Phillipo Bukililo
JF-Expert Member
- Dec 29, 2015
- 18,473
- 13,624
Mwanasiasa anapoongea ipime kauli yake kwa undani la sivyo utadanganyika. Nimekwambia kuwa Lowassa alikuwa ni meneja wa kampeni wa Kikwete. Yale maneno "ajali ya kisiasa" yalikuwa ni maalum katika kumliwaza Lowassa ambaye alikuwa anapita katika kipindi kigumu kisaikolojia baada ya kulazimika kujiuzulu uwaziri mkuu. Kumbuka kuwa ni katika kipindi hicho ndipo Lowassa alisemwa kuwa alikuwa anakunywa sana whisky ili kujiliwaza. Ndugu yangu kauli ile ya KIkwete akiongea na wazee wa Dar ilikuwa na lengo la kisiasa zaidi, na ilisemwa kwa nia ya Kikwete kutaka kujisafisha machoni pa Lowassa na marafiki zake. Suala la nani atapelekwa kwenye mahakama ya mafisadi, na lini, hilo liko chini ya mamlaka ya taasisi zinazohusika.Wale ambao siyo wana CCM na waliokuwa misled na wana CCM hao hao waliligundua hilo na kusema;
lol....! kumbe tuliingizwa mkenge kwa fitina za kisiasa za wana CCM wenyewe kumbe ukweli wa mambo ni kinyume chake!!??
Na ndiyo maana leo wako pamoja na yeye kasemehe na maisha yanaendelea!!
How come tena wana CCM nyie mliokuwa mnaamini kuwa huyu jamaa "alipatwa na ajali ya kisiasa tu", leo mmeshupaza shingo zenu mki - shout kuwa huyu jamaa ni fisadi papa to the extent kwamba anaundiwa na mahakama yake kabisa and yet mtu huyu yuko mitaani tu anadunda tena akiwa ameshajitoa katika wigo wa kulindana miongoni mwao!!??
Mpaka hapo unaweza kuona kuwa sijaikwepa hoja yako, nimeijibu na nimerudia tena kuijibu hapa na ndiyo maana narudia kukuambia hujui kuwa kwa mujibu wa sheria za Tanzania ni makosa mtu kuhonga pesa watu au mtu flani kwa kusudi la kupata nafuu ya ulinzi flani?
Si ndiyo maana yako ya "aliwapa pesa ndefu" (ukimaanisha hongo au rushwa na nadhani ukimaanisha kule alikohamia sasa i.e CHADEMA), au
siyo mkuu?
Ndiyo tunasema, let him be the first to be taken to that special court on graft and corruption jumlisha na hawa waliopewa "hela ndefu" kama washtakiwa wenzake na mashahidi vilevile!!
I hope you ha've gotten the point now!
Hapa hatukuhumu, tunaongea mambo mbalimbali kwa kujenga hoja. Lowassa ni waziri mkuu mstaafu, Kikwete ni rais mstaafu, mimi na wewe tukiwa kama watanzania wa kawaida, kwanini tusitafute mada nyingine ya kuongea. Punguza kiburi, punguza jazba wakati unaongea na watu kupitia jamii forum. Humu kuna watu wa aina tofauti wenye elimu tofauti lakini wanaunganishwa na mada zinazojadiliwa.