Yepi majukumu ya First Lady?

Safari_ni_Safari

JF-Expert Member
Oct 5, 2007
23,268
17,097
Hivi mke wa rais ana majukumu gani ktaifa?Mbona huyu wa sasa anafanya shughuli nyingi za kisiasa na mara nyingi husafiri on her own unlike her predecessors?
 
Hatajwi kwenye KATIBA yetu. Anayoyafanya ni kwa moyo na hiari yake tu. Tunakosea tu kumwita mke wa RAIS badala ya mke wa JK.
 
Kwa kweli hata mimi simwelewi huyu First Lady wetu. Utadhani ni waziri asiye na wazara maalumu. Hivi majuzi wakati Mzee akitembelea Mkoa wa Mbeya, Mzee alipita baadhi ya wilaya na mama naye akijivinjari kwenye wilaya zingine. Kweli sielewi au huyu ni first lady president?
 
Huku kote ni kutafuta sifa kuwa kamfunika mama Anna Mkapa,si unaelewa tena wanawake wa kiswahili
 
Ingawa anayechaguliwa huwa ni Rais (ikiwa ni mwanaume) lakini kumekuwa na mabadiliko na mtazamo mpya kuhusu hao wake wa maraisi "First Ladies". Imeonekana katika jumuia ya kimataifa ni vema na wao wakawa na majukumu fulani fulani, hasa ya kijamii. Wanakuwa kama mabalozi wa waume zao "Rais" katika shughuli za kijamii kama uhamasishaji wa chanjo, mambo ya mama na mtoto "MCH", uchumi wa kina mama na kadhalika. Ndio maana kwa hivi sasa kwenye vikao vya marais kama mkutano wa AU, wake wa ma-rais huwa na mikutano yao tofauti inayozungumzia huduma za kijamii. (Off course wanapata posho kwa kufanya hivyo).
Turudi hapa, nampongeza huyu wa sasa walao anachokifanya kinaoneka, anakwenda kwenye ziara, anatembelea vikundi mbalimbali hasa vya kina mama, anahutubia, (kumbuka akisimama jukwaani porojo za kisiasa zitakuwepo tu kwa kuwa ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa). Lakini kwa ujumla nampongeza sana kwa kazi anayofanya. Huyu wa sasa ni bora sana kuliko aliyepita.
Kusafiri peke yake ni kujituma. Hasubiri ziara za mumewe. hata hivyo ujue pia kuwa akialikwa mahali analipwa.
 
Hatajwi kwenye KATIBA yetu. Anayoyafanya ni kwa moyo na hiari yake tu. Tunakosea tu kumwita mke wa RAIS badala ya mke wa JK.

Sasa kama hatajwi kwenye katiba ,hii bajeti yake inatoka wapi,na ipo kwenye wizara gani? au kuna bajeti huwa inapitishwa kwa ajili ya misafara ya mke wa raisi?
 
Hatajwi kwenye KATIBA yetu. Anayoyafanya ni kwa moyo na hiari yake tu. Tunakosea tu kumwita mke wa RAIS badala ya mke wa JK.
sasa mbona anatumia raslimali zetu kuzurula nnchi nzima, mbona anatoaga komandi kama anamalaka fuklani hivi, mbona anatembea na msururu mrefu wa magari , walinzi rukuki, aah mimi naona ni sanaa tu.
 
Huyu mama licha ya kuwa anafanya kazi nyingi za kijamii lakini pia ana ajenda za kisiasa kwenye ziara zake!
 
Sasa kama hatajwi kwenye katiba ,hii bajeti yake inatoka wapi,na ipo kwenye wizara gani? au kuna bajeti huwa inapitishwa kwa ajili ya misafara ya mke wa raisi?
Zd,
Ofisi ya Rais inatengewa mihela mingi tu. Na yeye mwenyewe kama aliyemtangulia ana mfuko wake unaitwa WAMA. Mama Maria Nyerere tu ndiye hakuwa "huru" kiasi hiki si unajua tena wanaume wa mkoa wa Mara kwa wake zao?
 
Ingawa anayechaguliwa huwa ni Rais (ikiwa ni mwanaume) lakini kumekuwa na mabadiliko na mtazamo mpya kuhusu hao wake wa maraisi "First Ladies". Imeonekana katika jumuia ya kimataifa ni vema na wao wakawa na majukumu fulani fulani, hasa ya kijamii. Wanakuwa kama mabalozi wa waume zao "Rais" katika shughuli za kijamii kama uhamasishaji wa chanjo, mambo ya mama na mtoto "MCH", uchumi wa kina mama na kadhalika. Ndio maana kwa hivi sasa kwenye vikao vya marais kama mkutano wa AU, wake wa ma-rais huwa na mikutano yao tofauti inayozungumzia huduma za kijamii. (Off course wanapata posho kwa kufanya hivyo).
Turudi hapa, nampongeza huyu wa sasa walao anachokifanya kinaoneka, anakwenda kwenye ziara, anatembelea vikundi mbalimbali hasa vya kina mama, anahutubia, (kumbuka akisimama jukwaani porojo za kisiasa zitakuwepo tu kwa kuwa ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa). Lakini kwa ujumla nampongeza sana kwa kazi anayofanya. Huyu wa sasa ni bora sana kuliko aliyepita.
Kusafiri peke yake ni kujituma. Hasubiri ziara za mumewe. hata hivyo ujue pia kuwa akialikwa mahali analipwa.
Yaani kutembea sana kwake ndo inamfanya bora zaidi kuliko Mama Anna Mkapa? We kweli umekaa kishabiki sana. Huoni kwamba anatumia pesa za umma kutembea na kutoa misaada, sasa waziri wa wanawake na watoto ana kazi gani basi? Afadhali hata Kagame kaamua kumpa uwaziri kabisa mkewe.
Ila huyu festiledi wa sasa ni porojo tu na kutumia vibaya pesa za taifa. Afanye kazi za kusaidia jamii kwa kutumia funds zake mwenyewe, siyo kutegemea pesa zetu za kodi.
 
sasa mbona anatumia raslimali zetu kuzurula nnchi nzima, mbona anatoaga komandi kama anamalaka fuklani hivi, mbona anatembea na msururu mrefu wa magari , walinzi rukuki, aah mimi naona ni sanaa tu.
Sasa hivi hata wake wa Marais, Makamu, WM waliofariki wanalipwa kiasi fulani cha pesa. Hiyo misururu ni mbwembwe tu na kujipendekeza kwa mume wa huyu mama aliyewateua.
 
Sasa hivi hata wake wa Marais, Makamu, WM waliofariki wanalipwa kiasi fulani cha pesa. Hiyo misururu ni mbwembwe tu na kujipendekeza kwa mume wa huyu mama aliyewateua.
sasa haya mambo ndio hutia sana hasira, sasa kama mamlaka na wajibu wake haujatafsiriwa kikatiba, Je tunalipa hizo posho kwa base ipi, kwa rate ipi, kwa sheria zipi, mimi kusema ukweli mke wa Kikwete-sio mke wa Rais ananiboaga sana kujidai nae ni sehemu ya mamlaka ya nnchi hii, tunabeba mizigo mizito sana, hawana huruma nasi...aah basi tu.
 
Mbona msafara wake una tumia ngao na sio STK kama zamani?.Juzi nilipishana nae na msafara mrefu tu..nadhani anapaswa kumsindikiza mzee ziarani n sio kivyakevyake...nasikia rais akiwa mwanamke hakuna first gentleman..anaitwa officila consort to the presidency...funny
 
Sina tatizo na ziara za mke wa Jakaya,tatizo langu ni matumizi ya fedha zetu kugharamia ziara zisizo na tija.Fedha zingekuwa zinatokana na michango ya hiyo NGO yake lingekuwa jambo la busara.
 
Kazi za hawa ma fist lady wa siku hizi ni kufungua SACOS na NGOS ili wapate chochote kwa manufaa yao na si kwa ajili ya wananchi. Nafikiri ni ufisadi wa aina yake. Sijui Mama Nyerere alifanya nini, lakina ukianzia kwa kwa mzee wa ruksa, Mkapa na huyu wa JK, utaona wamekuwa na sauti kubwa karibu sawa na waume zao.

Hiyo ndiyo ccm inayojenga matabaka badala ya kujenga Nchi.
 
Huyu mama licha ya kuwa anafanya kazi nyingi za kijamii lakini pia ana ajenda za kisiasa kwenye ziara zake!

Ni kweli ana agenda za kisiasa ndio maana kagombea kuwa mjumbe wa mkutano mkuu wakati tayari mmewe ni raisi, funy!! Inawezekana kashakua na ndoto za Hilary Clinton.
 
mimi kinacho niboa ni kule kufunga barabara anapokuja who is she mpaka apokelewa kama raisi? mnalazimishwa kusimamisha magari yenu kando hakuna kupita eti first lady anapita,,,this is bullshit..hana watoto kwani wa kulea nyumbani.
 
Infamous,
Hilo ndio suala linalonikera...ukisahtundika ngao kwenye msafara lazima watu wapishe njia
 
Back
Top Bottom