SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,129
- 7,896
Wengine mara kwa mara tumekuwa tunajitahidi kusema ukweli na kuwapa maua yao hawa Yanga toka msimu huu unaanza.
Ni ukweli ulio wazi kuwa Yanga inacheza mpira wa kueleweka, ni timu yenye kasi na inaweza kulazimisha ushindi pale mambo yanapokuwa magumu.
Pamoja na kwamba kuna mara kadhaa katika ligi ya NBC ni kama ilibebwa kiaina mfano katika ile game ya Kagera Sugar ila "overall" hauwezi kubeza uwezo na kiwango ambacho wamekionyesha.
Naona kabisa hata kama wangepata ushindi mwembamba jana, Yanga ilikuwa na uwezo wa kwenda kulazimisha sare au hata ushindi katika mechi dhidi ya Al Ahly.
Ni ukweli ulio wazi kuwa Yanga inacheza mpira wa kueleweka, ni timu yenye kasi na inaweza kulazimisha ushindi pale mambo yanapokuwa magumu.
Pamoja na kwamba kuna mara kadhaa katika ligi ya NBC ni kama ilibebwa kiaina mfano katika ile game ya Kagera Sugar ila "overall" hauwezi kubeza uwezo na kiwango ambacho wamekionyesha.
Naona kabisa hata kama wangepata ushindi mwembamba jana, Yanga ilikuwa na uwezo wa kwenda kulazimisha sare au hata ushindi katika mechi dhidi ya Al Ahly.