Zanzibar NI Nchi-Samia Suluhu

Zanzibar NI Nchi-Samia Suluhu

Nyerere ndie nö 1 alieipoteza Tanganyika!
...
Akumbukwe kwa lipi?
Ivi unajua bila u..... Wa nyerere kusingekua na mivutano hii?
...
Dah! Naskitika sana nikiona mtu anaejiona anaakili timamu afu akaleta story za nyerere kuhusu muungano! Story zenyewe za kumsifia!
...
Wizi mtupu!

Acha wehu we mburula yule mkatoliki alikua na akili sana.Elim yako ya madrasa ndo iliyokupotosha na kuwaza kinyumenyume
 
Weye umetokea wapi tena?? Tanzania Bara ni nchi gani hiyo tena? Mbona mwatuchanganya nyie?? Na Tanzania ndiyo wapi huko tena?
Naona swali hilo ulipaswa kumuuliza Nape na mwenyekiti wake na mpango wao wa serikali mbili,Zanzibar na Tanzania.
 
inauma sana tunapelekwa kama hatuna akili vile

Kuna haja ya kuwa na muungano wa maridhiano kwani kila upande una haki ya kujiamulia mambo. Kusudi ya muungano ni umoja lakini hakuna umoja wa kusukumana.
 
hapoo ndipo ugomvi ulipo. Ukitaka kugombana na wazenji waambie hivyo tu. Muungano wa kweli ni ule ambao nchi zinapoungana inapatikana nchi moja tu. Sasa huu muungano wetu wa nchi moja kupotea na nyingine ikabaki mi siuelewi kabisa.

ndo hapo haya jamaa mguu nje mguu ndani.
 
Acha wehu we mburula yule mkatoliki alikua na akili sana.Elim yako ya madrasa ndo iliyokupotosha na kuwaza kinyumenyume

Dah! Bange za mchana mchana mbaya sana! Au umechanganya mavi ya ng'ombe?
...
Binadamu asie na akili ni nani?
Jee kunamwanadamu alietimia kiakili? Kama ni kweli, mbona nyerere na akili zake alishindwa kuendesha nchi na akamuachia Mwinyi?
...
Hivi karume alitaka muungano kwa mda gani? Mbona mpaka sasa tunao muungano!
Ni nani alieleta janja ya nyani kwenye muungano huu?
Ivi we tutusa unadhani bila ya ..... Wa nyerere leo tungeanza kuisaka Tanganyika?
...
Yaani sijui hata upo kijiji gani!
Na hata sijui kama unatambua kuwa nyerere ameshafariki!
Mpu.uzi no 1 Tz!
Na laiti tungekua na wapu.uzi kama wewe kumi tu! Sjui hatma ya Taifa letu ingekuaje!
Hem nisepe nisijibizane na kiazi!
 
[h=1]Daily Archives: April 20, 2012[/h][h=1]MAKALA: Muungano lazima uhojiwe[/h]
NA Bakari M. Mohamed
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ameiapisha Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Hatimaye tume hiyo itaanza kazi mwanzoni mwa mwezi Mei, 2012! Hata hivyo, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametahadharisha juu ya watu kuhoji Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Inaezekana kuna wasiwasi na kutokana na fununu zilizopo, kwamba sehemu fulani ya wananchi wameanza kuhoji "uhalali" wa muungano wetu kutokana na nyufa, songombingo na kero zisizoisha juu yake. Na wengi wanadhani kwamba mchakato wa Tanzania kupata Katiba Mpya ndio msingi wa kutatuliwa kwake! Hizi zote ni dhana katika kuelekea kwenye ujenzi wa muungano imara na unaozingatia uhuru na haki ya nchi mbili kwenye muungano.


Ni takriban miaka 48 sasa tangu Tanganyika na Zanzibar, nchi mbili huru na zilizokubalia (kwa kukosa budi), kuingia kwenye "muungano" na kuwa na mfumo wa serikali mbili (2) kama ilivyo sasa! Ukiachilia mbali kuongezeka kwa mambo ya muungano kutoka kumi na moja (11) ya awali (tazama kifungu cha 5(1) (b) cha Sheria Namba 22 ya 1964) hadi mambo ishirini na mbili (22) kama yaliyo kwenye Nyongeza ya Kwanza ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977, Toleo la mwaka 2005. Kwa ujumla, muungano umekuwa ukitumiwa kama nguvu ya wenzo (leverage) kwa kila kunapotokezea wananchi kuhoji "uhalali" na au hata uhuru na haki ya kuwapo kwake!
Kwa sehemu kubwa na kwa jinsi ya kipekee, kizazi cha sasa; yaani, kizazi kilichokuja baada ya 1977 wakati vyama vya TANU na ASP vilipoungana na kuzaliwa CCM hakuna mwenye "uoni" sahihi wa kwa nini muungano na jinsi gani muundo wa muungano umekuwa ukibakishwa "siri" baina ya wenye dhamana ndani ya CCM!
Ukiangalia kizazi cha miaka ya 1980 na kuendelea na ambao kwa sehemu fulani ndio wanaochukua zaidi ya asilimia 50 ya watu wote kwa mujibu wa takwimu za idadi ya watu wa Tanzania bado hawajapewa ukweli juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kwa jinsi hii, wakati huu tunapokwenda kuandika Katiba Mpya ndio muafaka na sahihi zaidi kwa wananchi wa Tanzania kupata nafasi ya kuhoji uhalali wa muungano kwa muundo na mfumo wake!
Nadhani na kwa matumizi ya busara na hekima iliyo kuu, haitakuwa muafaka kwa serikali ya CCM na viongozi wake (pamoja na Rais wa Nchi) kutumia "vitisho" vya kisheria na au kimamlaka katika kuwatisha wananchi wasijadili hatma ya muungano katika nukta za: (1) muundo wa muungano; (2) aina ya serikali ya muungano; na (3) nafasi ya kila nchi kwenye muungano.
Haitakuwa vema kwa uongozi wa serikali (na chama kinachotawala) kutumia hila, hadaa au ghiliba za mamlaka inayotawaliwa na sehemu ya viongozi "wahafidhina" na wenye taathira ya udikteta kutoka pande zote za muungano katika kupora uhuru na haki ya wananchi kutoa maoni juu ya jinsi muungano unavyotakiwa uwe kwenye Katiba Mpya.
Hakuna awezaye kuwazuwia wale wenye mamlaka na wanaotoa mamlaka ya kutawala na au kuongoza kujadili nini wanataka! Na lazima ieleweke hapa kwamba, hakuna mwenye haki ya kumiliki mchakato wa utowaji wa maoni ya uandikaji wa Katiba Mpya isipokuwa ni wananchi wa Tanzania, siyo?! Na Tanzania ni nchi (kama jamhuri ya nchi mbili zilizoungana) na kwa jinsi hiyo lazima nchi kwenye "muungano" zipate uhuru na haki sawa kwenye mizani ya kutoa hoja za jinsi muungano ulivyo na utakavyokuwa ndani ya Katiba Mpya. Uongozi wa kisiasa wa chama kinachotawala (CCM), hususan kwenye uongozi na menejimenti ya shughuli za serikali ya JMT, lazima uangalie jinsi unavyoweza kuongoza mchakato wa wananchi kutoa maoni yao bila kuwekewa "shoka begani" au kupigwa kabali!
Pamoja na pongezi kwa uongozi wa Rais Jakaya Kikwete katika kufanikisha uundwaji wa tume ya kuratibu ukusanyaji na hatimaye uchakataji wa maoni ya wananchi juu ya Katiba Mpya; tuna kila sababu ya kumuomba Mheshimiwa Rais kutumia nafasi yake vema katika kuepuka kupora mamlaka ya wananchi.
Hapa lazima iandikwe kwamba hawezi yoyote (hata kwa Katiba ya JMT ya 1977 Toleo la 2005) kuchukua mamlaka ya watu! Inawezekana, na kama wafanyavyo baadhi ya viongozi wenye taathira ya ukiritimba wa chama kimoja au udikteta wa kinyumenyume (indirect dictatorship) kuviza na au kuminya uhuru na haki ya wananchi kutumia uhuru na haki ya kutoa maoni katika kufikia malengo na utashi wa kuwa na katiba itakayotokana na utashi wao.
Wananchi waliokuwa wakifuatilia uanzishwaji wa mchakato wa Katiba Mpya wanajua jinsi Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura Namba 83 ya 2012 ilivyobishaniwa hata kabla ya kusainiwa na hatimaye kufanyiwa marekebisho yaliyoridhiwa na Bunge la JMT baada ya kutokea kwa sintofahamu kati ya wabunge wa CCM (na vyama vingine) dhidi ya wabunge wanaounda kambi rasmi ya upinzani.
Haikuwa kazi nyepesi katika kukubali uwezo mkubwa aliyopewa Rais wa Nchi na sheria inayotakiwa itoe uhuru na haki sawa kwa wananchi wote pasipo kuwa na aina yoyote ya kuminywa na au kumezwa kwa uhuru na haki ya maoni ya wananchi wote wenye akili na umri timamu katika kushiriki mchakato huu.
Ndio kusema kwamba, hakuna taasisi yoyote (hata tume yenyewe) inayoweza kupora na au kunyang'anya kwa namna yoyote iwayo nguvu na mamlaka ya wananchi katika kufikia uamuzi wa kuwa na au kutokuwa na mfumo wowote wa serikali unaoweza kukidhi utashi wa wananchi, utashi wa mazingira ya kisiasa, kiuchumi na kijamii na utashi wa wakati (muda) tulionao.

Hakuna shaka yoyote kwamba wananchi wa pande mbili za muungano, yaani Tanganyika na Zanzibar, wanatambua kwamba; "Zanzibar ni nchi ndani ya muungano." Hili ni jambo linalohitaji mjadala mpana na kama halitatatuliwa na "ainisho" la kisheria ndani ya Katiba Mpya kuna uwezekano hata huu muungano tunaotaka "kuulinda kwa nguvu zote" ukafeli (hatuombi itokee)!
Kwa muktadha huu na kwa kutambua umuhimu wa uhuru na haki ya wananchi wote wa Tanzania (Tanganyika na Zanzibar) kushiriki moja kwa moja kwenye mchakato wa kuandika Katiba Mpya haitakua busara na wala si hekima kuzuwia kwa namna yoyote iwayo wananchi wasiujadili muungano.
Yeyote atakayejaribu kuzuia mjadala wa muungano wakati wa ukusanyaji wa maoni ya Katiba Mpya atakuwa anachochea "uasi" na atakuwa anakoleza moto wa madai mapya juu ya kuwapo kwa muungano na hata uwepo wa serikali ya JMT. Hatuwezi kuzuia mawazo ya udadisi wa kujua hatma ya muungano kutoka kwa kizazi cha 1980 na 1990 ambao kwao kujua ni sehemu ya maisha yao; na hatuwezi kuzuwia nafasi ya utambuzi wa ukweli juu ya uhuru na haki ya watu katika kufikia utashi wa kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Kama kuna watu, kikundi cha watu au hata chama cha siasa (pamoja na CCM) chenye dhamira ya kuzima na au kuzuiwa (kwa nguvu ya dola) wananchi kujadili hatma ya muungano wenye sura tunayoiona sasa kuna kila dalili kwamba mchakato wote wa ukusanyaji wa maoni ya kuandika Katiba Mpya unaweza kuingia dosari za kiutendaji na kuathiri uchakataji wa maoni ya wananchi na hata upatikanaji wa Katiba Mpya kuwa wenye mashaka.
Kila penye mashaka yasiyotolewa ufafanuzi wenye mashiko ya kisayansi (kwa uchunguzi na mantiki) panaweza kuleta vurugu wakati wa kura za maoni kwa vile hakuna atakayekubali kuburuzwa na mtu, watu au kikundi cha watu baada ya kuwa wananchi wote wana wajibu na haki ya kushikriki kwenye kuandika katiba Mpya.
Binafsi na kwa kufuatilia habari na taarifa (za chini kwa chini) za mwenendo wa kisiasa ndani ya mduara wa uongozi wa serikali ya JMT kuna uwezekano wa kutokea msuguano baina ya "wahafidhina" na "waliberali" wa pande zote za muungano, yaani Tanganyika na Zanzibar!
Kwa kuwa manufaa ya ubinafsi na ukiritimba hata utoaji wa maoni baina ya makundi haya mawili na ya hatari yenye masilahi binafsi zaidi kuliko ya masilahi ya umma; kuna kila dalili za mivutano au minyukano ya ndani kwa ndani na hata kupelekea "kampeni" chafu na za uharibifu wa mujtamaa katika kupata maoni yenye kuzingatia utashi wa misingi ya katiba bora na yenye kuzingatia utashi wa wananchi badala ya utashi wa watu wachache wenye choyo na ubinafsi kayaya.
Tunapokwenda kuanza kuhesabu siku ya kwanza ya ukusanyaji wa maoni; kila mwananchi anatakiwa awe msingi wa maoni na ndiyo chemchemi ya uhuru na haki ya kuwa na katiba itakayotokana na wananchi kwa ushiriki wa moja kwa moja kwenye mchakato wote. Haitakuwa busara kwa tume, kama nilivyoonesha kwenye makala ya tarehe 4 Aprili, 2012 kufanya kazi kwa "shinikizo" kutoka kwa yoyote.
Tume inatakiwa iwe huru, ifanye kazi kwa haki, na kwa matumizi ya busara (na hekima) ya hali ya juu kwa kuzingatia weledi (maarifa, ujuzi (ustadi) na maadili) wa hali ya juu. Napenda kusisitiza hapa kwamba; kwa kuwa dhima (kazi) ya ukusanyaji na hatimaye uchakataji wa maoni ya wananchi juu ya uandishi wa Katiba Mpya ni ngumu, wajumbe wa tume ni budi kutambua kwamba wamekabidhiwa dhamana ya kulinda amani ya Tanzania!
Ubabe na au aina yoyote ya kuwanyima wananchi uhuru na haki ya kuujadili muungano na au hata kuweka "mipaka" juu ya nini kijadiliwe na nini kisijadiliwe tunaweza kushuhudia vurugu za maono zinazoweza kuondoa hali ya utulivu na masikilizano na hata kuvuruga mujtamaa kwenye uwiano murua wa mlinganyo wa kisiasa unaostawi (balanced political equation).
Hakuna anayetaka Tanzania iingie kwenye hamkani ya kisiasa, kama ilivyotokea kwa jirani zetu Jamhuri ya Kenya, wakati walipokuwa wakiandika katiba yao; au hata kutamani kutokea fujo na sintofahamu au vuta nikuvute baina ya makundi ya kisiasa, kijamii au kiuchumi juu ya mchakato uliyoanza kwa ujenzi wa taasisi (tume) iliyopewa na kukabidhiwa imani kubwa na wananchi wa Tanzania.
Wale wote wanaodhani kwamba wanaweza kutumia ushawishi na au nguvu ya wenzo (leverage) kwa kuwatumia baadhi ya wajumbe wa tume; ambao kwa sehemu yao walikuwa aidha watumishi wa ngazi "nyeti" kwenye utawala cha kimoja (na chama kushika hatamu) wenye taathira ya moja kwa moja ya uhafidhina (conservatism) na ukiritimba (vanguarism) nadhani wana wajibu kujiepusha na uingiliaji wa aina yoyote iwayo.
Tume iachwe iwajibike kwa kazi yake kwa kuzingatia uhuru, haki, usawa na weledi katika kila hatua ya mchakato hadi pale mwisho watakapoandika kielelezo cha Katiba Mpya kwa jinsi yatakavyoakisi maoni halisi na ya kweli ya wananchi kwa mujibu walivyoshiriki kwenye mchakato.
Kwa jinsi hii ni wajibu; na ndivyo inavyotarajiwa, kwamba tume (na wajumbe wa tume) watafanyakazi ya ziada katika kuhakikisha kwamba wananchi wanapewa nafasi ya kwanza katika kupata haki ya kujua, kuona na kusikia sababu za wao (kama wenye nchi) kushiriki kwenye utowaji wa maoni!
Tume haitakuwa na tija na au ufanisi kama wajumbe hawatachukua muda wa kutosha katika kuwafikia wananchi "wote" wa Tanzania kwa uwiano utakaozingatia maeneo ya kijiografia na kwa mujibu wa uwiano wa sehemu za utawala kwa pande zote za muungano, yaani Tanganyika na Zanzibar! Haki ya wananchi wa Tanganyika ichukuliwe kwa mujibu na njia ileile ya uhuru na haki ya wananchi wa Zanzibar bila ya kuathiri mtazamo wa kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Hata kama kunaweza kudhaniwa kwamba, Zanzibar ni sehemu "ndogo" ya Jamhuri ya Muungano; na Tanganyika ni sehemu kubwa kwa eneo na idadi ya watu, bado kuna kila sababu ya kuchukua dhana na falsafa ya muungano ulikuwa wa nchi mbili na bado utambulisho wa nchi moja ungalipo na hata Katiba ya JMT ya 1977 (Toleo la 2005) inatambua uwepo wa nchi hiyo.
Kama hivi ni kweli, na kama kuna kila dalili ya kuwapo kwa maafikiano juu ya uboreshaji wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika kujenga Tanzania imara na inayostawisha maafikiano, maelewano na mafungamano ya kijamii, kisiasa na kiuchumi ni lazima wananchi wapewe nafasi ya kujadili nukta zote zinazohusu muungano na kuingizwa ndani ya Katiba Mpya.
Kwa kuwa si rahisi kwa kila mwananchi wa Tanzania kupata fursa ya kuchangia maoni kutokana na muda, mazingira, miundombinu, fursa na maarifa (uelewa na ujuzi wa misingi ya katiba) nachukua nafasi hii kutoa elimu kidogo kwa wale wote watakaobahatika kuchangia maoni mbele ya tume itakayoanza kazi ya kukusanya maoni ya wananchi.
Mambo muhimu ya kuzingatia wakati tunajadili muungano na nini kiingizwe kwenye Katiba Mpya juu yake ni wajibu wetu kuzingatia uhuru na haki juu ya: (1) uwepo wa jamhuri ya muungano aina ya muungano na eneo la muungano; (2) uwepo wa serikali ya muungano na aina ya serikali itakayokidhi utashi wa pande zote za muungano; (3) mambo ya muungano kwa utashi wa makubaliano ya awali ya muungano na jinsi uamuzi wa kuongeza na au kupunguza unavyoweza kuathiri muungano; (4) mgawanyo wa nafasi za uongozi na mamlaka ndani ya muungano; na (5) ardhi na rasilimali za nchi – umiliki, menejimenti na matumizi.
Nukata hizi tano (5) zilizoainishwa hapa kama hazitaangaliwa, kujadiliwa, kudadavuliwa (matini na batini) na hata kuwekewa masharti, mipaka na uainishwaji makini na wenye taathira inayozingatia uhuru na haki ya wananchi wa pande mbili za muungano kuna kila dalili kwamba kero zilizopo sasa zitaongezeka kwa kadiri wananchi wanavyokuwa wakinyimwa fursa na wasaa wa kutumia hekima na busara ya watu walio sawa na huru kujadili hatma ya nchi zao (yaani, Tanganyika na Zanzibar).
Tume iruhusu mijadala ya ukusanyaji maoni kwa uhuru na haki bila kuingilia uhuru na haki ya kujadili na au kuhoji. Hivyo basi, ni vema kwa wajumbe wa tume kutaraji maoni yanayoweza kugusa hisia zao hususan ukizingatia kwamba wajumbe wa tume ni binadamu wenye maoni yanayoweza kutofautiana pia!
Ni matumaini ya wananchi walio wengi kwamba tume itatumia ukomavu wa fikra na kuepuka "vurugu za maono" na mitazamo ya kiitikadi (kisiasa, kijamii, kiuchumi na kidini) ili kuhakikisha kwamba wananchi wanapewa nafasi ya kuandika katiba wanayoitaka. Hata kama kukiwa na tofauti kwenye mitazamo ya hoja au falsafa ya uelewa wa misingi bora ya katiba bora utakuwa wajibu wa wajumbe wa tume kutumia akili ya ziada katika kuelimisha zaidi kuliko kukosoa kwa vile wananchi wengi wa Tanzania hawana elimu ya misingi ya katiba na hata hawaijui Katiba ya JMT ya 1977 (Toleo la 2005).
Nina imani kubwa na wajumbe walioteuliwa na kuapishwa kwamba kwa uhuru, haki, usawa na weledi waliokuwa nao wanaweza kutupatia Katiba Mpya itakayotokana na wananchi wote na suala la muungano litapatiwa ufumbuzi wa kudumu kwa uhuru na haki kwa pande zote za muungano!
Chanzo: Bofya hapa!

By ijuekatiba
 
Kukosa kiti UM hakuondoi ukweli kwamba Zanzibar ni nchi. Tanzania ni Muungano wa nchi ngapi? Kama ilikuwa nchi wakati wa kuungana na Tanganyika, itaendelea kuwa nchi milele kama ilivyo kwa Tanganyika ambayo imekuwa "ruhani" yaani nchi isiyoonekana.

Ndugu yangu,Tanganyika tulibadili jina na Kujiita Tanzania baada ya kujiongezea himaya ya Zanzibar,Zanzibar ni Koloni letu ndio maana hakuna hata Siku Moja Mkutano au Kikao kinachohusu Tanzania kikafanyika Zanzibar na wala Zanzibar haiwezi kugharimia kwa Sababu ipo Chini ya Himaya ya Tanganyika(hutamkwa Tanzania).
 
mkuu mimi ni muumini wa serikali moja tu.

Mkuu siwezi kupinga mawazo yako, but kuundwa serikali moja haiwezekani kutokana mchakato unavyoendelea!
...
Jee ikiwa hiyo haiwekani?
 
1. Tanzania ni nchi moja na ni Jamhuri ya Muungano.

Katiba ya JMT Ibara ya 1
 
33.-(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.

(2) Rais atakuwa Mkuu wa Nchi, Kiongozi wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu.



34.-(1) Kutakuwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ambayo itakuwa na mamlaka juu ya mambo yote ya Muungano
katika Jamhuri ya Muungano, na pia juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania Bara
 
ARTICLE 1 -Montevideo Convention

The state as a person of international law should possess the following qualifications: (a) a permanent population; (b) a defined territory; (c) government; and (d) capacity to enter into relations with the other states.
 
ARTICLE 3

The political existence of the state is independent of recognition by the other states. Even before
recognition the state has the right to defend its integrity and independence, to provide for its conservation and prosperity, and consequently to organize itself as it sees fit, to legislate upon its interests, administer its services, and to define the jurisdiction and competence of its courts.

The exercise of these rights has no other limitation than the exercise of the rights of other states
according to international law.
 
Back
Top Bottom