Ulimbo
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 3,767
- 4,035
Hakujua kuwa Daladala halikuwa lake, yeye alikuwa abiria tu. Sasa alifika kituoni ikabidi ashuke na abiria mwingine akapanda.Kuna msemo usemao shetani hana rafiki!!
Leo nimekumbuka aliyekuwa msajili wa vyama vya siasa aliyepata kutikisa anga la siasa Za Tanzania kwa mbwembwe huku akionesha waziwazi kuibeba CCM!!
Tendwa alijawa kiburi, Jeuri na majivuno hasa!! Mara nyingi aliapa kukifutia usajili chama cha CHADEMA kiasi kwamba chama hicho kilitangaza kutoshirikiana nae!!
Nimejiuliza tu Leo yu wapi huyu mtangulizi wa Mutungi? Ya wapi matambo yake? Ki wapi kiburi chake? I wapi jeuri yake?
Anayejua alipo atujuze!!
Hii ni rejea kidogo ya siku Za nyuma