Zaidi ya bilioni 25 zatafunwa; Watendaji waanza kuwajibishwa!

Vocha za mil. 330 zimeibwa
Imeandikwa na Fadhili Abdallah, Kigoma; Tarehe: 24th January 2011


POLISI mkoani Kigoma wamemkamata Ofisa Kilimo wa Wilaya Kasulu, Benard Kazaura kwa upotevu wa vocha za pembejeo za ruzuku zenye thamani ya Sh milioni 330 na watu wengine wanne kwa kukutwa na noti bandia.

Kamanda wa Polisi mkoani Kigoma, George Mayunga alisema juzi kuwa Kazaura na wenzake wanatuhumiwa kuhusika katika wizi wa vocha za ruzuku zenye thamani ya Sh milioni 330 zilizokuwa kwenye gari walilokuwa wakisafiria.

Mbali na ofisa huyo, wengine waliokamatwa kwa tuhuma hizo ni dereva wa Halmashauri ya Kasulu, Dauson Alfred na askari Polisi wawili, Sajenti Kididu na PC Jacob waliokuwa wakisindikiza gari lililokuwa na vocha hizo.

Kamanda huyo alisema kuwa watuhumiwa hao, walikuwa wakisafirisha vocha hizo kutoka Dar es Salaam kwenda Kasulu mkoani Kigoma, na waligundua upotevu wa sanduku moja la vocha hizo wakiwa mkoani Dodoma.

"Watuhumiwa wote mara baada ya kuanza safari kutoka Dar es Salaam walifika Dodoma na kuamua kulala, lakini asubuhi wakati wakiingia kwenye gari kwa ajili ya kuendelea na safari, dereva aligundua moja kati ya maboksi mawili yaliyokuwa na vocha halipo," alisema Kamanda Mayunga.

Alifafanua kuwa baada ya watuhumiwa kugundua upotevu huo, waliamua kutoa taarifa Polisi Dodoma na kuendelea na safari na baada ya kufika Kasulu, walikamatwa kwa tuhuma hizo.

Watuhumiwa wote watafikishwa mahakamani baada ya uchunguzi na kwa hao askari polisi hatua za kinidhamu za jeshi hilo zinaendelea kabla ya kufikishwa mahakamani.

Wakati huo huo, wakazi wawili wa Mwanga mjini Kigoma, Mengi Rajab na Taus Said wamekamatwa mjini Kibondo na noti bandia za Sh elfu kumi zenye thamani ya Sh 960,000 wakati wakitaka kununua bidhaa katika duka moja mjini humo.

Kamanda Mayunga alisema watu hao walifika katika duka la Erick Jacob kutaka kununua bidhaa mbalimbali ambapo baada ya kukusanya walichohitaji, walitoa fedha ambazo zilitiliwa shaka na muuzaji ambaye aliwataarifu polisi ambao walifika na kuwatia mbaroni watuhumiwa.

Mkazi mwingine wa mjini Kigoma Zarina Hamisi amekamatwa na noti bandia zenye thamani ya Sh 220,000 wakati akitaka kununua mafuta ya mawese kwa wakulima.
 
Hii inaonyesha taifa halipo salama tena, manake kila anayepata nafasi wembe ni ule ule UFISADI!

Tafakari na chukua hatua.
 
What rocked the Titanic?

these revelations are just a tip of an iceberg!

attachment.php
 

Attachments

  • tip of an iceberg.jpg
    tip of an iceberg.jpg
    9 KB · Views: 66
Is it possible for Chadema to track these funds in all the districts in tanzania and give us a report? au angalau kwenye zile halmashauri wanazoziongoza?

I guess this is more than the EPA, Richmond, and the like.
 
[h=2]Vigogo watafuna vocha za bil 1.3/=[/h] Monday, 11 July 2011 07:54 newsroom


* Mkurugenzi akiri wizi mkubwa kufanywa
* Hali sasa ni tete, vigogo watupa zigo kwa DC
NA MWANDISHI WETU, CHATO
WAKATI serikali ikiwa katika mkakati wa kuwawezesha wakulima kuendesha kilimo cha kisasa, zaidi ya sh. bilioni 1.3 za pembejeo zimetafunwa wilayani Chato, imebainika. Habari za kuaminika zimesema kuwa mabilioni hayo ya shilingi yametafunwa na baadhi ya watumishi wa serikali wilayani hapa, hivyo wakulima wengi kushindwa kupata pembejeo hizo. Uchunguzi wa Uhuru umebaini kuwa wilaya ya Chato ilipata vocha za pembejeo zenye thamani ya sh. bilioni 1.5 kwa ajili ya wakulima 26,596.
Hata hivyo, imebainika kuwa wakulima waliopatiwa vocha hizo ni 3201 pekee ndio waliopata, ambapo thamani yake ni sh. milioni 154.
Chato ilipokea vocha 26,596 za mbegu ya mahindi yenye thamani ya sh. 265, Vocha 26,596 za mbolea ya kupandia yenye thamani ya sh. milioni 691 pamoja na vocha 26,596 za mbolea ya kukuzia yenye thamani ya sh. milioni 585, lakini ni asilimia 10 tu ya wakulima ndio waliopata pembejeo.
Wakizungumza na Uhuru baadhi ya wakulima pamoja na wadau wa kilimo wilayani hapa, walisema wameshindwa kufikia malengo yao kutokana na kukosa pembejeo, ambazo tayari walitegemea kuzipata na hasa baada ya uhamasishaji mkubwa uliofanywa na serikali.
Mkulima Musa Juma mkazi wa kijiji cha Muranda kata ya Buselesele katika Tarafa ya Bwanga, alisema yeye ni miongoni mwa wakulima waliotakiwa kunufaika na pembejeo hizo lakini hakupata.
Hata hivyo, alisema kuwa jina lake lilikuwa kwenye orodha ya wakulima waliostahili kupatiwa na kwamba, lilionekana limesainiwa kuwa amechukua pembejeo za sh. 150,000.
Pia, imebainika kuwa katika maeneo mengi pembejeo zilipelekwa na mawakala na baadaye zilirejea kuzichukuliwa tena katika vijiji vya Rubambagwe, Katende na Ilemelahuku.
Vijiji vingine vya Mwabaruhi katika kata ya Katende, ambacho kilitengewa vocha 726, lakini zote ziliishia kwa wajanja na vijiji hivyo hazikupata.
Katika uchunguzi huo pia imebainika kuwa kuna baadhi ya vijiji vilipokea pembejeo ambazo hazilingani na idadi ya vocha zilizopelekwa.
Kijiji cha Muranda kilipelekewa mifuko 27 ya mbolea aina zote badala ya mifuko 484 huku Kijiji cha Kitende kilipokea mifuko 10 kati ya 484 wakati vijiji kama vile Busaka na Katete walipatiwa kilo mbili za mahindi.
Ubadhirifu huo unadaiwa kufanya kati ya watendaji wa Vijiji, maofisa wa kilimo wilaya kwa kushirikiana na mawakala sita waliopewa kazi ya kusambaza pembejeo hizo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Hamida Kwikwega, alipoulizwa juu ya kashfa hiyo alikiri kuwepo kwa ubadhirifu mkubwa.
Hata hivyo, alisema kuwa Mkuu wa wilaya hiyo Hadija Nyembo ndiye anayefahamu kwa undani juu ya ubadhirifu huo kwani, ndiye Mwenyekiti wa Kamati ya Pembejeo.
"Kama ni suala la ubadhirifu hilo ni kweli hakuna ubishi kuwa fedha za pembejeo za wakulima zimetafunwa na baadhi ya watumishi wa serikali, tena ni fedha nyingi sana na wakulima waliopaswa kunufaika hawajanufaika na chochote. Hii imeathiri ualishaji wa chakula.
"Wilaya ilipokea sh. bilioni 1.542 kwa ajili ya pembejeo na wakulima 26,596 walipaswa kunufaika, lakini hadi sasa hivi tunavyozungumza wakulima waliopata ni asilimia 10.1," alisema.
Pia, alisema kuwa tayari ofisi yake imewasilisha suala hilo kwenye vyombo vya sheria kwa ajili ya hatua zaidi na kamba, udanganyifu na viongozi kukosa uadilifu ndiyo chanzo cha wizi huo.
Kwa upande wake Ofisa Kilimo wilaya Chato, Charles Ntaki alipotafutwa alisema kuwa hawezi kuzungumzia chochote juu ya sakata hilo kwa kuwa alikuwa katika kikao.
Pia, alisema kuwa kazi yake katika ugawaji pembejeo alikuwa ni katibu hivyo, shughuli yake kubwa ilikuwa ni kuandika tu.
"Unasikia vikao vinavyohusiana na pembejeo, nilikuwa ni Katibu kazi yangu kubwa ilikuwa ni kuandika wanachosema wajumbe na hasa mkubwa wangu hivyo, kama unahitaji kujua juu ya ubadhirifu huo muulize DC ndiye anajua kila kitu mimi mtanionea bure tu…..'' alisema Ofisa kilimo huyo.
Mkuu wa Wilaya hiyo Hadija Nyembo hakuweza kupatikana kuzungumzia ubadhirifu huo, ambapo mwandishi wetu alielezwa kuwa yuko nje ya wilaya kikazi.
Hata hivyo, juhudi za kumsaka ili azungumzie suala hilo zinaendelea hasa ikizingatiwa kuwa yeye ndiye aliyekabidhiwa dhamana.
 
Wawajibishwe haraka. Tena hao Wabunge wanaopoteza muda kujigamba baada ya kupitisha private motion za kuleta bills ambazo

1) Zitatoa Stricter penalties and consequences.
2) Zitakazoharakisha trials.
3) Zitakazowabania dhamana watendaji wanaohujumu uchumi kwa design hizi
 
Back
Top Bottom