Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

sokoinei

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
1,832
Reaction score
566
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kauli hii ya Makamba ni muendelezo wa kile kinachodaiwa kwamba Kambi ya Lowassa ya Urais inachanja mbuga kuelekea Ikulu hapo 2015.

Source; Radio Free Afrika tuzungumze Magazeti.
 
Makamba ni miongoni mwa watu ambao walimrubuni Mkapa baada kupewa kitu kidogo kumchagua EL awe Waziri kipindi kile kwa hatushangai hiyo kauli na Mwendelezo tu wa sinema yao ya ufadhili wa ufisadi ndani ya ccm-Yaani hilo zee limeishi na Nyerere hata haoni aibu kuwapigia kampeni watu wasio waadilifu?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kwa ujumla kwenye swala la ufisadi huwezi kumtenganisha el na sisim, ila kwa mwendo anaokwenda nao nihakika masai anaelekea kutinga magogoni
 
Habari wana bodi,hapa siandiki mengi, lakini ya mzee Makamba kwamba Lowasa ni mtu wa watu ni ya kusafisha njia kueleka 2015 pasi na shaka yoyote,sasa ni hivi mimi nitagombea ubunge lakini kama huyu mtu atagombea urais, nitageuka frontier kufundisha watanzania wote madhara ya kuwekwa huyu mv, kwanza najua ameingia mkenge maana anayo yafanya ni kinyume cha upendo hata unao hubiriawa na mwenge kabla ya Mungu.

Walah nasema, ccm kama mkimleta EL, vita yenu haitakuwa na CDM pekee, bali wazalendo wote. Mashaka juu ya mtu huyu ni mengi, itoshe tu kusema kwamba hafai hata.
 
Kwa ujumla kwenye swala la ufisadi huwezi kumtenganisha el na sisim, ila kwa mwendo anaokwenda nao nihakika masai anaelekea kutinga magogoni

Jamaa anaenda kimya kimya. Hapigi kelele yeye ni harambee kwa kwenda mbele
 
Kwa ujumla kwenye swala la ufisadi huwezi kumtenganisha el na sisim, ila kwa mwendo anaokwenda nao nihakika masai anaelekea kutinga magogoni

Nani kakuambia Lowassa ni Mmasai,au kwa kuwa anaishi Monduli jimbo lenye Wamasai wengi?
Kwa wale wanaopenda kupotosha ukweli basi mjue Lowassa ni MMERU na sio Mmasai!
Wamasai ni watu waadilifu mno,na wasio na Ukabila na Ubaguzi km wa Lowassa anaejaribu kutugawa watu wa Arusha haswa Wachagga na Wamasai. Ushindwe Mmeru ktk jina la Yesu.
 
Hawezi kutinga magogoni kama rais wa nchi,atatinga magogoni kwenda kuomba msamaha kwa dr slaa ili hasipelekwe segerea kwa madudu ya richmond na epa,kwani akigombea lowasa tu dr slaa kaingia ikulu.
 
Kwa ujumla kwenye swala la ufisadi huwezi kumtenganisha el na sisim, ila kwa mwendo anaokwenda nao nihakika masai anaelekea kutinga magogoni

napenda watu wenye maono kama wewe..Lowassa ni strategist sana...2015 October anakabidhiwa nyago...
 
Hawezi kutinga magogoni kama rais wa nchi,atatinga magogoni kwenda kuomba msamaha kwa dr slaa ili hasipelekwe segerea kwa madudu ya richmond na epa,kwani akigombea lowasa tu dr slaa kaingia ikulu.

wewe nawe..mimi ni chadema damu lakini akiwekwa Lowassa sijui na Wenje kugombea urais namchagua Laigwanan
 
CCM hamna ujanja, chagueni moja either EL awe mgombea wenu for 2015 au chama kife rasmi kama mkithubutu kukata jina kama mlivyozoea.
 
Kwa ujumla kwenye swala la ufisadi huwezi kumtenganisha el na sisim, ila kwa mwendo anaokwenda nao nihakika masai anaelekea kutinga magogoni

Inatosha mpendwa Naghenjwa,naomba useme masai anakwenda kuwa mgombea kupitia CCM sio kwenda magogoni,magogoni 2015 tunampa mtu na Chama kiadilifu sio hichi kinachoshindwa kununua vitanda mahospitalini na kuishia kuahidi bajaji kama ambulance za kubebea wake zetu wajawazito.....
 
Lowasa tayari njia ya kwenda Ikulu ni nyeupe kuliko Zuma wakati anagombea Urais.
 
Atawapurura vinyweleo mpaka mkome.. Muulizeni Mwakyembe..

... na mzee six alikoswakoswa wacha aanze kupayuka hovyo mpaka anagombana na igp, teheh teh chezeya janjawig weye, limeivuruga kambi ya wanyakyusa yoote chaliiii...
 
Back
Top Bottom