Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

Lowasa hawezi kua Rais wa nchi hii inayoongozwa kidini,labda wengi wetu tumesahau kua baada ya uongozi wa Rais muislam anayefuata kama akiwa mkristu ni lazima awe Mkatoliki,Lowasa siyo mkatoliki naye anajua hivyo ndiyo sababu amekua akitoa harambee nyingi makanisani kutaka kuwashawishi wakatoliki wamkubali.
 
Nani kakuambia Lowassa ni Mmasai,au kwa kuwa anaishi Monduli jimbo lenye Wamasai wengi?
Kwa wale wanaopenda kupotosha ukweli basi mjue Lowassa ni MMERU na sio Mmasai!
Wamasai ni watu waadilifu mno,na wasio na Ukabila na Ubaguzi km wa Lowassa anaejaribu kutugawa watu wa Arusha haswa Wachagga na Wamasai. Ushindwe Mmeru ktk jina la Yesu.

ma------ na ukabila.
 
Namkubali slaa. Ila magamba wakimsimamisha Lowasa namchagua, hata kama ni mwizi jamaa ni mchapakazi, ni mtendaji hasa, mambo mengi yatakuwa poa kuliko yalivyo sasa, huu ni ukweli mchungu
 
kama angekuwa ni mtu wa watu mbona mwaka 1995 na 2005 hakuwemo kwenye nafasi za juu za wagomea urais wa ccm? bora akae kando king'ang'anizi cha nini?
 
CCM inajiandalia mafuta ya kujikaangia yenyewe kwa kuendekeza makundi ndani ya chama.Ambapo kila kundi lina mtu wake ambae wanaamini kuwa anafaa kuwa kiongozi na atakaposhindwa kwenye kura za chama hicho watu wake hawataridhika na kushindwa huko hivyo wataungana na wapinzani kwa kulipinga kundi lililoshinda ili wakose wote.
 
Hawezi kutinga magogoni kama rais wa nchi,atatinga magogoni kwenda kuomba msamaha kwa dr slaa ili hasipelekwe segerea kwa madudu ya richmond na epa,kwani akigombea lowasa tu dr slaa kaingia ikulu.

Napoleon Bonaparte aliwahi kusema "Never interrupt your enemy whe he is making a mistake".....

Adui yako akiwa anafanya makosa usimgutue...Mwache ajikaange kwa mafuta yake mwenyewe.Usipunguze moto wala kutia maji.
 
January makamba anafaa kuwa kiongizi wa juu serikalini pale alikoaea mzee y m
 
Nitafurahi sana iwapo CCM itapitisha jina la Edward Lowasa kuwa mgombea wao wa urais 2015 kwani kufanya hivyo Chadema hawatahitaji kufanya kampeini yoyote wala kutumia Helikopita kuzunguka nchi nzima, kwani itakuwa kama baiskeli inavyoteremka mlimani, hakuna kunyonga ni vuuuuuuuu mpaka Ikulu. Lowasa ni mmoja wa wana CCM waliyopingwa vikali na Baba wa Taifa hayati Mwalimu JK Nyerere kugombea uraisi, mwingine aliyepingwa alikuwa ni rais Kikwete na hakuna mtanzania ambaye hajaonja adha/shida ya kumchagua Kikwete kuwa rais, ni majuto makubwa. Sidhani kama watanzania watarudia tena kumchagua mtu ambaye Nyerere alimkataa, huu ni wakati wa Chadema kushika hatamu (chama mbadala - kama alivyotabiri Nyerere) -TUMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUMKATAA EDWARD LOWASA
 
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kauli hii ya Makamba ni muendelezo wa kile kinachodaiwa kwamba Kambi ya Lowassa ya Urais inachanja mbuga kuelekea Ikulu hapo 2015.

Source; Radio Free Afrika tuzungumze Magazeti.
Unategemea nini kutoka kwa mzee makamba? historia ya mafanikio yake imejengwa katika kujikomba na kujipendekeza. Watu wa aina yake hawana uzalendo wa nchi bali wanasukumwa na tamaa za matumbo yao na wala siyo hoja za msingi wanazosimamia. Wako tayari kusaliti nchi kwa maslai ya matumbo yao na ya vizazi vyao. Hakuna mtu yeyote mwenye uzalendo wa kweli atakayesimama kumtetea EL kuwa ni muadilifu isipokuwa tu kama anajikomba ili akumbukwe kwenye ufalme ulioko kwenye ndoto za EL. Watanzania wezangu muda umefika sasa wa kutetea kile unachokiamini hata kama ukilazimika kula majani simama imara na huo ndio uzalendo wa kweli. Shime wazalendo tupinge mafisadi na wote wanonuka harufu ya rushwa wasiingie katika ikulu yetu.
 
Makamba aliachishwa ukatibu, siyo mstaafu! Kwa mtu aliyeshindwa kutekeleza majukumu mpaka akaachishwa kazi hawezi kamwe kumjua mtu anayefanya kazi vizuri. Makamba atakuwa anamuona Lowasa katika upeowake wa kuchmbua mambo amboko kulimfanya aachishwe kazi.
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kauli hii ya Makamba ni muendelezo wa kile kinachodaiwa kwamba Kambi ya Lowassa ya Urais inachanja mbuga kuelekea Ikulu hapo 2015.

Source; Radio Free Afrika tuzungumze Magazeti.
 
Wapiga kura Mataahira wamebakia wachache sana Tanzania na wenye akili timamu wameongezeka mara dufu (exponentially).Mwaka 2015 utakuwa ni mwaka tofauti kabisa kwa Abdul Lowassa kwasababu atakwenda kukutana na sisi Wapiga kura wenye akili timamu na hapo ndipo safari na ndoto zake za siku zote za kutaka kuingia Ikulu ili kufanikisha dili zake na za jamaa zake zitakapokuwa zimekufa rasmi.Trust me Makamba Senior,Your buddy Lowassa will never be the President of this Country as long as we sane Tanzanians live,Never!Tulipuuza onyo la Mwl Nyerere kwa JK leo hii tunaishi kwa majuto makubwa,Tutakuwa zaidi ya Mataahira tukirudia tena makosa ya kusahau onyo la Baba wa Taifa kuhusu Lowassa na kumpeleka Magogoni.Nahisi haya maumivu tunayayapata chini ya Utawala wa Mbayuwayu ni nafuu ukilinganisha na yale tutakayoyapata chini ya Fisi.Tutajuta tukifanya kosa la tukimpeleka huyu Fisi Buchani (Magogoni).
 
Magamba wakimpa EL kupeperusha bendera 2015 njia itakuwa rahisi sana kwa CDM kuingia Magogoni......!!
 
tuombe sana Mungu! Mungu hashindwi na chochote, atatuonyesha yupi anafaa
 
Mlie tu mbona mnataka kutudanganya kwa kumsafishia njia sasa ni zamu ya wengine hivi rafiki wa lowasa wanaompa hela chafu za kutoa misikitini na kanisani atawalipa nini akipata urais? atauza nchi zaidi ya richmond
 
CCM hamna ujanja, chagueni moja either EL awe mgombea wenu for 2015 au chama kife rasmi kama mkithubutu kukata jina kama mlivyozoea.

CCM hawana Uthubutu wa kukata jina lake.Kama kumfukuza Diwani tu hawawezi ndio itakuwa Lowasa.
 
Makamba aliachishwa ukatibu, siyo mstaafu! Kwa mtu aliyeshindwa kutekeleza majukumu mpaka akaachishwa kazi hawezi kamwe kumjua mtu anayefanya kazi vizuri. Makamba atakuwa anamuona Lowasa katika upeowake wa kuchmbua mambo amboko kulimfanya aachishwe kazi.

Mkuu usiulize uadilifu kwa mwalimu mkuu wa shule msingi tuliyeambiwa aliachishwa kazi kwa kumrubuni mwanafunzi wake kimapenzi huko Tanga na hajawahi kukanusha
 
Wapiga kura Mataahira wamebakia wachache sana Tanzania na wenye akili timamu wameongezeka mara dufu (exponentially).Mwaka 2015 utakuwa ni mwaka tofauti kabisa kwa Abdul Lowassa kwasababu atakwenda kukutana na sisi Wapiga kura wenye akili timamu na hapo ndipo safari na ndoto zake za siku zote za kutaka kuingia Ikulu ili kufanikisha dili zake na za jamaa zake zitakapokuwa zimekufa rasmi.Trust me Makamba Senior,Your buddy Lowassa will never be the President of this Country as long as we sane Tanzanians live,Never!Tulipuuza onyo la Mwl Nyerere kwa JK leo hii tunaishi kwa majuto makubwa,Tutakuwa zaidi ya Mataahira tukirudia tena makosa ya kusahau onyo la Baba wa Taifa kuhusu Lowassa na kumpeleka Magogoni.Nahisi haya maumivu tunayayapata chini ya Utawala wa Mbayuwayu ni nafuu ukilinganisha na yale tutakayoyapata chini ya Fisi.Tutajuta tukifanya kosa la tukimpeleka huyu Fisi Buchani (Magogoni).

Wenzio tunamfariji asife kwa Kihoro wewe unampa za uso.Lowasa ana Matumaini makubwa na amepoteza Fedha nyingi sana,anahitaji Maneno ya Faraja.
 
Namkubali slaa. Ila magamba wakimsimamisha Lowasa namchagua, hata kama ni mwizi jamaa ni mchapakazi, ni mtendaji hasa, mambo mengi yatakuwa poa kuliko yalivyo sasa, huu ni ukweli mchungu

Mgunduzi foreva,
Mwanafalsafa mmoja alisema, kama binadamu hana kitu anachokiamini na kuwa tayari kukifia, ana matatizo. Nakushauri kama unamkubali Slaa, pigania unachokikubali hadi tone la mwisho.
 
Naamini ule usemi usemao wazazi wetu wakifikia umri wa uzee wanakua na "akili za kitoto"..
 
Back
Top Bottom