Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

Yusuf Makamba: Lowassa ni mtu wa watu!

Majambazi,wangoa kucha na meno na mafisadi nao pia ni watu.
nazani hayo makundi ndio haswa huyo mzee anayasemea
 
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kauli hii ya Makamba ni muendelezo wa kile kinachodaiwa kwamba Kambi ya Lowassa ya Urais inachanja mbuga kuelekea Ikulu hapo 2015.

Source; Radio Free Afrika tuzungumze Magazeti.
Birds of the same feathers fly together!!!

Hatujamsahau Yussuf Makamba, kinara wa kukiua Chama cha Mapinduzi hadi kikaketi chini, hasa wakati wa uchaguzi wa 2010.

kati ya makatibu wakuu bomu waliowahi kuiongoza CCM yeye ni Nambari Wani!!!

Sasa leo akibuka na kumsifia Lowassa a.k.a "Edwatalib", mutu ya mapesa kwa wadini, hatushangai sana maana upeo wa Makamba unajulikana.

Zaidi zaidi inabidi tu apumzike kwa amani na aendelee na miradi yake aliyofadhiliwa na akina Manji Morogoro.
 
Sheikh nani vile, jamaa ameslimu kwa ajili ya kura za waislamu.
 
Nani kakuambia Lowassa ni Mmasai,au kwa kuwa anaishi Monduli jimbo lenye Wamasai wengi?
Kwa wale wanaopenda kupotosha ukweli basi mjue Lowassa ni MMERU na sio Mmasai!
Wamasai ni watu waadilifu mno,na wasio na Ukabila na Ubaguzi km wa Lowassa anaejaribu kutugawa watu wa Arusha haswa Wachagga na Wamasai. Ushindwe Mmeru ktk jina la Yesu.
Wameru ni Wamasai kwa asilimia 100. Sema wameasi toka zamani toka umasaini, ila they are Masai damu damu
 
Msikilizeni vizuri Makamba lakini.
CCM kweli kazi ipo. Chama kila siku kambi zinazidi kuongezeka.


Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kauli hii ya Makamba ni muendelezo wa kile kinachodaiwa kwamba Kambi ya Lowassa ya Urais inachanja mbuga kuelekea Ikulu hapo 2015.

Source; Radio Free Afrika tuzungumze Magazeti.

Anajua akisema hivyo hayo maneno yatamlipa ikitokea Lowassa yuko mjengoni.Kazi bado tunayo.Nini maana ya mtu wa watu? Ni aina ya rais aliyeainishwa kwenye mchakato wa katiba mpya au?Rais mtu wa watu: sifa hii inatosha kuwaletea maendeleo Watanzania maskini?
 
Mropokaji Makamba nae si mshauri mzuri, ni wa kupuuza tu!
 
Makamba ni miongoni mwa watu ambao walimrubuni Mkapa baada kupewa kitu kidogo kumchagua EL awe Waziri kipindi kile kwa hatushangai hiyo kauli na Mwendelezo tu wa sinema yao ya ufadhili wa ufisadi ndani ya ccm-Yaani hilo zee limeishi na Nyerere hata haoni aibu kuwapigia kampeni watu wasio waadilifu?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
Hili lizee linaloitwa yusufu makamba ni janga la taifa.kwanza ni lifisadi papa...linapenda sana kujipendekeza likiona mahali kuna ulaji.nakumbuka lilijipendekeza kwa kikwete kusudi mtoto wake January apewe uwaziri.hili zee halifai hata kidogo halina uzalendo na nchi.
 
CCM hamna ujanja, chagueni moja either EL awe mgombea wenu for 2015 au chama kife rasmi kama mkithubutu kukata jina kama mlivyozoea.
Umelipwa kiasi gani nami nijiunge kumpigia debe
 
Makamba anaamini EL akipata urais sasa....na yeye akiwa pembeni yake atakuja kumuachia JM!
 
Mkuu usiulize uadilifu kwa mwalimu mkuu wa shule msingi tuliyeambiwa aliachishwa kazi kwa kumrubuni mwanafunzi wake kimapenzi huko Tanga na hajawahi kukanusha

Hivi mtu kafukuzwa kazi ya Ualimu Mkuu halafu akaishia kuwa Mkuu wa mkoa wa Dar kwa miaka 12 na Katibu Mkuu wa CCM kwa miaka 8. Sasa hudhani kwamba ameidhihirisha kwa vitendo nadharia ya upiganaji. To me, thats my hero.
 
ntapiga kura kwa mara ya kwanza akigombea lowassa. ni mchapakazi na mtu wa watu wote kuhusu richmond epa cjui nn !! Only God Knwz.
 
Habari kama hizi zinaonyesha jinsi wengine walivyokosa imani nje ya ccm mpaka ndani kama lowassa naye atakuwa rais.
 
Hivi mtu kafukuzwa kazi ya Ualimu Mkuu halafu akaishia kuwa Mkuu wa mkoa wa Dar kwa miaka 12 na Katibu Mkuu wa CCM kwa miaka 8. Sasa hudhani kwamba ameidhihirisha kwa vitendo nadharia ya upiganaji. To me, thats my hero.

Unamaanisha kuwa Mkuu wa Mkoa anayeteuliwa na Rais ambaye amatokana na chama ambacho kina walakini katika Uadilifu?Unamanisha Katibu mkuu wa chama ambacho maadili yameshuka to zero?Anayeteuliwa na mwenyekiti wa chama kinacholinda haiba za Drug dealers?Chama ambacho kina Mwenyekiti ambaye ni Rais wa nchi anayehofia wezi wa EPA?Chama chenye serikali inayosimamia shughuli zake bungeni kupitia Waziri Mkuu anayetamani kuua wanaoua Albino badala ya kufuata sheria?Chama ambacho kimeunda serikali inayowapandisha vyeo makamanda wa vyombo vya dola waliohusika moja kwa moja(kwa mujibu wa ripoti) katika mauaji ya wananchi ?Kamuhanda forinstance!

Kama huyo ni Hero wako nadhani basi huna tofauti na huyo Mwalimu Mkuu aliyembaka mwanafunzi na kuwa promoted na chama na serikali hiyo hiyo iliyofilisika kimaadili
 
You very wrong big-headed moron,It's already known who will fly the Opposition flag.I simply feel sorry for CCM Party coz Lowassa is too strong to stop him from securing his Party's Presidential candidacy once that's done i guarantee you Malecela Junior CCM will lose it badly and in shame the election.

- Duh!! guaranteee Chadema will lose it badly hilo wala halina ubishi, maana hakuna mjadala wa Urais zaidi ya wagombea wa CCM, tumia akili kidogo tu nani Strong Candidate wa Upinzani saa hivi kwa nafasi ya Urais?

Le Mutuz
 
Kwa upande wangu Lowasa anawazidi mbali wanasemwa kuwa wanania ya kugombea kupitia CCM mwaka 2015.Jamaa ni mchapa kazi na anaweza kuchukua maamuzi magumu lakini sakata la RICHMOND limemtoa kwenye sifa.
 
Baada ya kuwa kimya kwa muda mrefu Yusuf Makamba katibu mkuu mstaafu wa CCM ameibuka na kudai kuwa Mbunge wa Monduli na Waziri mkuu wa zamani EDWARD LOWASSA ni mtu wa watu na anafaa kuwa kiongozi wa juu ktk serikali.

Kumbe EL alikuwa waziri mkuu tokea awamu ya 3 ya Ben? Nilikuwa sijui mkuu.
 
Makamba ni miongoni mwa watu ambao walimrubuni Mkapa baada kupewa kitu kidogo kumchagua EL awe Waziri kipindi kile kwa hatushangai hiyo kauli na Mwendelezo tu wa sinema yao ya ufadhili wa ufisadi ndani ya ccm-Yaani hilo zee limeishi na Nyerere hata haoni aibu kuwapigia kampeni watu wasio waadilifu?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Kumbe Lowassa alikuwa waziri mkuu tokea awamu ya 3 ya mzee wa Kiwira sio? Nilikua sijui mkuu.
 
Back
Top Bottom