Yupo wapi "first lady"?

Yupo wapi "first lady"?

ni mama wa taifa kwa sasa kuna haja ya kumuulizia,lakini haina mantiki yoyote hata akionekana,hatukumuitaji yeye tulimuhitaji magufuli,haya ya wengine waliyoyafanya ni yaziada tu...
 
Wasukusu hawana tabia za kuwatanguliza wanawake, wao wana mfumo dume, si ni safi sana.
 
Kazi ya first lady ni kumwandalia JPM chakula cha nguvu baada ya kazi ngumu ya kutumbua majipu! Huoni kitengo cha mapishi kilikatwa kwa maana ya kubana matumizi sasa wewe unataka azunguke wapi, ikulu panamtosha kuzunguka na kumsubiria mmewe bana.
 
Ni kweli siku hazigandi. Katika awamu ya Tatu tulimwona Mama Anna Mkapa akizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa "Fursa sawa kwa wote".

Hakuchi Hakuchi mwisho hucha, Muda ulipofika Mama Anna Mkapa akaondoka na Mama Salma Kikwete akashika usukani. Yeye kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake alizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa WAMA. Lengo na nia ni kuwainua wanawake na kuchochea juhudi zao katika kujiletea maendeleo.

Awamu ya Tano imeingia kwa kishindo. Tofauti na awamu mbili za nyuma "First lady" wa awamu hii hajionyeshi kama ni mtu mwenye kupenda kuonekana. Hili lilijionyesha katika kampeni za uchaguzi lakini linadhidi kudhihirika kadri Muda unavyosonga.

Swali la kujiuliza "Yupo wapi First Lady"? Je, angali anajipanga kuona aifanyie nini jamii au atakuwa kimya kama wakati wa kampeni?

Mwache mtu amuudumie mumewe.unahoji hoji nini bana
 
siyo muuza sura kama unapenda wauza sura nenda Msoga na Monduli.
 
Kwa kweli mtoa mada kakosa adabu. Mke wa rais we wamrakia nn. Hii serikali sio ya show off ni ya kazi 2. Acheni cheap politics. Kila zama na maisha yake. Janet endelea kumlea rais wetu ili aiongoze tanzania vyema.
 
Unataka na yeye aanze kutembea na Ving'ora kama first lady wa zamani?
 
Yupo jikoni anamuandalia mumewe chakula ndio kazi inayomuhusu hizo nyingine wanadandia tu haziwahusu kwani hujui?
 
Hakuna jambo zuri kama kupata mziwanda ndani ya mjengo mweupe kama kumbukumbu ya uwepo wao pale.
Kwa hiyo msimuulize ulize aweza kuwa kwemye maandalizi na yanahitaji utulivu wa mwili na akili
 
Alisema kwa wasukuma wanawake siyo issue. Tehe!
 
Unataka arande arande mwishowe adhalilishwe kama fulani bureeeee....
 
Anasimamia kitengo cha mpishi Ikulu. Mambo ya WAMA na EOTF tuna Makamu wa Rais mwanamke hivyo ata deal na hayo kwa ukaribu zaidi.

Queen Esther

Ni kweli siku hazigandi. Katika awamu ya Tatu tulimwona Mama Anna Mkapa akizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa "Fursa sawa kwa wote".

Hakuchi Hakuchi mwisho hucha, Muda ulipofika Mama Anna Mkapa akaondoka na Mama Salma Kikwete akashika usukani. Yeye kama ilivyokuwa kwa mtangulizi wake alizunguka huku na kule kwa mwamvuli wa WAMA. Lengo na nia ni kuwainua wanawake na kuchochea juhudi zao katika kujiletea maendeleo.

Awamu ya Tano imeingia kwa kishindo. Tofauti na awamu mbili za nyuma "First lady" wa awamu hii hajionyeshi kama ni mtu mwenye kupenda kuonekana. Hili lilijionyesha katika kampeni za uchaguzi lakini linadhidi kudhihirika kadri Muda unavyosonga.

Swali la kujiuliza "Yupo wapi First Lady"? Je, angali anajipanga kuona aifanyie nini jamii au atakuwa kimya kama wakati wa kampeni?
 
Back
Top Bottom