Zamani ilikuwa raha

Zamani ilikuwa raha

Na ratiba za kuburudisha zilikuwa zinatolewa kwenye gazeni, ratiba za band, cinema, usoma kwenye gazeti la mfanyakazi, unajua leo niende avalon cinema au kuwaona vijana jazz....


Nakumbuka kulikuwa na bendi nyingi za dansi, kulikuwa na Tabora jazz, DDC Mlimani park, tancut almas, yaani bendi zilikuwa nyingi nyingi sana zenye ladha ya kimuziki wa Kitanzania haswa, na wengi wetu tulikuwa tunacheza kwenye vumbi ukumbini hahahahaha

Wanamuziki walikuwa wanavaa mavazi fulani kung'aa ng'aa na mapozi fulani niliyapenda sana
 
wee unaona kuchagua bega ni vizuri??
kumbuka tulikuwa hatupewi uhuru wa kuchagua umpendae atiii...........kidume kikikumind kinakubeba tena kikisaidiwa na vidume wengine wee upendo utajifunzaga kumpendaga huko huko.

mbaya zaid ilikuwa ukishakaa kwake hata kama hamtakutana kimwili usiku huo tayari wewe umeshakuwa mkewe huwez kutoroka na kurudi nyumban tena, na hata ukitoroka hupokelewi na wazazi manake wanajua tayari ushatolewa ubikira.

Tatizo lenu mkipewa nafasi ya kuchagua mnatumia vigezo feki, pia mnachagua wengi siyo mmoja..., bora msiwe na option tu nyie
 
Kilimanjaro Hotel umenikumbusha zamani sana wakati bado nipo kinda tulikuwa tunapelekwa kuangalia mashindano ya magari Kilimanjaro Hotel ndio wanapomalizia mashindano yao kuna dereva mmoja anaitwa DUDU(Singasinga)
alikuwa anatisha sana akiingia yeye watu DUDU huyo. Kwanza lazima achimbe sana mashine lazima uisikie kisha gari imejaa(imetapakaa tope) tele.
Nakmbuka kusoma kuwa alfariki miakakama au 4 iliyita. R.I.P

Jamani kuna mtu yeyote mwenye data za DUDU


Na Beth Shekland ( Skumbuki SP) jamani mnaangalia pale Kilimanjaro Hotel wanvyoanza mashindano ya magari.
 
kwan wewe hujasoma imeandikwa tamaa ya wmanaume itakuwa juu ya mwanamke?

Sasa umekuja kwenye point...., kuwa na mchepuko mmetilazimishaaaaa jaman, mmetumia vibaya hiki kipengele cha tamaa yetu vby, mmetuwekea mchina hapo nyuma, mmepiga jeki hapo kifuani n.k........! hakika MUNGU atujaalie utulivu wa kuyashinda haya.
 
Sasa umekuja kwenye point...., kuwa na mchepuko mmetilazimishaaaaa jaman, mmetumia vibaya hiki kipengele cha tamaa yetu vby, mmetuwekea mchina hapo nyuma, mmepiga jeki hapo kifuani n.k........! hakika MUNGU atujaalie utulivu wa kuyashinda haya.
ivi tumewalazimisha ama nyie ndio mmeshindwa kustahimili hizo tamaa zenu?
ivi inakuwaje unapenda/tamani mchina?
 
Zamani saa unarekebisha, kulingana na redio. Baada ya zile ngoma unasikiliza: ti, ti, ti, tiiiiiiiiiiiiiiii. Hi ni Redio Tanzania Dar es salaam

Ha ha ha ha ha Mkuu wewe umenikumbusha mbaaali sana na zile ladha zao sauti za watangazi wa Redio Tanzania Dar Es Salaam na kale kamlio wa ti ti ti ti tiiiiiiiiiiiiiiiii
Walikuwa wanaanza hivi, "Hivi sasa ni saa mbili kamili za usiku, hii ni taarifa ya habari kutoka Redio Tanzania Dar Es Salaam,

Kigoma

Waziri Mkuu wa Tanzania Ndugu John Malecela amewataka wakulima wa zao la mawese mkoani Kigoma kuongeza kwa bidii uzalishaji wa wa zao hilo....."

Daaah nimekumbuka sana enzi hizo hahahaha!
 
Na ratiba za kuburudisha zilikuwa zinatolewa kwenye gazeni, ratiba za band, cinema, usoma kwenye gazeti la mfanyakazi, unajua leo niende avalon cinema au kuwaona vijana jazz....

Na kiingilio haikuwa haba kivile ha ha ha
 
Na Beth Shekland ( Skumbuki SP) jamani mnaangalia pale Kilimanjaro Hotel wanvyoanza mashindano ya magari.
Huyo Beth alikuwa enzi za kina DUDU?

Wanaanza na kumalizia Kilimanjaro Hotel.

Apumzike kwa amani, kumbe DUDU ameshatangulia mbele ya haki.

Sikuwa nafahamu, nashukuru kwa taarifa
 
Kwenda sekondari ilikuwa ni heshima kwa jamii inayokuzunguka. Wakati wa kwenda shule husindikizwa na kundi la watu huku umesaidiwa sanduku. Tulipanda treni.

Tiketi tulitunza kwani nauli tulirejeshewa baada ya safari. Makonda wa treni (tt) walikuwa ni wahindi.

Mwl.alipohamishwa shule ilipikwa pilau, pia mashairi yaliimbwa.

Picha tulipiga studio tena baada ya kusevu kwa muda mrefu.... Tofauti na siku hizi ''selfie''.

Tulisikiliza RTD, kwa miziki idhaa ya biashara.

Range rover haikuruhusiwa ku paki benki. Peugeot 504 iliaminika ni gari ya wahuni/majambazi.
Namba za serikali ilikuwa stb, stc, std, stg. Za wahisani ilikuwa tx - plate number nyekundu.

Sikukuu ya saba saba ilifana sana kitaifa ilifanyika. Na mikoa mingine ilishiriki pia.

Vitabu madaftari shule za msingi ilikuwa bure. Daftari likijaa unapeleka kwa mwl.wa darasa anakupa jipya
ole wako karatasi zikutwe pungufu, viboko vilitawala mashuleni na nidhamu ilikuwepo pia.

Wanafunzi shule ya msingi baadhi walikuwa wananyoa ndevu.

Itaendelea.

MUENDELEZO.
Nyakati za sikukuu tulisheherekea pamoja...kama ni Eid hata wakristu walisheherekea na kama ni krismasi hata waislamu walisheherekea.

Cartoon katika gazeti alikuwa ni chakubanga...kwa yeyote aliyenunua gazeti alianza kucheki kibonzo cha chakubanga.....na mitaani utasikia,jamani kuna mtu ameona chakubanga ya leo
kwa aliyeona basi huwasimulia wenzake.

Picha za wacheza mpira katika magazeti zilikatwa vizuri na kubandikwa ukutani hasa kwenye vyumba vya vijana(picha ilikuwa black &white)...uzalendo huu leo hakuna watu ni Man U na chel..nini sijui.

Gazeti la Sani lilikuwa ni burudani tosha kwa enzi hizo,Lodi lofa ,Pimbi,kipepe,Ndumilakuwili.,,na mitaani baadhi ya watu walipewa majina haya.

Kulikuwa hakuna mauaji kama sasa hivi,kwa waliofanya ujambazi walijulikana kiurahisi na wengi walikuwa hawauwi,jiwe Fatuma lilihusika kuvunjia milango.

Ilikuwa nadra sana kwa vijana kufariki,na iwapo jambo hili likitokea basi wazee hukusanyika kwa pamoja na kujadili ''what went wrong''?

Viwanda vingi vilifanya kazi Kiltex,Mwatex,Morogoro shoes,pia kulikuwa na mafuta ya Mara ambayo yalikuwa yakiwekwa kwenye wali au kupikia chapati basi majirani woote watajua.

Kulikuwa na shirika la ndege la Afrika mashariki,liliheshimika sana,nakumbuka kulikuwa na dege kubwa la mizigo liliitwa ''Simba''...baada ya kutoka Dar,KIA na Nairobi basi moja kwa moja mpaka kwa malkia.

Kwa vijana waliobalehe siku ya kulamba papuchi hakuna gesti,biashara huishia katika vichaka,mashamba ya mahindi au mapagale..nyumba ambazo bado hazijakamilika kujengwa.

Kulikuwa hakuna UKIMWI watu walichomwa sindano na zilichemshwa kabla ya kuchoma wengine.

Hospitali ilikuwa bure kwa maana ya Bure kweli.Hutoi hata senti tano.Ingawa za kulipia zilikuwepo pia.

Senti hamsini iliitwa thumuni,sumni.

Kipindi maarufu cha mahoka redioni kilivutia wengi.Mahokaaaaaaa A A A.

Mida ya saa nane nane mchana kulikuwa na kipindi cha kuimba mashairi redioni...kilikuwa kinawaboa watu wengi sana,ila kwa sasa.....

Itaendelea........




 
Nimekumbuka driving sinema jioni tulikuwa tunaenda kuangalia sinema babu kwa kukaa njee
 
Let us kee the records straight. TAMAA YA MWANAMKE ITAKUWA JUU YA MWANAUME. Sio kinyume chake. Hivo ndivo yasemavo maneno yaMungu na ndivo ilivo.

MWANZO 3:16 Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako, na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto, na TAMAA YAKO YAKO ITAKUWA KWA MUMEO, naye atakutawala.
 
Shule za msingi zote walivaa kaptula na sketi za blue tena fupi juu ya magoti!
 
Back
Top Bottom