Safari_ni_Safari
JF-Expert Member
- Oct 5, 2007
- 23,268
- 17,097
Hivi mke wa rais ana majukumu gani ktaifa?Mbona huyu wa sasa anafanya shughuli nyingi za kisiasa na mara nyingi husafiri on her own unlike her predecessors?
Hatajwi kwenye KATIBA yetu. Anayoyafanya ni kwa moyo na hiari yake tu. Tunakosea tu kumwita mke wa RAIS badala ya mke wa JK.
sasa mbona anatumia raslimali zetu kuzurula nnchi nzima, mbona anatoaga komandi kama anamalaka fuklani hivi, mbona anatembea na msururu mrefu wa magari , walinzi rukuki, aah mimi naona ni sanaa tu.Hatajwi kwenye KATIBA yetu. Anayoyafanya ni kwa moyo na hiari yake tu. Tunakosea tu kumwita mke wa RAIS badala ya mke wa JK.
Zd,Sasa kama hatajwi kwenye katiba ,hii bajeti yake inatoka wapi,na ipo kwenye wizara gani? au kuna bajeti huwa inapitishwa kwa ajili ya misafara ya mke wa raisi?
Yaani kutembea sana kwake ndo inamfanya bora zaidi kuliko Mama Anna Mkapa? We kweli umekaa kishabiki sana. Huoni kwamba anatumia pesa za umma kutembea na kutoa misaada, sasa waziri wa wanawake na watoto ana kazi gani basi? Afadhali hata Kagame kaamua kumpa uwaziri kabisa mkewe.Ingawa anayechaguliwa huwa ni Rais (ikiwa ni mwanaume) lakini kumekuwa na mabadiliko na mtazamo mpya kuhusu hao wake wa maraisi "First Ladies". Imeonekana katika jumuia ya kimataifa ni vema na wao wakawa na majukumu fulani fulani, hasa ya kijamii. Wanakuwa kama mabalozi wa waume zao "Rais" katika shughuli za kijamii kama uhamasishaji wa chanjo, mambo ya mama na mtoto "MCH", uchumi wa kina mama na kadhalika. Ndio maana kwa hivi sasa kwenye vikao vya marais kama mkutano wa AU, wake wa ma-rais huwa na mikutano yao tofauti inayozungumzia huduma za kijamii. (Off course wanapata posho kwa kufanya hivyo).
Turudi hapa, nampongeza huyu wa sasa walao anachokifanya kinaoneka, anakwenda kwenye ziara, anatembelea vikundi mbalimbali hasa vya kina mama, anahutubia, (kumbuka akisimama jukwaani porojo za kisiasa zitakuwepo tu kwa kuwa ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM taifa). Lakini kwa ujumla nampongeza sana kwa kazi anayofanya. Huyu wa sasa ni bora sana kuliko aliyepita.
Kusafiri peke yake ni kujituma. Hasubiri ziara za mumewe. hata hivyo ujue pia kuwa akialikwa mahali analipwa.
Sasa hivi hata wake wa Marais, Makamu, WM waliofariki wanalipwa kiasi fulani cha pesa. Hiyo misururu ni mbwembwe tu na kujipendekeza kwa mume wa huyu mama aliyewateua.sasa mbona anatumia raslimali zetu kuzurula nnchi nzima, mbona anatoaga komandi kama anamalaka fuklani hivi, mbona anatembea na msururu mrefu wa magari , walinzi rukuki, aah mimi naona ni sanaa tu.
sasa haya mambo ndio hutia sana hasira, sasa kama mamlaka na wajibu wake haujatafsiriwa kikatiba, Je tunalipa hizo posho kwa base ipi, kwa rate ipi, kwa sheria zipi, mimi kusema ukweli mke wa Kikwete-sio mke wa Rais ananiboaga sana kujidai nae ni sehemu ya mamlaka ya nnchi hii, tunabeba mizigo mizito sana, hawana huruma nasi...aah basi tu.Sasa hivi hata wake wa Marais, Makamu, WM waliofariki wanalipwa kiasi fulani cha pesa. Hiyo misururu ni mbwembwe tu na kujipendekeza kwa mume wa huyu mama aliyewateua.
Huyu mama licha ya kuwa anafanya kazi nyingi za kijamii lakini pia ana ajenda za kisiasa kwenye ziara zake!