Hapo kwenye Red panahitaji ufafanuzi ile wanetu waelewe vyema by the way nitaongeza hapa;
- Kuhamishiwa Mtwara au Sumbawanga kwa mfanyakzi ilikua laana tosha
- Tulitishwa kupelekwa Mafya (kisiwani)
- Ukivaa chumpi mpya hasa za Zabron au 007 lazima kale ka chuma kaonekane ili washikaji wajue umenunuliwa mpya
- Matozi waliitwa magwangwe na maranyingi walikua hawatawazi
- Wakuu wa wilaya waliweza kukutandika bakora mbele ya mkeo
- Ubakaji ilikua tendo la kawaida tuuu lilitwa Mande au mtungo
- Tulisafiri kwa juma kwenda Mtwara
- Wakazi wa Kigoma walijivunia biasha ya homela homela wenyewe wakiita pia BIZE
- Form 4 alikua msomi na angeweza oa mtoto wa mwenyekiti wa kijiji
- Ma bwana mifugo walitutibu GONO pia kwa sindano za ng'ombe na tulipoa
- Tulipanda foleni ili tupate kipande cha sabuni ya Ilula
- Chai walikunywa waungwana wa town sis zetu uji kwa asali
Hapo kwenye red mkuu pana maelezo mengi sana. Lakini ni kuwa Nyerere alipendwa, kuheshimiwa, kuwaadmired na kuheshimiwa na kila mtu. Alichokisema kilikuwa ndiyo dira na kilitekelezwa na kila mtu bila ubishi. Alikuwa ndiye chanzo cha fikra ambapo baadaye tuliimba "zidumu fikra sahihi" ambapo kwa sehemu kubwa zilikuwa sahihi kweli. Huyu ndiye alianza kuongoza nchi akiwa mchanga na nchi ikiwa changa pia. Alijitahidi sana kutuunganisha kama taifa kwa kuua ukabila na udini. Alipigigania ili kila mwananchi afaidi kile kidogo tulicho nacho kwa usawa. Alianzisha Azimio la Arusha ili kuhakikisha kuwa kwa sehemu kubwa viongozi wanajali wananchi kwanza kwa kuweka maadili makali ya uongozi. Kwa kutumia rasmali za nchi na misaada kutoka kwa nchi rafiki, alitoa elimu kuanzi ya msingi hadi chuo kikuu na afya bure. Hivo ndizo nyakati ambazo kila kitu kilikuwa kinapatikana shuleni kuanzai daftari, kalamu, vifutio na vitabu bure. Daftari likiisha unakwenda kwa mwalimu anakupa jingine. Hakukuwa na maduka ya dawa enzi hizo kwani dawa zote zilikuwa zinapatinaka katika hospitali bure. Mkuu wengi wetu tunaochangia uzi huu kama sio Nyerere tusingejua hata maana ya Jamii Forums kwani tusingekwenda shule kutokana na umasikini na huenda tungekuwa tulishakufa zamani kwa maradhi kutokana na kushindwa kujitibu kama ilivyo sasa. Hata hawa viongozi wakubwa ambao wanaifisidi nchi wasingekuwa katika nafasi hizo kama si kazi ya Nyerere.
Nyerere alijenga viwanda vingi na mashirika mengi ambamo wasomi na wasio wasomi waliajiriwa. Wakulima walikuwa na uhakika wa soko la mazao yao kwani tulikuwa na viwanda vingi hapa nchini na pia kulikuwa na utaratibu wa kuuza nje wakati huo chini ya Gapex. Mzee yule aliuvunjilia mbali ukabila na udini kupitia elimu na ajira. Ukimaliza shule ya msingi unapelekwa mkoa mwingine kabisa na ukiajiriwa unapelekwa mkoa mwingine kabisa. Kwa mtindo huo tukajikuta tunaoleana na hivyo kuwa taifa moja. Hii ilifanikiwa kutokana na kuvunja uongozi wa kikabila wa machifu ambao katika nchi nyingine umeendelea na kuleta mapigano ya kikabila. Alijenga heshima kubwa sana ya nchi nje ya mipaka yetu hata ikulu paliheshimika sana mpaka akapaita mahali pa takatifu. Tena yeye kwa miaka zaidi ya 24 alikuwa pale bila fensi lakini palikuwa na heshima kubwa sana. Kama binadamu alikiri kuwa kuna maeneo alikosea lakini si kwa kusudi la kujinufaisha bali katika mkondo wa kumsaidia mtanzania masikini na akasema viongozi wanaomfutia wanapaswa kuchikua mema na kuyaacha mabaya ingawa mwishoni mwa maisha yake alisikiktika sana kuwa viongozi wanaacha mema na kuchukua mabaya ikiwa ni pamoja na kuliua Azimio la Arusha. Mzee yule aliteseka sana kuisimamisha nchi bila hata kujipendelea yeye ndiyo maana huwezi kusimama mahali ukasema Nyerere alijinufaisha yeye kwa kuiba au kuifisidi nchi hii. Nyakati zile zilikuwa ni za chama kimoja hivyo angekuwa na roho ya tamaa na wizi kama waliomfuatia angeweza kuchukua hata sehemu kubwa ya Dar es Salaam kuanzia Ubungo hadi Kiluvya na kusema ni eneo au shamba lake. Angekuwa na utajiri wa majumba na mali nyingi nyinginezo bila hata kuwepo mtu wa kumuuliza au kumuhoji kwani hakukuwa na uhuru wa kuhoji kama ilivho sasa. Huyo ndiye Nyerere ambaye nimesema alikua kama Mungu kutokana na hayo niliyasema. Mungu amrehemu, Amini.
Sasa mkuu angalia kimbunga cha madalali, mafisadi, wezi na wauaji waliokuja baada ya Mwalimu walichokifanya walipoingia ilkulu:
- Wakalivunjilia mbali Azimio la Arusha na kuanzi kujitajirisha wao na familia zao
- Wakajiuzia nyumba za serikali alizojenga Nyerere kwa ajili ya watumishi wa serikali
- Wakapiga mnada viwanda, mashamba na mashirika yote ya umma aliyoanzisha Mwl ikiwemo benki iliyokuwa kubwa kabisa ya NBC
- Ikulu palipokuwa pa takatifu wakapageuza pango la wanayang'anya na sehemu ya biashara. Kutoka hapa ndipo dili za EPA, Richmond, Rada na hatimaye Escrow zilipopigwa. Wake zao wakatumia ikulu na rasmali zake kuanzisha NGO zao kwa migongo ya masikini wa nchi hii, Wengine kama haitoshi wakaanzisha na makampuni binafsi na wake zao na kujimilikisha baadhi ya mashirika ya umma kwa bei ya kutupa
- Migodi yote wakabinafsisha
- Elimu na afya vikageuzwa biashara ndio maana si ajabu ukasikia mtua anaomba msaada wa Sh laki 3 au 5 ili akatibiwe katika hospitali ya umma kama Muhimbili na kukosa hatimaye kufa lakini wakati huo huo utaambiwa kuna mtu analipwa sh. 1.5 kwa siku kwa kusimamia ufungaji wa viti vya bunge la katiba mpya
- Wakulima wakaachwa wajifie wenyewe kwa kukosa masoko ya mazao yao lakini hata pale wanapopata masoko serikali inawazuia kuuza kwa kisingizio cha njaa au magendo wakati huo huo ikichukua ushuru mkubwa na kuwaacha wakulima na umasikini wa kudumu
- Serikali ikageuka muuaji wa raia kwa kuwalipiua kwa mabomu na risasi za moto wanapiokuwa katika shughuli zao za amani za kisiasa na kijamii. Mifano ni mingi - Zanzibar, Arusha, Morogoro, Iringa, Songea, Mbeya, operesheni tokomeza nk
- Uongozi ukageuzwa ni biashara badala ya utumishi. Wakajiita waheshimiwa. Wenye pesa sasa ndiyo wanaoununua uongozi na wengi wako kazini na mabilioni yao wakiwanunua wananchi kwa njia mbali mbali ili wawa unge mkono
- Chama kilichokuwa cha wakulima na wafanyakazi kikageuzwa kuwa cha wafanyabiasha na matajiri. Sasa hivi ndio ajabu unasikia viongozi wa chama wakihubiri sera za udini, ukabila na ukanda kuonesha jinsi walivyofilisika kisiasa
- Wananchi kufurushwa, kuumizwa katika maeneo ya asili ili kuwapisha wanyama kwa kisingizio cha hifadhi ya wanyama
nk. nk.
Hivyo mkuu hakuna kiongozi anayeweza kupewa heshima kama alizopewa Nyerere kwa kazi kubwa aliyofanya kwa sasa. Sasa hivi si ajabu ukasikia au kusoma kuwa kiongozi mkubwa kabisa anaitwa fisadi, mwizi, mwongo, dhaifu, mwoga, msafiri, omba omba, vasko da Gama, nk nk. Kwasababu hizi ndizo nyakati ambapo wezi wanatetewa kuwa hawakuiba kwakuwa ndizo nyakati ambazo pesa za umma zinageuzwa kuwa za binafsi, ndio nyakati ambazo wezi wanaiba na nyingine wanazipeleka pahala pa takatifu alipopaacha Nyerere, ndio nyakati ambazo unasikia wezi wanapewa muda wa kujirekebisha, ndizo nyakati ambazo wezi wanaambiwa warudishe walichoiba halafu watafichiwa siri na hawatashitakiwa, ndizo nyakati unazosikia tapeli wa serikali(richmond) anakaribishwa pahala pa takatifu alipopaacha Nyerere, ndizo nyakati unazosikia tuhuma zote ovu zianatokea pahala patakatifu. ndizo nyakati unazosikia kuwa watu wanabeba pesa za migao kutoka benki kwa maboksi, lumbesa na mifuko ya sandalusi. Madudu na maajabu yote hayo yangepita mlango gani nyakati za Nyerere? Nina imani majina yatakapotoka tutashangaa mshangao wa kufa kwani hayo ya wenye milioni 10 za mboga, maaskofu na majoka yenye makengeza ni cha mtoto! Time'll tell!