Joseverest
JF-Expert Member
- Sep 25, 2013
- 51,991
- 69,381
Naaam wasalam wakuu,
Ile siku maalumu iliokuwa ikisubiriwa kwa hamu hatimaye imefika..Pambano la watani wa jadi katika soka la bongo, leo mtoto hatumwi dukani
Karibuni katika matukio mubashara(live updates) ya mtanange huu wa kukata na shoka baina ya mahasimu wa Soka la bongo, #KariakooDerby Yanga na Simba utakaochezwa saa 11 jioni Estadio De Benjamin Mkapa.
Huu ni mchezo wa namba 160 ligi kuu ya NBC 2021/2022 Yanga akiwa ni mwenyeji wa mchezo wa leo dhidi ya mtani Simba.. mchezo uliopita wa ligi kuu uliochezwa December 11, 2021, timu hizi zilitoshana au kuchoshana nguvu kwa sare ya bila kufungana/Suluhu...0-0
Pia Simba mechi ya mwisho kimashindano imetoka kupoteza Penalti 4_3 kutoka Orlando Pirates mnamo tarehe 24/4/2022 na hivyo kufurumushwa nje ya mashindano ya kimataifa yaani katika kombe la Shirikisho Afrika. CAFCC.
Yanga ilicheza mechi ya mwisho ligi kuu na Namungo Fc tarehe 24/4/2022 na kushinda 2_1.
Watabiri wa mambo wanasema huu mchezo wa watani wa jadi unaweza kutoa taswira juu ya Ubingwa wa ligi kuu msimu huu..Yanga ikiwa kileleni mwa ligi na point 54 huku Simba akiwa na alama 41 (Tofauti ya point 13). Ni mchezo ambao unatarajiwa kuwa wa kasi, nguvu, akili, maarifa na uzoevu mwingi hasa ukizingatia timu hizi zinapokutana haijalishi nani yuko vizuri kwa form au kiwango, wachezaji hubadilika na kucheza soka la kiushindani sana....
Nani ataibuka kidedea? kaa nami hapa mwanzo, kati na mwisho kupata kila kinachojiri kutoka katika dimba hili lenye kumbukumbu nzuri ya Hayati Benjamin Mkapa Dar es salaam
NB: Je 'watatetema' au 'watatetemeka' tena?
_____________________________________________________________
Updates zaidi kukujia kadiri zinavyopatikana
1655' Timu zinajiandaa kuingia dimbani hapa
01' Mpira umeanzaaaa, simba wameanzisha
05' Simba wanapata faulo ya kwanza kuelekea Simba na inazaa kona ambayo inashindwa kuleta matokeo
12' Djuma Shaaban anacheza gonga safi na Mayele kulekea lango la Yanga, Inonga anatibua mipango
14' Simba wanapata faulo karibu na 18 ya Yanga, Diara anapangua na kuwa counter kuelekea Simba, Feisal anapiga shuti linalotoka nje
20' Timu bado zinasomana kwa shambulizi za hapa na pale
Yanga wanaenda mbele, Mayele anapitishiwa anaikosaa inaokolewa na Inonga
28' 🟡Morrison anaenda nje kutibiwa, anapewa kadi ya njano pia Diarra anapewa kadi ya njano kwa kufanya malumbano uwanjani
32' Sakho anamchezea rafu Kibwana, faulu Yanga wanapata inapigwa inaokolewa
37" Simba wanapata faulu, alishika job nje ya 18..inapigwa na Chama inatoka njee
39' Onyango anatibua mpira aliokuwa nao Fiston Mayele kuelekea langoni mwa Simba, Kona.
🟡
40' Vurugu zinatokea kwa lango la Simba...Moloko na Inonga wanapewa kadi ya njano wote wawili
wakati huo ni kona,inapigwa na Saidoo inaokolewa
45+2' Mugalu anamdondosha Aucho, free kick, Refa anakuwa mkali kwa Mugalu
45+3' Half time
45' Mpira umerejea na Yanga wanasogea langoni kwa Simba bila kupata faida ya goli
46' Simba wanagonga pasi kuelekea Yanga lakini mipango yao inatibuliwa
48' 🟡Khalid Aucho anapewa kadi ya njano kwa kumchezea ndivyo sivyo Sadio Kanoute
54' Kibu Dennis anaingia kuchukua nafasi ya Benard Morrisson, Mzamiru anaingia kuchukua nafasi ya Kanoute.
56' Mkude anapewa kadi ya njano kwa kumuangusha Saidoo
67' Nkane anaingia kuchukua nafasi ya Moloko
71' Almanusura Mayele aandikishe bao la kwanza, shuti lake linaishia kwenye nyavu za pembeni. Yanga 0-0 Simba
73' Mugalu anapiga kichwa kutoka kwenye mpira wa adhabu ndogo, Diarra anaukamata barabara
74' Nkane anapiga mpira unaoambaa langoni mwa Simba, Feisal anashindwa kuupata.
79' Farid Mussa anaingia kuchukua nafasi ya Feisal Salum
85' Simba wanafanya jaribio maridadi baada ya Diarra kupoteana langoni
90+4' Mpira umekwisha, Yanga anapata alama 55 na kuendelea kubaki kileleni na Simba anasalia namba mbili akiwa na alama 42.
========
Mwamuzi wa Mchezo wa Leo ni Ramadhani Kayoko na wasaidizi wake ( Frank Komba [Line1] & Mohamed Mkono [Line2] bila kusahau Elly Sasii [4th Official] ) ilivyotangazwa awali
Azam Tv kupitia chaneli ya Azam sports 1 HD watakuwa mubashara (live).
Kwa wanaotaka Link ikipatikana itawekwa hapa
-----------‐-------------------------------------------------
SIO RASMI utabiri Kikosi cha Simba kinachoanza (STARTING XI)
Manula,Kapombe,Zimbwe Jr,Onyango,Inonga, Mkude,Chama,Sakho,Morrison,Kagere,Bocco
Kocha: Pablo Franco Martin/Suleman Matola
utabiri wa Kikosi cha Yanga kinachoanza (STARTING XI)
Diarra,Shaban,Kibwana,Mwamnyeto,Job,Bangala,Aucho,Moloko,Ntibazonkiza,Feitoto,Mayele
Kocha: Cèdric Kaze
(Kocha Nasridin Nabi bado anatumikia adhabu ya kadi nyekundu kwa hiyo atakuwepo jukwaani)
UPDATES SAA 1630
KIKOSI RASMI CHA YANGA KINACHOANZA
DIARA
DJUMA
KIBWANA
JOB
MWAMNYETO (CAPTAIN)
BANGALA
AUCHO
MOLOKO
NTIBAZONKIZA
FEISAL
MAYELE
SUBs: Mshery,Bacca,Yassin,Mauya,Sureboy,Ngushi,Farid,Nkane,Makambo
KIKOSI RASMI CHA SIMBA: Formation 4-2-3-1 Manula,Kapombe,Hussein(C),Onyango,Henock,Mkude,Sakho,Kanoute,Mugalu,Chama,Morrison
Subs:Beno,Israel,Kennedy,Nyoni,Mzamiru,Bwalya,Bocco,Kibu,Mhilu
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
------------------------------------------------------------------
Sent from my M2101K6G using JamiiForums mobile app
Ile siku maalumu iliokuwa ikisubiriwa kwa hamu hatimaye imefika..Pambano la watani wa jadi katika soka la bongo, leo mtoto hatumwi dukani
Karibuni katika matukio mubashara(live updates) ya mtanange huu wa kukata na shoka baina ya mahasimu wa Soka la bongo, #KariakooDerby Yanga na Simba utakaochezwa saa 11 jioni Estadio De Benjamin Mkapa.
Huu ni mchezo wa namba 160 ligi kuu ya NBC 2021/2022 Yanga akiwa ni mwenyeji wa mchezo wa leo dhidi ya mtani Simba.. mchezo uliopita wa ligi kuu uliochezwa December 11, 2021, timu hizi zilitoshana au kuchoshana nguvu kwa sare ya bila kufungana/Suluhu...0-0
Pia Simba mechi ya mwisho kimashindano imetoka kupoteza Penalti 4_3 kutoka Orlando Pirates mnamo tarehe 24/4/2022 na hivyo kufurumushwa nje ya mashindano ya kimataifa yaani katika kombe la Shirikisho Afrika. CAFCC.
Yanga ilicheza mechi ya mwisho ligi kuu na Namungo Fc tarehe 24/4/2022 na kushinda 2_1.
Watabiri wa mambo wanasema huu mchezo wa watani wa jadi unaweza kutoa taswira juu ya Ubingwa wa ligi kuu msimu huu..Yanga ikiwa kileleni mwa ligi na point 54 huku Simba akiwa na alama 41 (Tofauti ya point 13). Ni mchezo ambao unatarajiwa kuwa wa kasi, nguvu, akili, maarifa na uzoevu mwingi hasa ukizingatia timu hizi zinapokutana haijalishi nani yuko vizuri kwa form au kiwango, wachezaji hubadilika na kucheza soka la kiushindani sana....
Nani ataibuka kidedea? kaa nami hapa mwanzo, kati na mwisho kupata kila kinachojiri kutoka katika dimba hili lenye kumbukumbu nzuri ya Hayati Benjamin Mkapa Dar es salaam
NB: Je 'watatetema' au 'watatetemeka' tena?
_____________________________________________________________
Updates zaidi kukujia kadiri zinavyopatikana
1655' Timu zinajiandaa kuingia dimbani hapa
01' Mpira umeanzaaaa, simba wameanzisha
05' Simba wanapata faulo ya kwanza kuelekea Simba na inazaa kona ambayo inashindwa kuleta matokeo
12' Djuma Shaaban anacheza gonga safi na Mayele kulekea lango la Yanga, Inonga anatibua mipango
14' Simba wanapata faulo karibu na 18 ya Yanga, Diara anapangua na kuwa counter kuelekea Simba, Feisal anapiga shuti linalotoka nje
20' Timu bado zinasomana kwa shambulizi za hapa na pale
Yanga wanaenda mbele, Mayele anapitishiwa anaikosaa inaokolewa na Inonga
28' 🟡Morrison anaenda nje kutibiwa, anapewa kadi ya njano pia Diarra anapewa kadi ya njano kwa kufanya malumbano uwanjani
32' Sakho anamchezea rafu Kibwana, faulu Yanga wanapata inapigwa inaokolewa
37" Simba wanapata faulu, alishika job nje ya 18..inapigwa na Chama inatoka njee
39' Onyango anatibua mpira aliokuwa nao Fiston Mayele kuelekea langoni mwa Simba, Kona.
🟡
40' Vurugu zinatokea kwa lango la Simba...Moloko na Inonga wanapewa kadi ya njano wote wawili
wakati huo ni kona,inapigwa na Saidoo inaokolewa
45+2' Mugalu anamdondosha Aucho, free kick, Refa anakuwa mkali kwa Mugalu
45+3' Half time
45' Mpira umerejea na Yanga wanasogea langoni kwa Simba bila kupata faida ya goli
46' Simba wanagonga pasi kuelekea Yanga lakini mipango yao inatibuliwa
48' 🟡Khalid Aucho anapewa kadi ya njano kwa kumchezea ndivyo sivyo Sadio Kanoute
54' Kibu Dennis anaingia kuchukua nafasi ya Benard Morrisson, Mzamiru anaingia kuchukua nafasi ya Kanoute.
56' Mkude anapewa kadi ya njano kwa kumuangusha Saidoo
67' Nkane anaingia kuchukua nafasi ya Moloko
71' Almanusura Mayele aandikishe bao la kwanza, shuti lake linaishia kwenye nyavu za pembeni. Yanga 0-0 Simba
73' Mugalu anapiga kichwa kutoka kwenye mpira wa adhabu ndogo, Diarra anaukamata barabara
74' Nkane anapiga mpira unaoambaa langoni mwa Simba, Feisal anashindwa kuupata.
79' Farid Mussa anaingia kuchukua nafasi ya Feisal Salum
85' Simba wanafanya jaribio maridadi baada ya Diarra kupoteana langoni
90+4' Mpira umekwisha, Yanga anapata alama 55 na kuendelea kubaki kileleni na Simba anasalia namba mbili akiwa na alama 42.
========
Mwamuzi wa Mchezo wa Leo ni Ramadhani Kayoko na wasaidizi wake ( Frank Komba [Line1] & Mohamed Mkono [Line2] bila kusahau Elly Sasii [4th Official] ) ilivyotangazwa awali
Azam Tv kupitia chaneli ya Azam sports 1 HD watakuwa mubashara (live).
Kwa wanaotaka Link ikipatikana itawekwa hapa
-----------‐-------------------------------------------------
SIO RASMI utabiri Kikosi cha Simba kinachoanza (STARTING XI)
Manula,Kapombe,Zimbwe Jr,Onyango,Inonga, Mkude,Chama,Sakho,Morrison,Kagere,Bocco
Kocha: Pablo Franco Martin/Suleman Matola
utabiri wa Kikosi cha Yanga kinachoanza (STARTING XI)
Diarra,Shaban,Kibwana,Mwamnyeto,Job,Bangala,Aucho,Moloko,Ntibazonkiza,Feitoto,Mayele
Kocha: Cèdric Kaze
(Kocha Nasridin Nabi bado anatumikia adhabu ya kadi nyekundu kwa hiyo atakuwepo jukwaani)
UPDATES SAA 1630
KIKOSI RASMI CHA YANGA KINACHOANZA
DIARA
DJUMA
KIBWANA
JOB
MWAMNYETO (CAPTAIN)
BANGALA
AUCHO
MOLOKO
NTIBAZONKIZA
FEISAL
MAYELE
SUBs: Mshery,Bacca,Yassin,Mauya,Sureboy,Ngushi,Farid,Nkane,Makambo
KIKOSI RASMI CHA SIMBA: Formation 4-2-3-1 Manula,Kapombe,Hussein(C),Onyango,Henock,Mkude,Sakho,Kanoute,Mugalu,Chama,Morrison
Subs:Beno,Israel,Kennedy,Nyoni,Mzamiru,Bwalya,Bocco,Kibu,Mhilu
++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
------------------------------------------------------------------
Sent from my M2101K6G using JamiiForums mobile app