Yesu sio Mungu

Yesu sio Mungu

Ngoja nimwelimishe mtoa mada:
Mungu sio mwanadamu yaani sio mtu:
Hili swala ndio shetani anapo simama na kuwadangaya watu:
Yesu ni binadamu kama anavyo ona mtoa mada:

Hapo kale Mungu aliamua kushuka duniani ili aonge na watu wake:
Sasa anashukaje, maana akija kama alivyo dunia haiwezi kuhimili kishindo chake:

Mungu ni Roho Takatifu na sio mwili, Mungu hana mwili kama huu wetu:
Kwakuwa ni chanzo cha uhai tunamwita Roho Mtakatifu badala ya Roho Takatifu:

Yohana (Joh) 4:24
Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli.

Hivyo basi mtu wa kawaida akimwona Yesu anajua kabisa ni mtu:

Kutokana ba Biblia takatifu achaneni na Satanic Verses, Mungu mara nyingi tu alishuka duniani kwa umbo la mtu:

Aliwahi kushuka na kuongena na Ibrahimu kama mtu akiwa na Malaika wawili:

Mwanzo 18:1
Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.
2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,
3 akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako.
4 Na yaletwe basi maji kidogo mkanawe miguu, mkapumzike chini ya mti huu.
5 Nami nitaleta chakula kidogo, mkaburudishe moyo, baadaye mwendelee, iwapo mmemjia mtumwa wenu. Wakasema, Haya, fanya kama ulivyosema.
6 Basi Ibrahimu akaenda hima hemani kwa Sara, akasema, Himiza vipimo vitatu vya unga safi, uukande, ufanye mikate.
7 Ibrahimu akapiga mbio kwenda kundini, akaleta ndama wa ng'ombe aliye laini, mzuri, akampa mtumishi, naye akahimiza kuiandaa.
........
Yesu alizaliwa kwa mpango wa Mungu ili ashuke katika mwili wake na aongee na watu wake:
Wengi watashangaa hii hoja lakini hawashangai Jini au Mzimu kuingia katika mwili wa mtu na kuongea mambo wanayopenda:
Jini anaweza ila Mungu hawezi wanavyo fikiri:

Soma hapa:
Luka 4:18
Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,
28 Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo.
(Wayahudi walikasirika kwakuwa waliona amekufuru kwa hilo andiko)
.....
Baada ya kubatizwa na Yohana Mungu alishuka katika umbo la Yesu kwa mfano wa ndege Hua yaani Njiwa:
Toka siku ile Yesu akaanza kuhubiri injiri, kufufua wafu kuponya wagonjwa nk.

Tunaposema Yesu ni Mungu tunauangalia ule muda mchache ambao Mungu alishuka katika mwili wa Yesu:

Hili jambo hata baadhi ya ndugu zake Wayahudi hawakulijua

Yohana 10:30
Mimi na Baba tu umoja.
31 Basi Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige.
32 Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?
33 Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.
......
Ndio maana kuna wakati Yesu anaonge kama mtu:
"Naona Kiu"

Na kuna wakati anaongea kama Mungu Mwenyezi:

Mathayo 9:2
Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza,
👉Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
Hivyo ndivyo ilivyo:
Anayesema Yesu ni Binadamu ni sawa: mwana wa Adam:
Ila katika Lugha ya Kinabii kutokana na Biblia huyu ndiye Yesu na alizaliwa kwa kusudi hili tu:

Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto mwanamume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;
Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa ajabu,
Mungu mwenye nguvu,
Baba wa milele,
Mfalme wa amani.
..........
Puuzeni maneno ya Satanic Verses, hizi za juzijuzi tu:
Manabii wa Mungu walishaongea na it is the FINAL:
Hiyo MUNGU alitaka kuja Duniani aongee na watu wake umeitoa wapi?
 
Nani aliye fufuka mwenyewe na aliyesema atafufuka kwa muda flani baads ya kifo chake ili isiwe bahati au uzushi wake ?
Yesu kufa na kufufuka ilikua inajulika na aliwaambia wanafunzi wake sio jambo la bahati mbaya, pili wapo wengi waliofufuka Eliya na Elisha walifufua pia wafu, Kwauwezo wa MUNGU hakuna linaloshindikana hvo hoja yako ya kufa na kufufuka sio kigezo cha kusema Yesu ni MUNGU
 
Nasema hivi mtu akija na hoja yeye mashiko kuwa Yesu ni mungu nampa laki 1 niliiweka kwenye kibubu kwa zaidi ya miezi mitatu, ntakupa akiba yangu yote.

Uje umekula mambo ya matusi, sijui roho mtakatifu usiyalete hapa leta hoja nzito

Arianism
Arianism ni nini?
 
Yesu kufa na kufufuka ilikua inajulika na aliwaambia wanafunzi wake sio jambo la bahati mbaya, pili wapo wengi waliofufuka Eliya na Elisha walifufua pia wafu, Kwauwezo wa MUNGU hakuna linaloshindikana hvo hoja yako ya kufa na kufufuka sio kigezo cha kusema Yesu ni MUNGU
Kwanini unazani yesu sio mungu ili tuanze kujadili kwenye upande huo ? unajua mimi bado najifunza kama umegundua kitu kipya kiseme hapa
 
Nasema hivi mtu akija na hoja yeye mashiko kuwa Yesu ni mungu nampa laki 1 niliiweka kwenye kibubu kwa zaidi ya miezi mitatu, ntakupa akiba yangu yote.

Uje umekula mambo ya matusi, sijui roho mtakatifu usiyalete hapa leta hoja nzito

Arianism
Uzuri huko mbinguni kila mtu atawajibika peke yake. Wanaoamini acha waamini na wewe usiyeamini baki na imani yako hiyo hiyo.
 
Mitume hawakuwa makamanda wa jeshi lolote au hawakuwa wapiganaji au mafunzo ya upanga wengi walikuwa wavuvi na watu wa kawaida nani alikuwa mpiganaji kwenye mitume ?
Mitume Gani kwanza unaowaongelea wa Yesu au wa MUNGU kama Mussa, Daudi, Yoshua,Suleiman, Ibrahim wote walipgana vita
 
Musa na daudi na youshua hawakuwa mitume bali manabii

niambie nini maana ya nabii

na nini maana ya mitume
Sikilza ww Mimi sio mjinga Kwa wakristo mitume niwale wanafunzi wa Yesu na wanaosambaza injili hili nalijua

Kwa mantiki hiyo basi usingesema mtume Muhammad angesema nabii Muhammad Toka ulivoanza maana Muhammad hakua mwanafunz wa Yesu wala msambaza habari za Yesu
 
Sikilza ww Mimi sio mjinga Kwa wakristo mitume niwale wanafunzi wa Yesu na wanaosambaza injili hili nalijua

Kwa mantiki hiyo basi usingesema mtume Muhammad angesema nabii Muhammad Toka ulivoanza maana Muhammad hakua mwanafunz wa Yesu wala msambaza habari za Yesu
Nini maana ya mitume

na nini maana ya nabii

msaada tafadhali hebu tuongee kama marafiki tu
 
Wewe unaamini yesu ni mungu lakini bado umepungukiwa unachanganya roho mtakatifu na mungu baba bado hujui muundo huu utakuwa vipi, kwahiyo hoja yako wewe hapa nikumtambua yesu kama mungu huko pengine unapotosha
Mimi naongea kwa maandiko na Aya:
Sitaki waropokaji kuni nukuu na kuongea pumba zao:
Siku nyingine ukitaka kuongea na mimi ongea kwa Aya
 
Mtoa mada ili kupata majibu ya swali lako inabidi tujiulize haya maswali matatu
1. Yesu Kabla Hajaja Duniani: Alikuwa nani?
2. Yesu Akiwa Duniani: Alikuwa Nani? na Alikuwa na Uwezo Gani?
3. Baada ya Yesu kufa na kufufuka alienda wapi
4. utofauti wa yesu na Wanadamu Wengine na viumbe wengine.

Twende sasa

1. Yesu Kabla Hajaja Duniani: Alikuwa nani?
Kabla ya kuja duniani, Yesu alikuwa Neno wa Mungu, ambaye alikuwa na Mungu na alikuwa Mungu mwenyewe. Hili linathibitishwa na Yohana 1:1, “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwa kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.” Yesu hakuanza kuwepo alipofanyika mwili, bali aliishi milele akiwa na Baba. Katika Wakolosai 1:16 tunafundishwa kuwa kwa yeye vitu vyote viliumbwa, vya mbinguni na vya duniani – hii inaonyesha kuwa Yesu ni Muumba na si kiumbe. Kwa hiyo, kabla ya kuzaliwa duniani, Yesu alikuwa na uungu kamili, mamlaka ya kiungu, na alishiriki utukufu na Baba tangu milele (Yohana 17:5).

2. Yesu Akiwa Duniani: Alikuwa Nani? na Alikuwa na Uwezo Gani?
Yesu alipokuja duniani, alichukua mwili wa kibinadamu lakini hakuwacha uungu wake. Alikuwa na asili mbili kwa pamoja: Mungu na mwanadamu. Wafilipi 2:5–8 inaeleza kuwa, ingawa alikuwa sawa na Mungu, alijinyenyekeza akajifanya kuwa mtumishi na akawa kama wanadamu. Akiwa duniani, Yesu alionyesha uwezo wa kiungu: alisamehe dhambi (Marko 2:5), alijua mawazo ya watu (Mathayo 9:4), alituliza dhoruba kwa neno moja (Mathayo 8:26), na alifufua wafu kama Lazaro (Yohana 11). Mambo haya hayawezi kufanywa na mwanadamu wa kawaida; ni sifa za Mungu pekee. Hii inathibitisha kuwa hata akiwa duniani, Yesu alikuwa Mungu kwa uwezo na mamlaka.

3. Baada ya Yesu kufa na kufufuka alienda wapi
Baada ya Yesu kufa msalabani na kufufuka, hakurudi tu mbinguni bali alirudia utukufu wake wa awali akiwa sasa na mwili wa utukufu. Wafilipi 2:9–11 inasema kuwa Mungu alimwadhimisha sana na kumpa jina lipitalo kila jina, na kwamba kila goti lipigwe na kila ulimi ukiri kuwa Yesu ni Bwana. Hii inaonyesha kuwa Yesu alirudi katika hali yake ya Uungu wa milele akiwa na mamlaka juu ya kila kitu. Biblia pia inamwonyesha Yesu kama anayeketi katika mkono wa kuume wa Mungu (Waebrania 1:3), akifanya kazi kama Kuhani Mkuu na Mwombezi wetu mbinguni.

4. utofauti wa yesu na Wanadamu Wengine na viumbe wengine.
Yesu Kristo ni wa kipekee kabisa kati ya wanadamu wote waliowahi kuishi. Tofauti kuu ni kwamba Yesu hakuwa na dhambi hata siku moja. Watu wote wanakosea, lakini Biblia inasema wazi kwamba Yesu hakutenda dhambi wala hakuwa na hila yoyote (1 Petro 2:22). Hii inamfanya Yesu awe mtakatifu kabisa, tofauti na wanadamu wengine ambao wanahitaji wokovu na msamaha wa dhambi.

Zaidi ya hayo, Yesu si tu mwana wa Mungu kwa njia ya imani, bali ni Mwana wa Mungu kwa asili ya milele. Hii inamaanisha Yesu hakuzaliwa tu kama binadamu, bali alikuwa na asili ya kiungu tangu milele (Yohana 3:16). Wanadamu wote ni watoto wa Mungu kwa imani, lakini Yesu ni wa pekee katika hii hali, akiwa na uhusiano wa kipekee na Baba yake mbinguni.

Tofauti nyingine kubwa ni kwamba Yesu si kiumbe kama malaika au mwanadamu wa kawaida, bali ni Muumba wa vitu vyote vilivyo mbinguni na duniani. Biblia inasema kwa Yesu vitu vyote viliumbwa, ikiwa ni viti vya enzi, mamlaka, na viumbe vyote (Wakolosai 1:16-17). Hii inaonyesha kuwa Yesu ni chanzo cha maisha na nguvu zote, tofauti kabisa na viumbe aliyeumba.

Pia, Yesu ana mamlaka ya kiungu ambayo hakuna mwanadamu au kiumbe mwingine anayeweza kuipata. Alisamehe dhambi, jambo ambalo ni haki ya Mungu peke yake (Marko 2:5-7), alipokea ibada kutoka kwa wafuasi wake (Mathayo 14:33), na alishinda mauti kwa kufufuka kwake, akawa hai milele (Ufunuo 1:18). Kwa hivyo, Yesu ni wa kipekee katika kila upande — mtakatifu, Mwana wa Mungu, Muumba wa viumbe vyote, na Mwenye mamlaka ya milele.

Asante
 
Back
Top Bottom