You are not my type

You are not my type

Majibu kama haya yanatolewa na wale wanaojudge kile wanachokiona leo. Hawajui kuwa kuna kesho, kwamba maisha hubadilika.


Huyo anayemuona ni type yako leo, mambo yakigeuka kesho utamkana. Wakati yule unayemuona si type yako kwa sasa, wakati huo wewe ndo utakuwa siyo type yake.


Let's Be Wise (especially ladies).
Kwa jinsi comment yako ulivyoiweka, naona umebase kwenye uchumi na privileges zingine lakini hiyo sio type bali ni hadhi
 
Aigoooo sunbaenim leo umekuja huku? Karibu, vuta kiti ukae
ahsante sana,

you are not my type
muonekano wako pamoja na haiba yako haijanivutia haijalishi ni mrembo kama miss tanzania 2006 japokuwa wengine wanakuona ni zaidi ya malaika na wanatamani kuwa nawewe muda wote mpaka kifo kiwatenganishe.

you are not my type
unavutia kimaumbile lakini mfumo wako mzima wa maisha haunivutii,eg unapenda starehe, unapenda umaarufu.

you are not my type
upo tofauti kabisa na msichana ninayemtafuta ili tuanzishe mahusiano, mfano labda hajafikia umri fulani.

kwa mtazamo wangu kwa mazingira ya kwetu ni maneno ambayo unapaswa ujisemee zaidi nafsini mwako kwa dhumuni la kumuelezea mtu fulani pindi unapotaka kufanya maamuzi
nadhani ni maneno mepesi zaidi kuliko you're not attractive.
 
ahsante sana,

you are not my type
muonekano wako pamoja na haiba yako haijanivutia haijalishi ni mrembo kama miss tanzania 2006 japokuwa wengine wanakuona ni zaidi ya malaika na wanatamani kuwa nawewe muda wote mpaka kifo kiwatenganishe.

you are not my type
unavutia kimaumbile lakini mfumo wako mzima wa maisha haunivutii,eg unapenda starehe, unapenda umaarufu.

you are not my type
upo tofauti kabisa na msichana ninayemtafuta ili tuanzishe mahusiano, mfano labda hajafikia umri fulani.

kwa mtazamo wangu kwa mazingira ya kwetu ni maneno ambayo unapaswa ujisemee zaidi nafsini mwako kwa dhumuni la kumuelezea mtu fulani pindi unapotaka kufanya maamuzi
nadhani ni maneno mepesi zaidi kuliko you're not attractive.
Ahsante sana sunbae wewe unafikiria kama mimi, sio upande huo tu. Unaweza usiwe my type kwa kuwa wewe muda wako wote unatumia kujisomea na kuabudu wakati mimi nataka mtu ambaye weekend nitaenda nae club, tucheze muziki, tunywe tufurahi na marafiki. Unaweza kuwa na kila kitu ila usinivutie kwa vile unacheka kama Jang Hyuk
 
Kwa hiyo hii mada hapa mliimalizaje?

Hitimisho......
Ahsante sana sunbae wewe unafikiria kama mimi, sio upande huo tu. Unaweza usiwe my type kwa kuwa wewe muda wako wote unatumia kujisomea na kuabudu wakati mimi nataka mtu ambaye weekend nitaenda nae club, tucheze muziki, tunywe tufurahi na marafiki. Unaweza kuwa na kila kitu ila usinivutie kwa vile unacheka kama Jang Hyuk
 
Hayo ni majibu ya kisichana,mwanamke hawezi kujibu hivyo;kuna mmoja alishawahi kunijibu hivyo,nadhani kwa sasa atakuwa anajilaumu.
 
huku anakupandisha na kukushusha + kubinua midomo
Hawa ni wale wasichana ambao bado wananukia maziwa ya mama na hawajajua maisha ndio wanapenda kutumia sana hiyo misemo,maisha yakiwachapa ndio wanapata akili nzuri,ni ngumu sana kwa mwanamke anayejitegemea kukujibu hivyo.
 
Ayo majibu ya dharau wanayapenda sana wanawake ambao ni wajinga au ni ma-teenager, maisha sio mapenz kuna mambo mengi, unamwambia sio type yangu MTU anayekaa na vinyongo kesho unahitaj msaada wa dharura tofaut kabisa na mahusiano kutoka kwake hakusaidii

Hata mzazi mtoto anapomuomba kitu na hataki kumpa au hana Mara nyingi hutumia busara, hata unapomkatalia MTU ustarabu ni kitu cha muhimu sana
 
Ayo majibu ya dharau wanayapenda sana wanawake ambao ni wajinga au ni ma-teenager, maisha sio mapenz kuna mambo mengi, unamwambia sio type yangu MTU anayekaa na vinyongo kesho unahitaj msaada wa dharura tofaut kabisa na mahusiano kutoka kwake hakusaidii

Hata mzazi mtoto anapomuomba kitu na hataki kumpa au hana Mara nyingi hutumia busara, hata unapomkatalia MTU ustarabu ni kitu cha muhimu sana
Ndugu yangu inategemea na huyo mtongozaji amekujaje kuna wanaume wengine hawajui kutongoza kistaarabu wanatumia kauli za kihuni sasa watu kama wao wanategemea uwajibuje mfano mzuri mimi mwenyewe nimeshatongozwa na wanaume kama hao lakini nitamtolea mfano huyu mmoja maana ndo aliyenikera kuliko wote

Tulikutana wakati tupo chuo tulikuwa tunasoma darasa moja ila tulikuwa hatuna mazoea kabisa ni ile tu kupishana na kusalimiana tu halafu nilikuwaga namuona ni mstaarabu nashangaa siku moja eti akaniambia "dada mimi nimekuelewa sana kama vipi twende kwangu basi unipe huo mzigo tu halafu baada ya hapo kila mtu aendelee na mishe zake" kamaliza hapo

Yaani nilimuangalia kwanza sikummaliza halafu bora hata angenikuta sehemu nimejipanga najiuza yaani yalikuwa ni mazingira ya chuo kabisa ila anaongea kauli kama hizo nilijikuta nimemchukia ghafla

Maana nilihisi labda sijui kanionaje yaani sijui kaniona mimi malaya sana hata hivyo sikutaka kumjibu vibaya nikamuacha sasa ndo ujiulize wanaume kama hao nao ukiwajibu vibaya utakuwa umekosea kweli? Mimi nadhani wanawake wengi huwa wanajibu kutokana na namna walivyotongozwa
 
Huyo nae hakuwa anakutongoza.

Naona alikuwa anataka kukununua. Tena ungemtemea na mate kabisa. Ulimwachaje hivi hivi mtu asiye na adabu.
Ndugu yangu inategemea na huyo mtongozaji amekujaje kuna wanaume wengine hawajui kutongoza kistaarabu wanatumia kauli za kihuni sasa watu kama wao wanategemea uwajibuje mfano mzuri mimi mwenyewe nimeshatongozwa na wanaume kama hao lakini nitamtolea mfano huyu mmoja maana ndo aliyenikera kuliko wote

Tulikutana wakati tupo chuo tulikuwa tunasoma darasa moja ila tulikuwa hatuna mazoea kabisa ni ile tu kupishana na kusalimiana tu halafu nilikuwaga namuona ni mstaarabu nashangaa siku moja eti akaniambia "dada mimi nimekuelewa sana kama vipi twende kwangu basi unipe huo mzigo tu halafu baada ya hapo kila mtu aendelee na mishe zake" kamaliza hapo

Yaani nilimuangalia kwanza sikummaliza halafu bora hata angenikuta sehemu nimejipanga najiuza yaani yalikuwa ni mazingira ya chuo kabisa ila anaongea kauli kama hizo nilijikuta nimemchukia ghafla

Maana nilihisi labda sijui kanionaje yaani sijui kaniona mimi malaya sana hata hivyo sikutaka kumjibu vibaya nikamuacha sasa ndo ujiulize wanaume kama hao nao ukiwajibu vibaya utakuwa umekosea kweli? Mimi nadhani wanawake wengi huwa wanajibu kutokana na namna walivyotongozwa
 
Ni Dharau
Yeye Kashakuona wewe ndio wa type yake.
Alafu wewe unajishaua
Tafuta jibu lingine la kumpa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom