Yutong Vs scania Vs ud

Na kwa taarifa tu, mabasi ya sumry yanayokufa njiani siku zote ni nissan ud na hino na wala si yutong, maana sumry hana yutong hata moja, na mabasi yanayokufa njiani mengi ni scania na kama kuna yutong utakuta ni chache na hata hayo machache utakuta wakati wa utengenezaji wamiliki au mafundi wao wametumia vipuli fake.

kibaya zaidi wamiliki wa mabsi aina ya scania walio wengi wanashindwa kulipa madeni yao tofauti na wanaotumia Yutong,

Huo ni ushauri wa dhati wenye nia ya kuruzindua wabongo,

Simba
kwenye suala la kuharibika wakati wa safari, yutong hazina guarantee mkuu, afadhali uharibikiwe na skania! Nimewahi kuharibikiwa na basi la Green star kuja mwanza, hapo shinyanga, tulilala hapo hapo! Na kwa taarifa, yutong za green star kuja mwanza zimechoka sana! zinalaza watu njiani mara kibao...wameleta mpya chache ku-backup ila hali sio nzuri, yutong ni janga mzee...hazina maana! zikikorofisha hamuondoki...systems zake ni electrified, haiwezekana kufanya utundu wa kienyeji kama kwa scania.
 
Katika hayo magari kila kitu bora kipo Scania, ila jamaa zako hata akili zao zishakuwa za kichina.
Nasikia kiwanda cha Scania kimechukuliwa na wachina tayari na wanachofanya ni kuendeleza pale wenyewe walipoachia.
 
Samahani kidogo....na hawa Faw vs Scania kwa upande wa maroli yupi mkali???
 
Hahaha mkuu pole, naona kama umechukia, nilikuwa nakutania kuwataja wafanya wa scania na wala sipajui hapo scania kibaha.

Ila mimi ni researcher ndugu yangu na ninazo statistics na si vema kuzitaja ila hata hao uliowataja nina uhakika watakubaliana nami, maana ni kweli wanazo scania na wanajitahidi tu, lakini nina wasiwasi ikiwa wakiongeza wataongeza kwa kununua scania.

Ningependa nikaishia hapo isije kuonekana nina ugomvi na scania ili hali hata kuwajua siwajui ila ninajua mbinu za ndugu zetu za hizi nchi za uaya wanavopenda kuponda chochote kisichotoka kwao. Wanangangania sifa walizokuwa nazo enzi hizo ambazo hawana. Na tukubali era yao kibiashara ishapita hii ni era ya wachina na ili mradi tuhakiki tunachonunua ni kizuri basi tuende na mfuo kwa kuangalia maslhi yetu na sio ya kuiga,

Smba

I think wewe umekuwa mtanzania sana. Mbona umetoa wazi mifano mingi kuonesha ubora wa Yutong as compared to Scania sasa inakuwaje unashindwa kutoa reseach findings zako.
As long as hakuna mtu alio fanya research ubishani wa YOUTONG VS SCANIA stats zake zitakazo letwa hapa itakuwa story za vijiweni tu ambazo aanyeongea sana ndo anashinda.
Unatumbi consumption ya mafuta tupe data authentic sio kwassbu we umeona yutong ulopanda likp hivo basi uka conclude

Eti speed, youtong linakimbia kuliko scania, thst statement is so subjective. Watu waje na stats hapa kuonesha Youtong inakimbia zaidi kuliko scania sio eti kwassbabu superfeo wanatumia Yutong na linawahi kufika Songea kuliko mabasi yanayo tumia scania. Bt mbona Ally's inatumia scania lakini lakini hyo njia ya mwanza, shinyanga hakuna mtu anayeigusa... So based on these subjective reason za mtu moja moja its not ryt to come hapa with that conclusion. This is Jf
 
Mhh???? Hapo kwenye ally's na greenstar. Ile ishu nyingine, naomba tusidanganywe na speed meter, kuna siku nimeifukuzia na corola mpaka 140 bado sikuuikamata . nadhan sisi wenyewe ndo hatujui keundesha biashara zetu Vizuri ila hajanishawishi mtu kununua yutong. za greenstar hazina miaka hata 2. LaKini ukiziangalia huwezi zifananisha na abood au zile za hood kwu uzuri
 
yutong-zk-06.jpg

kuna mtu anasema ulaya hamna yutong,hii ni nin?
 
wadau kuna kaubishi kapo hapa kijiweni kwetu kuhusu efficiency ya haya magari especially mabasi. Ubishi ume-base sana kwenye
1) speed ya mabasi, wengi wanaSema yutong ni funiko kuliko scania na ud.
2) ubovu- wamerate kuwa ubovu mchina anaongoza na relate kipindi yalipoingia Yalilaza watu njian nikiwemo na mimi. Ud wanatolea mfano sumry anavoPotea kwenye ushindan.
3)oil consumption. Mchina consumption yake iko chini kuliko wote. je ni kweli
NaOmba wadau na wajuzi wanisaisidie kwasabab nahitaJi kujua ubora wa haya Magar na hata wadau wengine ambao wanaweza kutaKa kuinvest kwenye biashaRa ya magari itawasaidia

Kama mmeweza kubishana, ina maana mnavyo vitu ambavyo kila upande unaamini ndio FACTS.

Labda sasa niwaulize swali, yupo kati yenu hapo kijiweni kwenu ambaye alishawahi kumiliki aina zote mbili angalau aseme kwamba ubishi wake una base kwenye experience?
 
hizi tutong zipo za matumizi ya mjini kama ile ya buffallo na zipo nyingine kwa matumizi ya barabara na mazingira magumu na scania hivyo hivyo .unapotaka kufanya uamuzi wa kununua usivutiwe na muundo ,utaelezwa .pili mafuta .ulaji wa mafuta ni kitu cha kuzinagatia ,engine oil inatumia kiasi gani ,formula iko hivi kama bodi ni nyepesi hutumia mafuta kidogo ,kama bodi ni nzito hutumia mafuta mengi hadi kuchanganya .mfumo wa gea pia huchangia gari kutumia mafuta mengi ,scania ina gea 8-12.yutong model zk3..ina gear 6.injini ni piston 6 ,scania ina piston 8 hivyo uwiano wa mgandamizo hadi kutokea muwako ni mkubwa ,yaani mafuta yanakandamizwa na piston yatatumika mengi .mambo ya transmission haya ni matatizo ya kiufundi yanarekebishika .
 
hizi tutong zipo za matumizi ya mjini kama ile ya buffallo na zipo nyingine kwa matumizi ya barabara na mazingira magumu na scania hivyo hivyo .unapotaka kufanya uamuzi wa kununua usivutiwe na muundo ,utaelezwa .pili mafuta .ulaji wa mafuta ni kitu cha kuzinagatia ,engine oil inatumia kiasi gani ,formula iko hivi kama bodi ni nyepesi hutumia mafuta kidogo ,kama bodi ni nzito hutumia mafuta mengi hadi kuchanganya .mfumo wa gea pia huchangia gari kutumia mafuta mengi ,scania ina gea 8-12.yutong model zk3..ina gear 6.injini ni piston 6 ,scania ina piston 8 hivyo uwiano wa mgandamizo hadi kutokea muwako ni mkubwa ,yaani mafuta yanakandamizwa na piston yatatumika mengi .mambo ya transmission haya ni matatizo ya kiufundi yanarekebishika .
ile ya buffalo ni ZONDA na sio YUTONG mkuu!
 
Wandugu yutng engine zake ni madhubuti asikudanganye mtu. ni za kimarekani toka magari ya MAN. MBIO NDO NYUMBANI KWAKE HAKUNA CHA MARCOPOLO WALA UD.
we ndugu inaonekana kuwa umetumwa na wachina na hata hoja yako haina mashiko. hebu nenda Iringa panda Yutong halafu mbele yenu ikae scania yeyote au hata nyie mtanglie wakati wa kupanda kitonga halafu uone mziki wa turbo ya scania na ule mluzi wake(turbo) hapo ndio utasema kuwa scania ni noma. acha kudangaya watu lakini. nimepanda new force,green star(zote hizo ni yutong) na hakuna kitu when it comes to Kitonga but scania ooh yeah kama kushuka vile cause pia nimepada scandinavia by then,hood,happy nation na Nganga. wacha kabisa.
 
yutong hawezi kuikamata scania hata siku moja labda km scania imechoka
 
Unapozungumzia ubora na uimara huwezi hata siku moja kulinganisha Scania na Yutong. Scania iko juu kwa kila kitu. Ikumbukwe kuwa kampuni nyingi za kutengeneza magari za China, ikiwa ni pamoja na Yutong, zimeanzishwa hivi karibuni na nyingi zinatumia teknolojia zilizoazimwa aidha Japan au Ulaya. Kwa mfano, haya mabasi ya Yutong (yenye injini mbele) Mchina amechukua teknolojia ya Volvo, hususan iliyotumika kuunda mabasi ya Volvo B7. Hata hiyo, ubora wa mabasi ya Yutong ni wa kiwango cha chini ukilinganisha na Volvo. Kuhusu mbio na uwezo wa kupanda milima, hii inategemea na nguvu ya injini ya basi husika. Injini ya Yutong ina uwezo wa horsepower 260. Ni wazi kwamba Yutong italitimulia vumbi basi la Scania lenye injini yenye uwezo wa horsepower 220, kwa mfano yale mabasi ya Scania F94 ya Hood. Lakini Yutong haiwezi kusogelea Scania F94HB za Abood ambazo injini zake zina uwezo wa horsepower 310. Scania hivi sasa ina modeli ya mabasi ya F330 yenye horsepower 330. Haya yana uwezo wa kuipita Yutong kama imesimama iwe tambarare au kwenye milima. Kama alivyosema mdau mmoja aliyetangulia, moja ya udhaifu mkubwa wa Yutong na ubovu wa ekseli ya nyuma. Wamiliki wengi huondoa ekseli hizo zikiwa bado mpya kabisa na kufunga za Scania.
 
Back
Top Bottom