Siku nyingine kama huna uhakika wa jambo ni vyema tu ukauchuna kuliko kukurupuka kwani utazidi kudharaulika. Kwa kukusaidia tu ni kwamba THINK TANKS wa Rais wako sasa ni wale wazee mahiri waliokuwa wasaidizi wa karibu wa Mwalimu Nyerere ( siwezi kuwataja majina kwa umuhimu na unyeti wao ) na wakisaidiana na Kiongozi wako mmoja mstaafu na baadhi ya watu aliokuwa nao. Hakuna mtu ambaye Rais wako haipiti siku lazima amjulie hali au hata aombe kuonana nae kama Mama Maria Nyerere na Rais wako anamuheshimu huyu Mama kama ambavyo anamuheshimu Mama yake na hata ushauri pia huomba kutoka kwake kisha unafanyiwa kazi na Wataalam. Kuna mengine ngoja niyamezee tu mate kwani yamekaa KIITIFAKI zaidi na jamaa karudi jana tu kutoka huku kwetu Kigali. Huyo Makongoro kuna kazi MAALUM na yeye atapewa na ukimya wake ni wa KIMKAKATI zaidi kutoka " eagle wing house ". Naomba niishie hapa niwahi zangu sasa kumshangilia Mwarabu leo taifa!