Zanzibar Kumekucha

Ni chuki zao ndo zinawafanya wahc 2nawanyonya,umeshawah kuona wabara wanavyonyanyaswa Z enji? Baa zao zinachomwa,je umewah kuckia duka la mpemba limechomwa moto Dar au Mby?


Mbona unalinganisha mambo mawili tofauti. Kule Zanzibar kuna maduka ya Wabara na kuna wamachinga kibao kutoka bara na hujasikia kuchomwa moto na hivyo hivyo mbona hutwambii kuna baa ngapi za Wapemba huko Bara. Ukiendda pahala basi angalau ishi kama wenyewe wanavyoishi sio uwapelekee madhara. Hivyo kwako baa umeiweka kitu muhimu?
 
Kwa mtazamo wangu hizi chokochoko hazitaisha, hata kama wakipiga kura, na wanaotaka muungano kuvunjika wakawa wachache, siku itafika watadai kwa nguvu tu.Hii ni hatari kwani hao wachache wataendelea kumwaga sumu kwa wengine.Ni kama ilivyokuwa madai ya mfumo wa vyama vingi mwaka 1992....wale wachache (20%) waliotaka vyama vingi wangelikataliwa...hali isingetulia mpaka wangekuja dai haki yao kwa nguvu.Hii hata kwa zanzibar inaweza ku-apply....nafikiri tuwaache waamue hatma ya nchi yao...mimi nimekaa na wazanzibari wa kawaida karibu wote walionesha kutoutaka muungano, wamekuwa ni watu wa kulalamika kila wakati...wanaona tunawanyonya...hata katika masomo wakifeli wanaona wanaonewa...juhudi hawana, hawapendi kufanya kazi kwa kujituma...jamani tuwaache waondoke kwa amani...dar si mbali watakuwa wanakuja kutusalimia...bara hatutapoteza kitu...tuna natural resouses kibao, virgin ardhi kubwa, misitu, mito, madini, mafuta,gesi, wanyama. Kama tutaacha ufisadi..na kulitumikia taifa kwa moyo wote huku serikali ikilipa watumishi malipo bora...tutapiga hatua kubwa sana kimaendeleo ndani ya muda mfupi tu.

Kwa mtazamo wako haki ya Zanzibar ni chokochoko navuguvugu za kudai haki huko kwenu ni kitu takatifu? Kuhusu maisha ya Wazanzibari ni bora ukanyamaza kwani Zanzibar haikuwa hivi kabla ya kuingia CCM na halafu si nyie mnaolalamika kuwa Wapemba wametajirika? Sasa mvivu nani wewe unaililia umasikini na yule alitajirika? Mnapochangia bora muangalie dharau zenu zisije zikakurudieni.
 
Hao wanaosema hawautaki muungano ni wale vikaragosi vya sultan Jamshid anaetaka kurudu kwa mlango wa nyuma ; kwani mwanae wa nje amepata madaraka sasa huko Zenj!!

Bulesi,
Hii lugha yako ndio your best?

Unaweza kutofautiana kimtazamo na mwengine bila ya ku-resort to name calling au matusi.

Mimi hujiuliza hizi hoja za waarabu kurudi Zanzibar au wale waliokimbia wakati wa mapinduzi watarudi....hupata tabasamu katika siku hiyo.

watu waliokimbia wakati huo leo wana umri gani?
Kama wana 60 over ni kusema they are done! mtu kama Ali mwinyi au Jumbe wana muda na siasa kweli?
kama wamejenga maisha yao huko kweli warudi kwenye umaskini,ujinga na maradhi?

Does this apply to Germans and English to come back to Tanganyika aka Tanzania bara?

Ni hoja dhaifu and pure scare tactic!

Wapate sovereignty yao halafu, tuone kama itakuwa hivyo. watakuwa na escape route,, EAC.

Wakuu, Tanganyika needs to get serious na sio kugawana umaskini.

Kama zanzibar ni mzigo kwetu wakiondoka ndio nafuu yetu.
kwa nini tunasubiri situation ya Eritria na Ethiopia au East timor na Indonesia?
 


Mkuu unakuwa kama mgeni na issue zinazohusu muungano? Zingatia haya;

  1. Mara ngapi ile kamati iliyochini ya Makamu wa Rais na waziri kiongozi(kabla ya marekebisho ya katiba zenji) walikaa na kutudanganya kuwa mapungufu yanafanyiwa kazi na hatuoni mabadiliko?
  2. kwanini bado watanzania mnapenda kuendelea kudanganywa kwa mambo yaliyowazi?
  3. Kwa hakika mapungufu ya Muungano HAYAZUNGUMZIKI tusidanganywe na viongozi wasio waadilifu na wasio litakia mema taifa hili..
  4. Kama bado tunaupenda Muungano hatuna budi kubadilisha mfumo wake hasa katika serikali...
Mimi naupenda Muungano but wanzanzibar wanakera mno,chokochoko nyingi wakati kiuchumi bado wako hoi....kama tunataka kuendelea nao tufanye mchakato wa kuwa na serikali tatu...FULL STOP...

Mbona mawazo yako mazuri unayaharibu hapo chini/ Si umeshasema kuwa tumekuwa tukidanganywa kuhusu kutatuliwa matatizo sasa kwani useme chokochoko iwa[po watu wanadai hatuwa za kweli?
Naomba kujuwa kwa upande wa Bara waliwasilisha kero gani vile kwenye Muungano? Au hawana kero wao ndio maana hawafanyi chochoko?
 
Umoja ni nguvu ikiwa wote mnajenga kitu kimoja. Lakini kama mmoja anajenga kitu chake kwa kutumia fito za wote inakuwaje? Zenj hawatumii tu fito za wote ila wanachomoa fito zilizojengwa kwenye nyumba. Kwa mfano walidai wapeperushe bendera yao - wakapata; wakataka wimbo wao - wakapata. Walipobadili katiba ili wajitenge zaidi wakasema Znz ni nchi. Hapa wakavunja katiba ya muungano kwa waziwazi ila mkuu wa nchi amawanyamazia. Hapo kuna muungano?

Unajuwa hii kauli ya mmoja kujenga kitu chake kwa kutumia fito za wote. Unaonaje hii tabia ya Tanganyika kujijenga kwa fito za Muungano hujaiona bado? Hebu nitafautilishie Bunge la Muungano na lile la Tanganyika? Bajeti ya Muungano na ya Tanganyika. Rais wa Muungano na Rais wa Tanganyika? Nafikiri hutoweza kutafautisha na huku ndio kutumia fito za Muungano kuijenga Tanganyika. Mfano mmoja ni ni umeme kwani ule umeme ni wa nani wa Muungano au wa Tanganyika?
Kwa upande mwengine Zanzibar inajengea fito zake mwenyewe na iwapo Muungano ukivunjika basi walichofanya kitabaki Zanzibar na kwa upande wa Bara kitabaki bara lakini kilifanywa kwa jina la Muungano.
 
Nonda at work, plz usipotoshe Nonda uchumi wa zanzibar ulikuwa mzuri sio kabla ya union bali sema kabla ya Mapinduzi, ni mapinduzi ambayo yaliwafukuza masettlers wengi wa kiarab na kupunguza imani ya wafanyabiashara hao kuwekeza zanzibar,kama ilivyokuwa huku bara na azimio la arusha-achana historia ya maskani. Karume akakuta pesa akatumia bila kuwekeza ktk return endelevu ili kuwa na revenue endelevu-zilipoisha kwisney. Kwanini kila falure yenu nyie zenj mnadai ni bcz Tanzania?(eh sory ni Darnyika)!

Bwana mipango mingi kama huielewi Zanzibar basi vitabu visikudanganye.
Masetler gani wa Kiarabu waliokuwa wakiekeza Zanzibar? zanzibar ikitegemea kilimo cha karafuu na minazi na mazao haya yalianguka bei wakati nchi kama indonesia walipoamuwa kuzalisha wenyewe. Kuendelea kiuchumi kwa Zanzibar hakukuletwa na Mapinduzi bali kuliletwa na kuundwa na Chama Mapinduzi.
Zanzibar ilihitaji kujibadilisha na kuingia katika mpango wa kuvutia wawekezaji lakini sera za CCM zikawa zinazuia jitihada hizo. Kinachohitajika kwa sasa ni kuiachia Zanzibar ijiamulie mambo yake na utaona inavyokimbia kimaendeleo na wala usifikiri kuwa Zanzibar inahitaji mgongo wa Tanganyika. Waachieni uhuru tu muone.
 
Mie nafurai ukifa muungano hata msongamano dar utapungua maana ikulu na mawaziri wote dodoma
 
Hapo nilipoweka red naomba utafakari yafuatayo: Mapinduzi ya Zanzibar yametokea January 12 1964, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulifanyika tarehe 22 April 1964 (siku rasmi uliposainiwa mkataba wa Muungano) - jee ni siku ngapi? Jibu 112!. Sasa kama umewahi kusoma historia ya Zanzibar utajua kabisa kwamba kwa kipindi hicho hata Zanzibar yenyewe ilikuwa haijakaa sawa. Na hata huku Tanganyika hakukuwa sawa baada ya mutiny iliyotokea January 19 (wiki moja baada ya mapinduzi). Kama kila kitu kilikuwa poa haraka zilikuwa za nini?
Hivi ulishakaa ukafikiria kuwa labda makubaliano ya kuungana yalikuwa yamefikiwa kabla ya mapinduzi? I.e. Tanganyika itoe msaada kwa kina Karume in return tuungane?
 
Hamtokaa salama!! luv this one please watch it all! its' amazing stuff!!



Mzee manafiki tu huyu ndio alieleta upemba na uunguja,na tunaweza kujitenga wewe nyerere si ulijifanya unaakiliii,,,sasa subirii
 
Last edited by a moderator:
Sikilizeni,watanganyika/watanzania nyinyi hamuuelewi maanga ya muungano na vipi munafaidika na vipi munapata hasara,wazanzbari ni watu ambao wasomi,wafanya biashara,na wenyewe uwezo kwa silimia kubwa ukipiga hesabu ya wananchi wa zanzibar.

Muungano unakuja kiuchumi,na uchumi ni kkifedha,wazanzibari ni wafanya biashara,ipo katika damu yao hasa,kwa hiyo katika huu muungano wao wanaufahamu zaidi kuliko watanganyika,kutokana wao ni wafanyaji biashara,kiuchumi hauwasaidiii,nyie ndio munao faidika muungano,kiufupi ni kwamba baadhi ya watu hawafahamu vitu gani ambavyo vinafanya nchi ukiwe kiuchumi ukiwacha hizo rasilimali mulizonazo.

Muna ropoka maneno tu ,,oh vunja waache wandee kwaoo,ah nini wewe,nyie ndio mutakao athirika,sisi wazanzibar tutabaki kama wazanzbari,jee nyinyi ? Kuna makabila kibao,na sasa kumeingia na udini,kutakuwa hakuna mtanganyika,na nyerere ameshawaleza,.musije kuiyacha zanzibar,kwani anafahamu fika kuwa zanzibar itabakia kuwa zanzibar.

Muungano huu hauna maana kwa wazanzbari kiuchumi,kwa maslahi yao kinchi,,hakuna mtu anaetaka kuuza utaifa wake,katika muungano kulikuwa na mataifa mawili,tanganyika na zanzibar,jeee leo hii mmoja afute utaifa avae koti la muungano huoni kuwa ni ulakini na usanii ?

Kura ya maoni sio wauliza wananchi kuvunja muungano au serikali tatu au moja...hapanaa

KURA IWAULIZE HIVI,Munataka muungano au hamutaki ?
muungano huo ukiwa unautaka uwe vipi ? Serikali tatu au wa kibiashara tu kama EAC.
 
Nimefurahi kusikia maoni yenu watanzania bara. Sisi wazanzibari tunataka nchi yetu. Sivo kamwe hivo munavofikiria kuwa ulimwengu wa ulaya wanakuwa kitu kimoja. East africa wanakuwa kitu kimoja. Huwezi kufananisha mapatano/ makubaliano na kutawaliwa. Sisi wazanzibari tumetawaliwa kikoloni. Na mtu akisoma nakala zenu, zinaonyesha wazi dharau mulionayo dhidi ya wazanziabri. "tukiwaachia nchi yao watauawana wao kwa wao". Kauli kama hizo ni za kejeli na wengi wenu hamujuwi athari ya muungano dhidi ya Zanzibar. Ikiwa mutakuwa na subira mukataka kujua kinachowafanya wazanzibari wakaukataa muungano pengine munge faidika katika kujua matatizo ya utawala wenu.Sisi ni wazanzibari popote pale tulipo duniani wala hatujitambulishi kama watanzania/ wabongo. Hilo ni lazima mulikubali katika akili zenu. Tuliweza kushirikiana kabla muungano na yunaweza kushirikiana baada ya muungano lakini mambo ya kuburuzwa na nchi yetu basi. Wala musifikiri tunaogopa, la hasha waliosababisha midahalo ya katiba Tanzania ni sisi wazanzibari na ukitaka kujua zaidi, tembelea blogi za kizenj uone kama ni waoga wakusema. Miezi miwili sasa hivi inaendelea mijadala na kongamano za katiba na wanaozungumza ni wananchi wa Zanzibari kwa mapenzi ya nchi yao Zanzibar. Tunawataka na nyinyi mulio bara muwe na kongamano kama zetu mujadili mustakbali wa nchi yenu.
 
huyu nyerere ni mungu wenu?. kila kitu nyerere munajuwa huyu mtu alivowafanyia nyinyi?.
 
Nonda at work?
Nonda mpotoshaji?
Nonda ana historia ya Maskani?
Nonda mzenj?
Tanzania....Darnnyika?

Mkuu.
Ningependa sana kuchangia juu ya mchango wako lakini naona umejaa jazba.

La msingi bila ya kuweka wazi ni kuwa umekubali kuwa tatizo ni viongozi, inatosha. Viongozi wa Tanzania, Tanganyika na Zanzibar. Wa Zanzibar siwalaumu sana kwani wamebanwa sana na Muungano.

Nooo Nonda, sina hata chembe ya jazba mkuu, lakini ule ndo ukweli, si Tanganyika wala muungano kilichoua uchumi wa Zanzibar ni Mapinduzi tu na kushindwa kusimamia vya kutosha sekta ya karafuu. Jaribu kutafuta post zako zote zihusuzo masuala ya Muungano/zanzibar/Tanganyika ndo utaona kwa nini niliesema Nonda at work. Niliandika Darnyika bcz, for me jina iz nothin just identification so hata kama tukiamua kuita jina lolote haitaongeza wala kupunguza status ya Taifa lolote, kinachomata ni mipango michache yenye utekelezaji madhubuti na wala siyo Mipangomingi!
 
Nimefurahi kusikia maoni yenu watanzania bara. Sisi wazanzibari tunataka nchi yetu. Sivo kamwe hivo munavofikiria kuwa ulimwengu wa ulaya wanakuwa kitu kimoja. East africa wanakuwa kitu kimoja. Huwezi kufananisha mapatano/ makubaliano na kutawaliwa. Sisi wazanzibari tumetawaliwa kikoloni. Na mtu akisoma nakala zenu, zinaonyesha wazi dharau mulionayo dhidi ya wazanziabri. "tukiwaachia nchi yao watauawana wao kwa wao". Kauli kama hizo ni za kejeli na wengi wenu hamujuwi athari ya muungano dhidi ya Zanzibar. Ikiwa mutakuwa na subira mukataka kujua kinachowafanya wazanzibari wakaukataa muungano pengine munge faidika katika kujua matatizo ya utawala wenu.Sisi ni wazanzibari popote pale tulipo duniani wala hatujitambulishi kama watanzania/ wabongo. Hilo ni lazima mulikubali katika akili zenu. Tuliweza kushirikiana kabla muungano na yunaweza kushirikiana baada ya muungano lakini mambo ya kuburuzwa na nchi yetu basi. Wala musifikiri tunaogopa, la hasha waliosababisha midahalo ya katiba Tanzania ni sisi wazanzibari na ukitaka kujua zaidi, tembelea blogi za kizenj uone kama ni waoga wakusema. Miezi miwili sasa hivi inaendelea mijadala na kongamano za katiba na wanaozungumza ni wananchi wa Zanzibari kwa mapenzi ya nchi yao Zanzibar. Tunawataka na nyinyi mulio bara muwe na kongamano kama zetu mujadili mustakbali wa nchi yenu.

Upupu mtupu, tena unawasha!
 
Unajuwa hii kauli ya mmoja kujenga kitu chake kwa kutumia fito za wote. Unaonaje hii tabia ya Tanganyika kujijenga kwa fito za Muungano hujaiona bado? Hebu nitafautilishie Bunge la Muungano na lile la Tanganyika? Bajeti ya Muungano na ya Tanganyika. Rais wa Muungano na Rais wa Tanganyika? Nafikiri hutoweza kutafautisha na huku ndio kutumia fito za Muungano kuijenga Tanganyika. Mfano mmoja ni ni umeme kwani ule umeme ni wa nani wa Muungano au wa Tanganyika?
Kwa upande mwengine Zanzibar inajengea fito zake mwenyewe na iwapo Muungano ukivunjika basi walichofanya kitabaki Zanzibar na kwa upande wa Bara kitabaki bara lakini kilifanywa kwa jina la Muungano.

Upupu mtupu, tena unawasha saaaana!
 
Sikilizeni,watanganyika/watanzania nyinyi hamuuelewi maanga ya muungano na vipi munafaidika na vipi munapata hasara,wazanzbari ni watu ambao wasomi,wafanya biashara,na wenyewe uwezo kwa silimia kubwa ukipiga hesabu ya wananchi wa zanzibar.

Muungano unakuja kiuchumi,na uchumi ni kkifedha,wazanzibari ni wafanya biashara,ipo katika damu yao hasa,kwa hiyo katika huu muungano wao wanaufahamu zaidi kuliko watanganyika,kutokana wao ni wafanyaji biashara,kiuchumi hauwasaidiii,nyie ndio munao faidika muungano,kiufupi ni kwamba baadhi ya watu hawafahamu vitu gani ambavyo vinafanya nchi ukiwe kiuchumi ukiwacha hizo rasilimali mulizonazo.

Muna ropoka maneno tu ,,oh vunja waache wandee kwaoo,ah nini wewe,nyie ndio mutakao athirika,sisi wazanzibar tutabaki kama wazanzbari,jee nyinyi ? Kuna makabila kibao,na sasa kumeingia na udini,kutakuwa hakuna mtanganyika,na nyerere ameshawaleza,.musije kuiyacha zanzibar,kwani anafahamu fika kuwa zanzibar itabakia kuwa zanzibar.

Muungano huu hauna maana kwa wazanzbari kiuchumi,kwa maslahi yao kinchi,,hakuna mtu anaetaka kuuza utaifa wake,katika muungano kulikuwa na mataifa mawili,tanganyika na zanzibar,jeee leo hii mmoja afute utaifa avae koti la muungano huoni kuwa ni ulakini na usanii ?

Kura ya maoni sio wauliza wananchi kuvunja muungano au serikali tatu au moja...hapanaa

KURA IWAULIZE HIVI,Munataka muungano au hamutaki ?
muungano huo ukiwa unautaka uwe vipi ? Serikali tatu au wa kibiashara tu kama EAC.

Shehe hoja nini, mbona hamueleweki? Watanganyika wanasema vunjeni tu muungano, Watanganyika hawana say, wao hawaujui na wala they dont care, sasa nyie ndo mna huruma sana au kitu gani kinachowafanya mdai Tanganyika imepoteza utaifa wake? Tanganyika haijapoteza utaifa wake hata kidogo, they recognized all over the world na wanadunda na si wabinafsi ndo maana wamekubali kujiita Watanzania simply nothing to lose if u call Tanzanian, Tanganyikan, Mnyamwezi, Mbongo yaani vyovyote wao poa tu-alimradi ujue tu huyu ni wa wapi.
 
Kwa mtazamo wako haki ya Zanzibar ni chokochoko navuguvugu za kudai haki huko kwenu ni kitu takatifu? Kuhusu maisha ya Wazanzibari ni bora ukanyamaza kwani Zanzibar haikuwa hivi kabla ya kuingia CCM na halafu si nyie mnaolalamika kuwa Wapemba wametajirika? Sasa mvivu nani wewe unaililia umasikini na yule alitajirika? Mnapochangia bora muangalie dharau zenu zisije zikakurudieni.
Amueni juu ya nchi yenu. Kwa maoni yangu sisi hatuna tatizo.Tutatoa baraka zote.Mkisha ondoka mtakuja gundua mchawi wala si muungano....matatizo mliyonayo ni mengi sana tu.
 
Amueni juu ya nchi yenu. Kwa maoni yangu sisi hatuna tatizo.Tutatoa baraka zote.Mkisha ondoka mtakuja gundua mchawi wala si muungano....matatizo mliyonayo ni mengi sana tu.

Hii ndo ajenda ya sisi Watanganyika always. tunabariki sana mjitenge, kwani kukosa rafiki ndo mwanzo wa kutafuta rafiki ati!-nyie amueni tu sio kufungua majukwaa ya kukashfu wengine hali ya kuwa kinachotakiwa ni only single statement-Muswaada wa kuvunja Muungano, au tuwasaidie kuudraft? Lakini kwa hoja ya sisi tudai Tanganyika yetu tuidai toka wapi na tunayo?
 
Muungano ukivunjika who is a looser?? wapemba wananunua mashamba Mbagala na Mkuranga kama vile wapo wete, Maduka ya kariakoo ni wapemba watupu, wachuuzi wa mchele pale Tandika ni wapemba, nenda shy wanunuzi wa mchele ni hao hao. Kwa upande mwingine, mtu wa bara ukiweka hata kioski cha soda zanzibar hakuna atakayenunua, achilia mbali ardhi ambayo hauwezi kupewa labda unywe kikombe cha babu. Jamaa hawaangalii mbali, wazanziba/pemba ni wakuzaliana sana, familia moja watoto sita, nane mpaka kumi, suala la global warming hawalioni kwao, ukubwa wa kisiwa chao unapungua siku hadi siku, sasa kisiwa kikimezwa watakwenda wapi?

Kwa maoni yangu binafsi, mbali na udungu tunaoutaka hasa watu wa bara kwa kifupi wao ndio wanaotunyonya tena kama kupe. Tumewapendelea sana sasa inaonekana tunajikomba ACHA WAVUNJE MUUNGANO WAO WENYEWE LITAKALOWATOKEA WAWE TAYARI KULIMEZA.
 
Back
Top Bottom