Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,116
Mkuu wa Wilaya ya Mjini Magharibi Unguja, Rashid Simai Msaraka amepiga marufuku, Wafanyabiashara wa Wilaya hiyo kuweka midoli yenye nguo zisizo za staha nje ya maduka yao.
DC Msaraka ametoa kauli hiyo baada ya kukutana na Mfanyabiashara maeneo ya Kwahani Zanzibar akiwa ameweka midoli hiyo nje ya duka ikiwa imevalishwa nguo ambazo zinadaiwa kupotosha maadili ya Zanzibar hususan kwa Watoto pindi wanapoona midoli hiyo imevishwa nguo hizo
DC Msaraka ameiambia AyoTV kuwa maarufuku hiyo imetokana na Watoto na Vijana kuona vitu visivyo na staha na kupelekea kuvuraga akili za Vijana wa Zanzibar Hatuwakatazi kuwa na midoli hiyo wala hatuwakatazi kufanya biashara hizo ila biashara hizo zifanywe ndani na zisiwekwe nje, Mtu anayetaka kuvaa nguo hizo avae
mwenyewe anajua utaratibu gani wa kuzivaa na wapi azivae"
Chanzo: Millard Ayo
Pia soma mada zinazohusiana
- Hii midoli ya fasheni kwenye maduka inayovalishwa nguo za ndani inavunja maadili
- Maadili: Midoli kwenye maduka ya kuuza nguo kuachwa uchi, hii imekaaje?
- Hii midoli ya madukani ni udhalilishaji wa wanawake. Waziri Gwajima piga marufuku matumizi yake
- Hii Midoli inayovalishwa Nguo za ndani za Kike na kusimamishwa hadharani inawaaibisha wanawake na mama zetu!
- Baraza la Sanaa Zanzibar: Wanaume Wanaosukwa kama Wanawake kukamatwa, faini ni Tsh. Milioni 1 au kifungo cha Miezi 6
- Zanzibar: Marufuku kucheza kwa kulowanisha nguo
- Zanzibar: Marufuku Wamasai kutembea na SIME na RUNGU
- Zanzibar kupiga marufuku shisha na sigara za kielektroniki
- Zanzibar yapiga marufuku kuuza (ku-export) mchele na sukari nje ya visiwa hivyo
- Kwanini michezo ya mapigano ni marufuku Zanzibar?
- Serikali ya Zanzibar yapiga marufuku matumizi ya nembo ya upinde wa mvua (Rainbow) mashuleni
- Yanayoendelea Zanzibar tusubiri majibu ya Wahanga na kuzaa gharika