Usiupotoshe umma ndugu yangu, wanaokataa muungano huu feki sio kikundi cha uamsho tu, bali ni waZanzibari wengi kwa umoja wetu.
Uamsho na jumuiya za Kiislamu ni viongozi tu waliolivalia njuga suala hili ambalo kwa muda mrefu tukitegemea vyama vya siasa vitufanyie na vimeshindwa.
Kilichotokezea ni kiongozi mmoja wa Jumuiya ya Maimamu ambaye alikuwapo kwenye muhadhara pamoja na maandamano ya amani, alichukuliwa jioni hii toka msikitini na kupelekwa kituo cha polisi cha madema, polisi wakidai kwa ajili ya kumhoji.
Wafuasi akina sisi tulifika kwa wingi na umoja wetu pale kituoni, na maelfu ya watu tulokuwa pale tukitaka nasi sote waujumuishe kwenye hiyo issue, kwa maana ndio tuliofanya maandamano yake bila kusindikizwa na mtu, bali uzalendo na uchungu tu tulionao wa Zanzibar yetu. Hapo ndio polisi wakaamua kututawanya kwa mabomu ya machozi na risasi za moto hewani. Lakini hadi muda huu niandikapo hapa, bado tupo kwa umoja wetu na tunazidi kufurika hapa pahala.
Hatutasita na harakati zetu hadi Zanzibar yetu imerudi mikononi mwetu na siyo koloni la Tanganyika. Wengi wanotwita koloni letu, tumetawaliwa tunakubali kwa sasa, ila muda si mrefu tutajikombowa!!