Yu wapi Dkt. Masumbuko Lamwai?

Yu wapi Dkt. Masumbuko Lamwai?

kweli mkuu.. na inaendelea kumtafuna mwenyekiti wetu kwa kumsaliti mke wake wa ndoa na kuzaa na mbunge wake wa viti maalum
Aseee ww unavurugu! Mbona unapenda kusema ukweli kwenye utani? Shaul yako wenzio hawapendi kuambiwa ukweli, ukiwaambia tu wanakuita msaliti!
 
Msomi huyu wa taaluma ya sheria, ambae aliwahi kuwa mwana siasa mahiri miaka ya 1995 yuko wapi? Anafanya shughuli gani? Naomba kujuzwa.
 
Yuko pale LUMUMBA anafagia,wakati mwingine anaonekana Dom nje ya makao makuu akiuza sare za chama chetu.
 
Dr Lamwai ni mwalimu pale Tumaini University kwa sasa.
 
Dr. Masumbuko Lamwai anaendelea na shughuli zake za Uwakili katika mahakama na mabaraza mbalimbali hapa nchini. Pia, Dr. Lamwai ni Mhadhiri Mwanadamizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Dar es Salaam. Yuko hasa hapa Dar es Salaam.
 
huyu msomi huwa ananishangaza,nywele hachani,havai viatu vya kufunika zaid ya sandals,hapigi pasi,mwilini yuko rough ila ubongo wake uko smart sana hata tundu lissu haoni ndani
 
Huyu bwana yupo ni wakili as makampuni mengi hapa mjini amekumbatiwa na yule bwana wa Forbes kwenye makampuni yake
 
na mimi niongeze neno .... anafundisha sheria chuo kikuu cha Tumaini kinachomilikiwa na kanisa la KILUTHERI (K.K.K.T.) DAR Campus. (mwenge njia ya kuelekea coca cola)
Anafundisha masomo ya CRIMINAL LAW & CIVIL PROCEDURE
Pia ni DEAN OF FACULTY (LAW)
 
Mulizeni mdogo wake mbunge wa rombo, mh Roman Selasini.
Rip Roman selasin alikuwa ni baba ake dr lamwai mdogo wake anaitwa joseph selasin ambaye ndo mbunge wa wa sasa wa rombo kupitia Ukawa
 
Dr. Masumbuko Lamwai anaendelea na shughuli zake za Uwakili katika mahakama na mabaraza mbalimbali hapa nchini. Pia, Dr. Lamwai ni Mhadhiri Mwanadamizi wa Chuo Kikuu cha Tumaini cha Dar es Salaam. Yuko hasa hapa Dar es Salaam.
Mara ya mwisho nilimuona mahakamani amevaa koti kubwa jeusi akitetea wezi wa kuku.

Ccm wabaya sana. Sasa kama walikuja kumkumbuka hapo sijui!
 
huyu msomi huwa ananishangaza,nywele hachani,havai viatu vya kufunika zaid ya sandals,hapigi pasi,mwilini yuko rough ila ubongo wake uko smart sana hata tundu lissu haoni ndani
Anamkaa na mtungini daily hiyo ndy shidaa,nyumbani kwake alikuwa na grocery basi kutwa kupiga chichaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom