M'bang'ang'walu
JF-Expert Member
- Jul 18, 2015
- 631
- 437
Ibada ya funga ni ya mja na muumba wake. Serikali inashindwa kutimiza majukumu yake badala yake inaingilia kazi za mungu sasa.SMZ Msitishe watu,
1.kwanza Sheria hiyo haipo na haijawahi kuwepo isookuwa wakati wa utawala wa Karume wakati Zanzibar ikiendeshwa na " decree"
2. Simamisheni shughuli zote za utalii mkwezi mzima wa Ramadhan kuondokana na kuwatesa bure wasio kuwa na hatia.
SMZ na ofisi ya Mufti muwe wa kweli msiwee wanafiki. Kama kweli uislamu una kuumeni na kujua kuwa Maimamu ndio wenye wajibu na Mamlaka ya kuwaelemisha umma kuhusu Mwezi mtukufu wa Ramadhani basi waachieni huru Maimamu wa UAMSHO na kurudi kuja kuwaamsha watu kuhusu maadili mema ya kiislamu.
Halafu kwani ibada ni kufunga tu? Kama wao wameamua kujipa majukumu ya kusimamia ibada kwa nini wasiweke hiyo sheria kwenye ibada nyingine, kwa mfano kila muda wa swala watu wote waingie misikitini. Na asionekane mtu yeyote barabarani au akifanya shughuli yoyote nyingine.
Watu wanajifanya wanapenda sana dini na mwenyezi Mungu wakati wao kwa madaraka yao wanatesa na kunyanyasa waislam wenzao kwa maslahi yao.