MUNGU sio jina ni cheo ie. Muumbaji. Kitabu cha Kutoka wakati Mungu anaongea na Musa kwenda kwa farao Mungu alimwambia Musa
Kutoka 3
13. Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
14. Mungu akamwambia Musa, MIMI NIKO AMBAYE NIKO;<br> akasema, Ndivyo utakavyowaambia wana wa Israeli; MIMI NIKO<br> amenituma kwenu.
Kwa hoja hii neno Mungu sio jina bali ni cheo ambacho hata miungu ya Misri ilikuwa nayo Musa anataka jina la Mungu na Mungu anajifunua jina lake kuwa hapo kama "NIKO AMBAYE NIKO".
Yohana 8
54. Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu.
55. Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika.
56. Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
57. Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58. Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Kumbe wayahudi walimwita Mungu wasiyemjua Yesu anawaambia yeye anamjua hivyo wamuulize atawaambia kuhusu huyo Mungu. Ni mfano na umeenda ofisini ile uko nje unamuulizia boss wa ofisi na uliyemkuta nje ndio yeye Ila hajajifunua maana hayuko na hujamkuta ofisini akaanza kukuuliza una shida gani wewe unang'anana kutaka kuongea na boss huku unatoa maneno ya kashfa anakuambia ukiniona Mimi umemuona boss wewe unang'ang'ana kutaka kumwona boss kumbe ni yeye Ila anaku enjoy tu Mara anakufukuza kisha anakuja mtu kukutonya kuwa huyo ndio boss sijui utafanyaje maana ulidhani boss at a kuwa kwenye suit Kali, kiatu kikali, yuko ofisini wakati wote, hachangamani na kuwa na ukaribu na watu n.k
Wafilipi 2
5. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
6. ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
7. bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
8. tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
9. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
10. ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
11. na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Anaposema kwa hiyo Mungu akamkilimia jina inamaanisha Mungu (ofisi) ikamkamkilimia. Mungu ni ofisi tu na sio kitu chochote mnachofikilia
Yohana 1
18. Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.
Sasa wewe uliyemuona Mungu said Yesu mfunue hapa huyo mungu tumuone.
Kibinafsi nasema Yesu ni Mungu kwa sababu anajua alipitia magumu yote katika mwili akashinda hivyo anajua udhaifu wangu vizuri. Sasa huyo Mungu wako asiyejua njaa, majaribu ya wanawake, ukata n. K simtaki maana ni mungu mjinga na muoga asiyejua hustle tunazopitia wanadamu yeye akae huko alike Sisi tunabanana na Mungu na Bwana wetu Yesu Kristo mfufuka mpaka atufukishe mbinguni. Amen.