Yesu ni jibu

Status
Not open for further replies.

Kibun'ga

New Member
Aug 26, 2011
2
5
Yule Sheikh Mtoto maarufu kama Sheikh Shariff ambaye aliitingisha Tanzania kwa ufahamu mkubwa wa Qur’an akiwa na umri wa miaka tisa hatimaye amesalimu amri na kuokoka, katika kanisa la Pentekoste Motomoto jijini Dar es Salaam .
Sheikh Shariff ambaye jina lake halisi ni Sheikh Shariff Mohamed Mikidadi tayari amebatizwa na kupewa jina jipya la Michael Sylivester Sewando, ambapo hivi sasa analelewa kiroho katika kanisa hilo lililopo Keko chang’ombe jijini Dar es Salaam .
….Licha ya Sheikh Shariff sasa Michael Sewando kuzaliwa katika familia ya kikatoliki ya mzee Sylivester Sewando na mama yake Joyce Mokiwa, alisema alisilimu baada ya kutibiwa maradhi yake na mganga muumini wa dini ya Kiislamu wakati akiwa mtoto.Katika umri mdogo, jambo hilo lilimfanya ghafla ajikute akianza kuipenda dini ya kiislamu na ndipo aliamua kujiunga nayo, ingawaje wazazi wake walimpinga vikali.Alisema ilibidi aondoke Nyumbani kwao Kawe Ukwamani na kuhamia kwa ndugu wa kiislamu na kuanza kuswali katika msikiti wa Al Shariff, International Dawas’ Islamic Centre Kawe Dar es Salaam. (SIDC) alikoingizwa rasmi katika dini ya Kiislamu.Alisema mara baada ya kujiunga na dini hiyo na kuanza kuswali katika msikiti huo, alijikuta akipata ufahamu mkubwa wa elimu ya Qu’ran pasipo kufundishwa. Sheikh Shariff alisema anachojua ni kwamba uwezo wa kuijua Qur’an aliupata kutoka kwa majini 2900, yaliyomuingia baada ya kujiunga na Uislamu.Alisema majini hayo ndiyo sababu pekee iliyomfanya awe mahiri sana katika elimu ya dini ya kiislamu. Akizungumza na wahadhiri mbalimbali nje na ndani ya Tanzania huku akifanya miujiza na kuendesha mihadhara mingi ya kiislam.Kwa mujibu wa Sheikh huyo aliyeokoka, maeneo aliyowahi kutoa mihadhara ni Kawe,Tandika , Mbagala, Njoro, Kilimanjaro, Mwembe tayari nchini Kenya , viwanja vya msikiti Mkuu wa Jijini na Kampala nchini Uganda .Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Sheikh Shariff alisema aliwahi kuishi chini ya bahari ya Hindi katika eneo la Maskati, nchini Oman , akifundishwa mambo mbalimbali na majini. Alisema akiwa chini ya bahari alikuwa akifundishwa na jini mkuu aliyemtaja kwa jina Lusifa ambalo ni la Shetani, ambapo alikuwa akilishwa mchanganyiko wa damu za binadamu na wanyama na mifupa ya farasi.Sheikh Shariff au Michael Sewando alisema Lusifa au mkuu wa majini ambaye alikuwa na umbo la mfano wa mjusi mkubwa, ndiye aliyemfundisha masuala ya uganga wa kienyeji kwa kutumia vitabu maarufu vya kijini. Mambo mengine aliyofanyiwa akiwa chini ya bahari ni pamoja na kuwekwa katika moto mkali kwa muda wa siku saba na baadaye katika baridi kali na giza totoro kwa siku hizo hizo.Nakumbuka nikiwa chini ya bahari ambako naamini ni kuzimu, Lusifa aliamuru kuwa kamwe nisilitaje jina la mtu aliyesulubiwa msalabani kwa maana yaYesu, kwa vile jina hilo ni baya na huharibu kazi za kuzimu. Pamoja na mambo mengine mengi ya ajabu aliyofanyiwa au kufundishwa na Lusifa, alisema baadaye alihitimu na kupatiwa mikoba mitatu iliyosheheni madawa ya mitishamba, viungo vya wanyama, binadamu na majoka. Unajua nilikuwa nafanya masuala ya kuagua watu kiganga huku pia nikiendesha mihadhara mbalimbali ya kiislamu’’ alisema akionyesha kitambulisho kinachoonyesha kuwa ni mganga wa kienyeji.Alisema katika shughuli zake aliwahi kuwasilimisha wakristo mbalimbali wakiwepo mapadri na wachungaji, ambapo ameahidi kuwarudisha kwa Yesu baada ya kuokoka. Aidha alibainisha kuwa aliwahi kuoa majini mawili na kusababisha ajali zilizopoteza maisha ya watu ili kupata damu na nyama za majini aliyokuwa akiyamiliki.Kuhusu jinsi alivyokutana na Yesu na kuokoka, alisema hivi karibuni wakati akielekea katika shughuli zake za uganga eneo la Mbagala Mgeni Nani, miguu yake ghafla ilinasa ardhini na akasikia sauti ya Yesu ikimwambia kwamba aachane na uchafu wake, ili atakaswe kwa damu yake Yesu lakini alitaka kupinga.Alisema akiwa katika hali ya kupinga sauti hiyo, alitokea mama mmoja aliyekuwa muislam lakini akaokoka, ambaye alimshauri aokoke na kumuongoza zaidi hadi katika kanisa la Pentekoste Motomoto lililoko Keko Chang’ombe alikomkiri Yesu na kuokoka baada ya kutolewa mapepo. Kanisa la Pentekoste Motomoto linaongozwa na Mchungaji Ibrahimu John ambaye kwa sasa ndiye baba wa kiroho wa Sheikh Shariff.Sheikh Shariff (Michael Sewando) alisema baada ya kuokoka, amekuwa akipata mashambulizi kutoka kwa majini na wachawi hivyo anaomba msaada wa maombi kutoka kwa wacha Mungu wote.SOURCE: MSEMA KWELI
 
Hillola kujaga kuokoka 2likuwa tunalisubiria tu kwa hakika Wakirsto wengi walikuwa wakimwombea sana huyu dogo kwa jinsi alivyo kuwa anawapotosha watu wa MUNGU na hakika neno hili litabakia kuwa ya kweli: KWA BWANA YESU KILA GOTI LITAPIGWA na bado wengi wataokoka tu.
 
sheikh sharif,babu wa loliondo,kondoo wa quran,josee chamilion nk
bado tutaona mengi tu.
my take.hizi ni siku za mwisho.
 
Sijabadili dini


SHEIKH Shariff Mikidadi Matongo, amekanusha taarifa iliyotolewa na chombo cha habari kinachomilikiwa na dhehebu moja la dini ya Kikristo kuwa ameokoka na kuacha dini yake ya Kiislamu.

Akizungumza na waandishi habari kwenye Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo), Msemaji wa sheikh huyo, Ally Mohamed, alisema taarifa hiyo inataka kuwabadilisha Waislamu kutoka kwenye imani yao licha ya sheikh huyo kuanza kazi yake akiwa na umri wa miezi tisa akitangza Uislamu .
Alisema taarifa hiyo iliandikwa na kuambatanishwa na picha ya sheikh huyo na nyuma yake kuwa na mchungaji wa dini hiyo ya kilokole akiwa anambatiza, jambo ambalo anasema hakulifanya.
Aliendelea kusema kama yeye alibatizwa katika dini hiyo wathibitishe na tukio hilo lilifanyikia wapi na huyo mchungaji aliyempa upako huo.
Aidha, alisema gazeti hakuweza kulitja kutokana na imani aliyonayo sheikh huyo kwa kutofanya maamuzi ya haraka ya kuwachukulia hatua za kisheria wamiliki wa chombo hicho.
Mohamed alisema taratibu zinafuatwa za kukaa chini na mmiliki wa gazeti hilo kuthibitisha kwake kuwa aliokoka, vinginevyo aombe radhi ili kurudisha imani ya Waislamu dhidi ya sheikh huyo.
"Sisi Waislamu pamoja na dini za Kikristo tunaheshimiana, kutokana na hili tukae chini tuombane radhi ili tusiweze kuvuruga imani yetu na hasa huwa tunashirikiana vizuri sana katika shughuli za kiimani, kwa hili tumefika pabaya," alisema Sheikh Mohamed.
Alisema taarifa hizo zilimfikia Sheikh Matongo akiwa nchini Comoro, alipokuwa ameitwa na Rais wa nchi hiyo, Abdallah Sambi, kwa ajili ya masuala mbalimbali yakiwamo ya dini ya Kiislamu.
Sheikh huyo alisema kutokana na taarifa hiyo, imemsababishia kuulizwa maswali na watu wengi, jambo ambalo linamsababishia mkanganyiko usiokuwa na maana.
Naye Sheikh Shariff Mikidad Matongo alisema ana hamu ya kukutana na Watanzania ili kufanya nao mihadhara ya kidini kutokana na muda mrefu kuwa nje ya nchi.
Alisema hivi sasa anajiandaa kwa safari katika nchi za Ufaransa, Sudan na visiwa vya Reunion kwa mialiko ya wakuu wa nchi hizo.

sorce tanzania DAIMA!!! http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=9159

SASA TUAMINI GAZETI GANI MSEMA KWELI AU TANZANIA DAIMA...????!

may take Mods hii thread haina tofauti na ule uzsshi wa shimbo! ificheni mpaka mpate uhakika! ili kijana wa watu aije akapata usumbufu usiokuwa wa lazima
 
Yule Sheikh Mtoto maarufu kama Sheikh Shariff ambaye aliitingisha Tanzania kwa ufahamu mkubwa wa Qur’an akiwa na umri wa miaka tisa hatimaye amesalimu amri na kuokoka, katika kanisa la Pentekoste Motomoto jijini Dar es Salaam .
Sheikh Shariff ambaye jina lake halisi ni Sheikh Shariff Mohamed Mikidadi tayari amebatizwa na kupewa jina jipya la Michael Sylivester Sewando, ambapo hivi sasa analelewa kiroho katika kanisa hilo lililopo Keko chang’ombe jijini Dar es Salaam .
….Licha ya Sheikh Shariff sasa Michael Sewando kuzaliwa katika familia ya kikatoliki ya mzee Sylivester Sewando na mama yake Joyce Mokiwa, alisema alisilimu baada ya kutibiwa maradhi yake na mganga muumini wa dini ya Kiislamu wakati akiwa mtoto.Katika umri mdogo, jambo hilo lilimfanya ghafla ajikute akianza kuipenda dini ya kiislamu na ndipo aliamua kujiunga nayo, ingawaje wazazi wake walimpinga vikali.Alisema ilibidi aondoke Nyumbani kwao Kawe Ukwamani na kuhamia kwa ndugu wa kiislamu na kuanza kuswali katika msikiti wa Al Shariff, International Dawas’ Islamic Centre Kawe Dar es Salaam. (SIDC) alikoingizwa rasmi katika dini ya Kiislamu.Alisema mara baada ya kujiunga na dini hiyo na kuanza kuswali katika msikiti huo, alijikuta akipata ufahamu mkubwa wa elimu ya Qu’ran pasipo kufundishwa. Sheikh Shariff alisema anachojua ni kwamba uwezo wa kuijua Qur’an aliupata kutoka kwa majini 2900, yaliyomuingia baada ya kujiunga na Uislamu.Alisema majini hayo ndiyo sababu pekee iliyomfanya awe mahiri sana katika elimu ya dini ya kiislamu. Akizungumza na wahadhiri mbalimbali nje na ndani ya Tanzania huku akifanya miujiza na kuendesha mihadhara mingi ya kiislam.Kwa mujibu wa Sheikh huyo aliyeokoka, maeneo aliyowahi kutoa mihadhara ni Kawe,Tandika , Mbagala, Njoro, Kilimanjaro, Mwembe tayari nchini Kenya , viwanja vya msikiti Mkuu wa Jijini na Kampala nchini Uganda .Katika hali isiyokuwa ya kawaida, Sheikh Shariff alisema aliwahi kuishi chini ya bahari ya Hindi katika eneo la Maskati, nchini Oman , akifundishwa mambo mbalimbali na majini. Alisema akiwa chini ya bahari alikuwa akifundishwa na jini mkuu aliyemtaja kwa jina Lusifa ambalo ni la Shetani, ambapo alikuwa akilishwa mchanganyiko wa damu za binadamu na wanyama na mifupa ya farasi.Sheikh Shariff au Michael Sewando alisema Lusifa au mkuu wa majini ambaye alikuwa na umbo la mfano wa mjusi mkubwa, ndiye aliyemfundisha masuala ya uganga wa kienyeji kwa kutumia vitabu maarufu vya kijini. Mambo mengine aliyofanyiwa akiwa chini ya bahari ni pamoja na kuwekwa katika moto mkali kwa muda wa siku saba na baadaye katika baridi kali na giza totoro kwa siku hizo hizo.Nakumbuka nikiwa chini ya bahari ambako naamini ni kuzimu, Lusifa aliamuru kuwa kamwe nisilitaje jina la mtu aliyesulubiwa msalabani kwa maana yaYesu, kwa vile jina hilo ni baya na huharibu kazi za kuzimu. Pamoja na mambo mengine mengi ya ajabu aliyofanyiwa au kufundishwa na Lusifa, alisema baadaye alihitimu na kupatiwa mikoba mitatu iliyosheheni madawa ya mitishamba, viungo vya wanyama, binadamu na majoka. Unajua nilikuwa nafanya masuala ya kuagua watu kiganga huku pia nikiendesha mihadhara mbalimbali ya kiislamu’’ alisema akionyesha kitambulisho kinachoonyesha kuwa ni mganga wa kienyeji.Alisema katika shughuli zake aliwahi kuwasilimisha wakristo mbalimbali wakiwepo mapadri na wachungaji, ambapo ameahidi kuwarudisha kwa Yesu baada ya kuokoka. Aidha alibainisha kuwa aliwahi kuoa majini mawili na kusababisha ajali zilizopoteza maisha ya watu ili kupata damu na nyama za majini aliyokuwa akiyamiliki.Kuhusu jinsi alivyokutana na Yesu na kuokoka, alisema hivi karibuni wakati akielekea katika shughuli zake za uganga eneo la Mbagala Mgeni Nani, miguu yake ghafla ilinasa ardhini na akasikia sauti ya Yesu ikimwambia kwamba aachane na uchafu wake, ili atakaswe kwa damu yake Yesu lakini alitaka kupinga.Alisema akiwa katika hali ya kupinga sauti hiyo, alitokea mama mmoja aliyekuwa muislam lakini akaokoka, ambaye alimshauri aokoke na kumuongoza zaidi hadi katika kanisa la Pentekoste Motomoto lililoko Keko Chang’ombe alikomkiri Yesu na kuokoka baada ya kutolewa mapepo. Kanisa la Pentekoste Motomoto linaongozwa na Mchungaji Ibrahimu John ambaye kwa sasa ndiye baba wa kiroho wa Sheikh Shariff.Sheikh Shariff (Michael Sewando) alisema baada ya kuokoka, amekuwa akipata mashambulizi kutoka kwa majini na wachawi hivyo anaomba msaada wa maombi kutoka kwa wacha Mungu wote.SOURCE: MSEMA KWELI
Dah! usanii mtupu,kweli Dunia ina mambo fix kwenye siasa ,dini ma mengine mengi kumbe kifaa kilioa majini! hahahah ujue leo nimecheka mpaka basi,huyu ni msanii tu hana jipya naona kaamua atoke na style ya kuokoka inawezekana waislamu walishamshtukia kuwa ni fix
 
<p style="text-align: center;"><font color="#ff0000"><font size="4"><b>Sijabadili dini </b></font></font><br />
</p><br />
<br />
<br />
<br />
<br />
sorce tanzania DAIMA!!! <a href="http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=9159" target="_blank">http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=9159</a><br />
<br />
SASA TUAMINI GAZETI GANI MSEMA KWELI AU TANZANIA DAIMA...????!<br />
<br />
may take Mods hii thread haina tofauti na ule uzsshi wa shimbo! ificheni mpaka mpate uhakika! ili kijana wa watu aije akapata usumbufu usiokuwa wa lazima
<br />
<br />

Keshananga kwenye mikono salama ya Yesu, hivyo usumbufu kutoka kwa lewiathan aliyemkimbia ni lazima.
Lakini shetani huyo wa chini ya bahari amekwisha kushindwa vibaya kwa JINA la YESU.
.
 
<br />
<br />

Keshananga kwenye mikono salama ya Yesu, hivyo usumbufu kutoka kwa lewiathan aliyemkimbia ni lazima.
Lakini shetani huyo wa chini ya bahari amekwisha kushindwa vibaya kwa JINA la YESU.
.

Tuache ushabiki na tutumie akili , My point ni kwamba kwa nini TANZANIA DAIMA limeletaleta habari nyingine..kukanusha hizi habari.? according to them muandishi hadi akaongea naye shekh sharif akakanusha hizo habari .

je gazeti la msema kweli limesema habari ya uongo.

je TANZANIA DAIMA .. lemeandika habari za uongo..

je shehe sharif nayeye ni kigeugeu kama yule msanii wa uganda "kinyonga" alipoona umaarufu umeshuka ..

ndio maana nikasema habari hii si ya uhakika inaweza ikachafua jina la mtu na kumsababishia usumbufu

http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.php?id=9159
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom