Yutong Vs scania Vs ud

kipimo cha haya mabasi huwa ni pale kitonga hasa uanze mlima ukiwa ndani ya happy nation (scania iliyochoka lakini moto) halafu mbele kuna sumry na new force enterprise zote engine mpya, happy nation inakaribia ilula sumry(UD) ndo inamalizia mlima wakati walianza mlima pamoja, scania ni machine hasa ndo maana kuna yutong zimefanyiwa 'modii' na kufungwa machine za scania
 
hivi kuna uwezekano wa kubadilisha engine. Mfano wa zile sumry ukaimplant engine ya scania
 
Ni karibia miaka mitatu sasa toka hizi yutong ziingie tz ila nimejaribu kuangalia yale makampuni yaliyoanza kununua sasa hayafai. Angalia new force zilivochoka sana. Ma ud ya sumry nimetokea kuyapenda na ukifungua web ya sks wanaonesha kuwa Wanaimplant hata ingine za scania kwenye basi,Ila sumry asingeweza chukua scania coz nasikia ni ageNt wa ud. Ila zile body za sumry Nimezipenda sna. Sijapanda gari ambalo ni tamu zaidi ya zile sema ubovu jaman, what is the problem with those buses au n Uendeshaj?
 
Dar express ana scania na benz,kilimanjaro bus ana scania na yutong nadhani hao wamiliki wanaweza tupa majibu sahihi SWOT
 
Scania ni imara na inadumu.bei yake mkasi pia spare zake.yutong cheap sana,nyepesi barabarani,ulaji mafuta mdogo lkn hazidumu kabisa/hazitaki shughuli nzito.Ud ni gari nyanya pia nzito sana road linapokuja swala la mwendo
 
Hakuna mashine ya mchina inayodumu hapa afrika. From china = Kisukari + Presha.
 
kama yutong ni bora kuliko scania, mbona mayutong mengi yaliyo dar wametoa diff iliyokuja nayo na wamefunga ya Scania, umeshapata jibu heehe

Hapo kwenye DIFF ndipo tatizo lilipo , zaidi ya hapo hakuna tatizo jingine cha muhimu ni kuzipumzisha tu, na service kwa wakati, safari ndefu hizi gari haziwezi.
 
yutong zinatatizo la diff hazihimili sana na wengi wanabadilisha wanaweka ya scania .. fuel consuption ya yutog ni kidogo , speed scania ina 120 kph na yutong ina 140 kph ...
 
Yutong zinafaa kwa safari fupi fupi za Dar - Tanga ama Dar - Moro, ama Arusha - Moshi n.k. hazitaki orduous duties kama zile za Dar- Mwanza ama Tunduma - Dar au Arusha - Mbeya. Si imara kwa duties za namna hiyo. Ni kweli kwamba Yutong hutumia mafuta kidogo kwa kilometa kuliko scania.
 
Nissani UD ni kwa safari ndefu za nje ya nchi na UD Usichezee tambalale na kwenye miteremko hata scania haifuati na ndio maana ukiangalia mabasi yanayoenda malawi,mwanza via nairobi,Uganda,Zambia hadi S.A ni UD yanauwezo wa kutembea muda mrefu,Scania kwenye milima sawa ina turbo ila safari ndefu bila kupumzika haitachukua muda mrefu itakuwa imekwisha,Yutong ni safari fupi kwa kweli ila wafanyabiashara wa TZ wanapeleka safari ndefu kama Mwanza,Kyela,Songea na Tunduma ila hayatokaa muda mrefu,Ila usafiri wa Tz unategemea na mkoa unaenda ukizingatia features zilizopo ndio maana makampuni mengi ya usafiri yanakufa kwasababu wanafuata abiria wanataka nini,I like dar express route zake ni zilezile dar-Arusha kazidi nairobi kutokana na magari anayotumia scania body marcopolo
 
kama unataka kujua yutong inakimbia kuliko scania panda haya mabus ya greenstar dar-mwanza route,utapata jawabu,inshort yutong zinatembea mkuu,dont try kushindanisha scania na yutong

nilitaka kuandika kama wewe..ile njia hizi marcopolo na scania mpya huwa tunaziacha mbali sana na yutong za green sema tatizo huwa hazitulii njiani na driver asipokuwa mwangalifu mkipata ajali kwa speed ile na kwa bodi ile ya karatasi hatoki kiumbe anayepumua.
 
nilitaka kuandika kama wewe..ile njia hizi marcopolo na scania mpya huwa tunaziacha mbali sana na yutong za green sema tatizo huwa hazitulii njiani na driver asipokuwa mwangalifu mkipata ajali kwa speed ile na kwa bodi ile ya karatasi hatoki kiumbe anayepumua.
umeona eeh nilipanda siku moja,kutokana na speed ikabidi niwaulize wahusika wamefunga nini kwenye zile bus,kumbe wameweka difu ya scania 124L
 
Kwa uimara Scania inaonoza kwa mbali kuliko Yutong, Zipo bus za 1990 zinatembea bila tatizo. mchina hadumu barabarani, nadhani mnakumbuka zila bus zenye rangi ya bendera ya Marekani zimekaa barabarani miaka 3 na sasa hazipo. Pia zile buffalo za kichina zilifanya kazi kwa miaka 2 zikafa. Scania ni moto, usipime.

naunga mkono hoja scania ni imara kwa kila kitu watu mnaangalia kukimbia mna maana gani na barabara zetu za makufuli speed inayotakiwa ni ya kawaida kwa barabara zetu speed inayotakiwa isizidi 120 kutokana na barabara zetu ila utakuta basi lipo 140 to 160 hii ni hatari kwa abiria halafu mnasifia kuwa inakimbia kumbe mnajitafutia vifo, asilimia kubwa ya ajali za barabarani hasa mabasi utasikia speed wakati inakimbia abiria wanafurahia saaana na wakiwapita wenzao ndio vifua vinawajaa kwa furaha huku mkijisemea mchina noma, hayo magari ya kichina baada ya miaka mitano mtaniambia yatakavyochakaa angalia hizo scania zina muda gani na zikoje. yale yale tuliokuwa tunasema vya bei rahisi vinagharama yake sana ila watu hawajui hilo.
 
620.jpg

546.jpg


SCANI NI GLOBAL BRAND WAKUU, Na iko Dunia nzima kuanzia sourh America, USA, ULAYA NA ASIA, ila YUTONG ZIKO AFRICA TU
 
... Nina Maswali kuhusu hii Mada.
Haya mabasi ya Scania tunaoyaona ya akina Dar Express yanatoka moja kwa moja Sweden, Brazili ama Afrika Kusini?
Tunasema Yutong ina bei nafuu kuliko Scania, Bei ya Wastani ya basi la Scania single/double deaf ni shillingi ngapi as opposed to bei yaYutong?
Unaponunua basi la Snania kwa mfano, unakwenda mwenyewe Afrika Kusini ama unakwenda tu pale Kibaha kwenye karakana yao na wao ndio wanakuagizia na we unalipa kwa pesa ya madafu hapa hapa?
Kama umenunulia Afrika kusini kwa mfano, Basi lako linaendeshwa kutoka huko hadi hapa ama linapakiwa ndani ya Meli na wewe unaenda kulichukulia KIbaha??
Nitashukuru kwa kueleweshwa:
 
... Nina Maswali kuhusu hii Mada.
Haya mabasi ya Scania tunaoyaona ya akina Dar Express yanatoka moja kwa moja Sweden, Brazili ama Afrika Kusini?
Tunasema Yutong ina bei nafuu kuliko Scania, Bei ya Wastani ya basi la Scania single/double deaf ni shillingi ngapi as opposed to bei yaYutong?
Unaponunua basi la Snania kwa mfano, unakwenda mwenyewe Afrika Kusini ama unakwenda tu pale Kibaha kwenye karakana yao na wao ndio wanakuagizia na we unalipa kwa pesa ya madafu hapa hapa?
Kama umenunulia Afrika kusini kwa mfano, Basi lako linaendeshwa kutoka huko hadi hapa ama linapakiwa ndani ya Meli na wewe unaenda kulichukulia KIbaha??
Nitashukuru kwa kueleweshwa:

Mkuu nijuavyo mimi SCANIA ZINATOKA SWIDEN ila Brazil na south Africa wao wanaunda BODY ZA MARCOPOL
 
umeona eeh nilipanda siku moja,kutokana na speed ikabidi niwaulize wahusika wamefunga nini kwenye zile bus,kumbe wameweka difu ya scania 124L
Haya sasa,kumbe mpaka ifungwe difu ya scania!nilitaka kushangaa scania inyanyaswe na yutong!labda huko mwanza,manake route ya mbeya happynation huwa anafanya kuzitanguliza greenstar,muro,saibaba,new force na super Feo kwa kuhofia kupigwa torch na trafiki wanoko wa Iringa,ila akiingia stand ya makambako akichomoka anawatoroka yaani mnaingia mbeya yeye ndo anatoka kuosha gari kwa ajili ya safari ya kesho.
 
higer bus ni kampun ambayo inacorporate na scania, juzi kati nimepanda machinga bus la mtwara ambalo ni higer bus jamaa wa yutong walikuwa Wanatufukuzia watupate wapi. Tuliingia mtwara Stendi saa saba na nusu wakati wengine waliotufuata Walianza kuiona saa tisa. Jaman scania ni funiko. Tusijaribu kulinganisha haya mabasi yetu Yaliyochongwa manzese na kitu yutong za kiwandani, wala Marcopolo ambazo nyingi ni za kuanzia miaka ya tisini. Tu compare kitu new brand ya scania na new yutong. Mbona kuna kitu scania ya carrier juu ya kwenda Liwale ya miaka ya tisin bado inakimbizana na hizi Yutong (wifi)
 
Back
Top Bottom