Tatizo lako mwanahabari ni kwamba unakariri kila kitu unachokisikia. Aliyeko CCM ni mchafu aliyeko CHADEMA ni msafi, maisha halisi hayafanani na fikra zako. Wanasiasa ni wale wale tu, hawa wa CHADEMA ambao leo unawaona kama vile ni watakatifu, walikuwa wanasafiri pamoja na wale wa CCM, wanaenda nje ya nchi, wanakaa miezi wakiwa pamoja halafu wakirudi bungeni wanaanza kuziteka akili zako, na wewe bila ya kujiuliza kwa undani unadanganyika jumla jumla. Msigwa aligombana na Kasesela, lakini kesho yake wote wawili wanapiga picha wakiwa wamevalia masuti mazuri wakikumbatiana kama marafiki wa siku nyingi. Freeman Mbowe, Edward Lowassa, Fredrick Sumaye, John Magufuli na wengine wenye dhamana kubwa unaowajua wewe, ni marafiki wa karibu sana, hawana muda wa uhasama. Nakwambia yote haya ili uweze kukua kifikra, ili usidanganywe na siasa za majukwaani.