================
Nataka kujua kipindi kwa kwaresma mbona hawakutoa tamko hili.

Kwaio wakristo wawe wanajificha wakati wa chakula cha mchana.

Hapana naona kuna harufu ya udini kuanza Zanzibar.[/QUOTE]
kingne ni kuwa haya mambo hayawekwagi hadharani kiasi hicho kama alivofanya maana inakuwa inakela ..mfungo wa mwingne aumie mwngne..na ndo nasemaga waislamu wakifunga mji mzima utajua....mbna sie tunakuwaga wapole tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom