Yussuf Manji, Omba Toba

Yussuf Manji, Omba Toba

Mawaidha mazuri lakini Manji alikwisha kuuza hicho kiwanja kwa Mtu mwingine ambae pamoja na bakwata walimshtaki sh. Ponda sijui kwanini Manji alaumiwe peke yake wakati wauzaji bakwata wameuza viwanja kwa watu wengi tu na zaidi ya hayo wamewashitaki mashehe waliowapinga lakini hawasomewi ahlul badr, kwanini ni Manji tu?
 
Duuh tatizo la yusuph ni ujeuri kwakuwa ana hela basi anawaona wengine wote maskini tu na hawana lolote la kumfanya
 
Ishara zipi zinazoonekana kwa macho ya binadamu zinaonesha mhusika ameomba toba kwa Allah, na Allah ametoa msamaha? Hiyo toba inafanyikaje?



Kama Allah ndio anajua zaidi kwa nini usimwachie jambo hili Allah?

Ndiyo kawachiwa Allah.

Toba haina kikomo.
 
Mawazo mazuri saana FF ila now it is a little too late. Weshamsomea ile kitu mbaya na sasa imeshaanza kutenda kazi. Nafuu ungekuwa upupu tungesema huo ni muwasho tu. Albadir ikishaanza kutenda kazi hakuna dua nyengine tena ya kumwokoa hapo.
Aksante kwa kutufahamisha kuwa kumbe Manji si Makonda kammaliza bali maovu yake alowafanyia hiana waislam. Poleni jamani ila, imani yetu inatufunza kuwa, hatuna hitaji la kupokea najisi. Iliibwa na viongozi ambao wengine weshatangulia mbele za haki. Mwache alilichumia janga lake, asitushirikishe kwani aliowanyima hiyo haki weshazoea kutokukumbuka. Na awe funzo kwa wale wapenda dhuluma. Aksante

Allah hachoki kusamehe. Dhambi zote anasamehe isipokuwa shirki tu.
 
Allah hachoki kusamehe. Dhambi zote anasamehe isipokuwa shirki tu.

Samahani FF,, nifumbulie hicho kitendawili. Dhambi ya shirki ni ipi ka sio hiyo unotaka Manji aturudishiye?? Alishaombwa na kuendewa na wenye haki wakamuonya dhidi ya hii dhulma, hadi imeamuliwa kumsomea dua. Sasa, acheni dua ifanye kazi yake kwani kibri dawa yake ndo hiyo. Hatutaki tena kuishiriki hiyo dhambi yake huyu bwana Manji. Aombe mwenyewe, Maulana akimsamehe na kumrejeshea awe funzo kwa wengi. Msidhani madhulumati yameisha, HAPANA. Yamejaa tele acha Mola ayafunze kwa dawa chungu
 
BAKWATA ni an organ within CCM,
Manji nae ni Mwanachama wa CCM,
So hii ni Biashara ya ndani kwa ndani,
Wote hawa (BAKWATA, CCM & Manji) hakuna anaeona kuna shida,
Ndio maana utawala uliopita chini ya Serikali ya CCM ulimtuhumu Issa Ponda kuleta uchochezi pale alipopinga huu unyang'anyi uliobatizwa jina la uuzwaji

Malizia basi, na waliomnyang'anya Oyster Bay? Na waliomtia ndani kwa tuhuma za madawa ya kulevya? Na ..., na...?
 
Mimi hapa nakubaliana na wewe 99%, ila hiyo 1% iliyobaki nakupinga.
Nakupinga kwa sababu huyu Sheikh Issa Ponda issa katika harakati zake za kuwatetea Waislam ikiwemo kupigania ule uwanja pale Chamg'ombe ameshawahi kusumbuliwa, kupigwa risasi, kuwekwa ndani, kuitwa gaidi na madhara mengineyo mengi tu na waliokua wakimfanyia hayo sio wengine bali Dola na utawala uliokuwepo awamu ya nne ambayo uliitetea sana.

Siajawahi kukuona ukipinga hili kwa kua tu ulikua na mahaba yako binafsi na utawala uliopita. Lei hii unakuja kukiri kua Manji aliwaonea waislam (utawala ulipita) lakini hukuwahi kuonyesha kukerwa na hili kipindi kile tuko utawala uliopita dada yangu. Anyway, kama sasa unakubali hilo basi Mwenyezi Mungu ni Mkubwa

Soma vizuri post namba moja.

Lini nilikubali Ponda kuadhibiwa? Lini nilikubali Manji kuuziwa viwanja vya Waislam?

Fikiri kabla hujakurupuka.
 
Pia tuwashauri na viongozi wa BAKWATA walioshiriki kufanya biashara na Manji kuomba toba.

Tena haraka sana. Kuna waliokufa midomo ikakataa kufunga. Si ishara njema.
 
Miji mingi duniani imeendelezwa na sekta binafsi..na kimsingi Manji alikuwa na mkataba na jiji alipokuja huyu Anayetaka matajiri waishi kama mashetani na gia yake eti maskini watakosa mahali la kuogelea ndo yakawa yaliyokuwa. Wakati ufukwe bado ungebaki free kwa kila mtu ila facilities nyingine ndo zingekuwa za kulipia.

Bakini na takataka yenu mnayoiita koko beach sijui ambayo ni kichaka cha wakabaji na wavuta bangi.

Hiyo ndiyo ukisikia irada ya mwenye kudhulumu. Hazidishiwi isipokuwa hasara.
 
Back
Top Bottom