MwanaCBE
JF-Expert Member
- Sep 23, 2009
- 1,771
- 804
Kenya, Rwanda, Burundi zinamuungano na nchi gani???Kidole kimoja hakivunji chawa
Kenya, Rwanda, Burundi zinamuungano na nchi gani???Kidole kimoja hakivunji chawa
Sio hilo tu, lakini siku Muungano ukivunjika, Pemba nayo itajitenga na Unguja huku kukiwa na uwezekano wa Tanzania kugawanyika vipande vipande katika maeneo ya kanda.UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU.
Dunia ya sasa ni juu ya umoja na ushirikiano. Tazama nchi za jumuiya ya Ulaya, wanazidi kuwa wamoja. Mifano ipo wazi, ni umoja wao katika kutafuta mafuta ya Afghan, Iraq, Kuwait, na sasa Libya kwa maendeleo ya watu wao na nchi zao. Zamu ijayo itakuwa ni Mafuta ya Unguja, Uranium ya Tanganyika, Mafuta ya Sudan ya Kusini, Mafuta ya Uganda, Angola n.k
Jumuiya ya Ushirikiano ya Afrika Mashariki inategemea kumpata Sudani ya Kusini kama mwanachama mpya mwaka huu. Iweje sisi Watanzania tufurahie kuuvunja Muungano wetu? Mimi binafsi, ninadhani maeneo yote yenye utata kwenye Muungano wetu yanazungumzika, hivyo yawe wazi na tuyazungumze ili tupate muufaka kwa munufaa ya Nchi yetu Tanzania.
Muungano ukivunjika, sehemu zote za Tanganyika, Unguja na Pembe haizitakaa ziwe huru na salama. Tanganyika itajikita zaidi Magharibi, Pemba na Unguja wataegemea Middle East. Kihistoria, Magharibi (Ukristo) na Middle East(Uislamu), piga ua na garagaza sehemu hizi ni MAHISIMU.
Wito wangu: CHONDE CHONDE, tusidhubutu kuukaribisha uhasimu huo katika nchi yetu, maana utatumaliza.
****** ataki muungao uongelewe kwenye katiba mpya, hiyo ni dhairi muungano unamatatizo sana. Inakuwaje znz wanajibadilishia tu katiba wanavyotaka wao. kuwe na serikali moja na rais mmoja au muungano uvunjike tuwe na serikali mbili kila mtu kivyake
Sio hilo tu, lakini siku Muungano ukivunjika, Pemba nayo itajitenga na Unguja huku kukiwa na uwezekano wa Tanzania kugawanyika vipande vipande katika maeneo ya kanda.
Tatizo la Muungano kwanza ni vipengele vyake vyenye utatanishi na mgawanyo usio sawa wa mapato ya nchi. Hapa nakusudia kutokuwepo mipaka ya wazi inayotenganisha mamlaka ya Serikali ya TZ Bara ambapo kuna serikali mbili ndani ya moja, ile inayoshughulikia mambo ya TZ Bara na ile inayoshughulikia mambo ya Muungano. hili linatuudhi hata hapa bara.
Tatizo la pili na hili ndio kubwa zaidi, ni ugawanyaji mbaya wa utajiri wa nchi. Kama utaangalia, sehemu tajiri na mhimili wa uchumi wa nchi, ndio masikini kabisa. Suluhisho moja katika mengi, ni kuwa vipengele vyenye utatanishi vinazungumzika na kujaribu iwezekanavyo kuendeleza sehemu zenye utajiri na sio kuzifanya kama shamba la bibi.
Muungano ni wa kihuni na muundo wa serikali yetu ni wa kihuni.
Nikifikiria vyanzo vya mapato Zenj kichwa kinauma. Mtauana sana. Tokeni sasa. Kura kama laki 2 za CCM zitapungua. Better
Tanganyika, kwanini iegemee magharibi?UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU.
Dunia ya sasa ni juu ya umoja na ushirikiano. Tazama nchi za jumuiya ya Ulaya, wanazidi kuwa wamoja. Mifano ipo wazi, ni umoja wao katika kutafuta mafuta ya Afghan, Iraq, Kuwait, na sasa Libya kwa maendeleo ya watu wao na nchi zao. Zamu ijayo itakuwa ni Mafuta ya Unguja, Uranium ya Tanganyika, Mafuta ya Sudan ya Kusini, Mafuta ya Uganda, Angola n.k
Jumuiya ya Ushirikiano ya Afrika Mashariki inategemea kumpata Sudani ya Kusini kama mwanachama mpya mwaka huu. Iweje sisi Watanzania tufurahie kuuvunja Muungano wetu? Mimi binafsi, ninadhani maeneo yote yenye utata kwenye Muungano wetu yanazungumzika, hivyo yawe wazi na tuyazungumze ili tupate muufaka kwa munufaa ya Nchi yetu Tanzania.
Muungano ukivunjika, sehemu zote za Tanganyika, Unguja na Pembe haizitakaa ziwe huru na salama. Tanganyika itajikita zaidi Magharibi, Pemba na Unguja wataegemea Middle East. Kihistoria, Magharibi (Ukristo) na Middle East(Uislamu), piga ua na garagaza sehemu hizi ni MAHISIMU.
Wito wangu: CHONDE CHONDE, tusidhubutu kuukaribisha uhasimu huo katika nchi yetu, maana utatumaliza.
Haíingii akilini kuwa huku tunajadili muungano wa nchi 5 za EA na huku tunajadili kuvunja muungano wa tanganyika na zanzibar
Nikifikiria vyanzo vya mapato Zenj kichwa kinauma. Mtauana sana. Tokeni sasa. Kura kama laki 2 za CCM zitapungua. Better
Unaweza kusema pia kuwa muungano wa Tanganyika na Zanzibar unaendeshwa kihuni na kwa ubabe.
Kwa kifipi ni unafiki mtupu.
Hakuna mipaka ya kimamlaka kwa serikali ya Muungano inapojigeuza pia kuwa serikali ya Tanganyika.
wakati inakuwa rahisi kuwambia wazenj wanakiuka katiba wanapofanya mabadiliko ya katiba yao, la ajabu ni kuwa Tanganyika haina katiba yake.
Mimi nashindwa kuelewa vipi mamlaka tatu kisheria zinatumia Katiba mbili tu!
This is more than mkorogo wa kichina!
Na sisi tunapiga kelele tuwe na serikali moja badala ya kudai serikali ya Tanganyika pia iwepo!!!
Je na sisi pia ni wahuni?
Kama wazanzibar watawaacha waTanganyika basi watanganyika watabaki wamedumaa, lakini wazanzibar hawatabaki salama!!!!!!!!!
Nukuu isiyo rasmi