Yanga elekezeni dua zenu kwenye mechi za Medeama

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,136
7,903
Wengi mmejikuta mnaangalia hatma ya Yanga kwa kuangalia tu mechi mbili za Yanga dhidi ya CRB na ile ya mwisho dhidi ya Al Ahly. Hakuna ambaye amewaza ni jinsi gani Medeama anaweza kuwa msaada mkubwa kwa Yanga.

Ukweli ni kuwa Yanga ni ngumu sana kuvuka kwa kucheza mechi zake pekee maana kama ambavyo tumejadili sana inahitaji amfunge CRB kwa tofauti ya goli 4 jambo ambalo ni gumu sana ingawa kwenye mpira lolote linaweza kutokea. Ikipata ushindi tofauti na huo Yanga inahitaji kupata angalau sare dhidi ya Al Ahly jambo ambalo nalo lina ugumu fulani.

Njia iliyo rahisi zaidi kwa Yanga ni kwa Yanga kumfunga CRB kwa ushindi wowote ule huku wakiombea Medeama ipate ushindi leo dhidi ya Al Ahly. Medeama ana nafasi kubwa ya kushinda leo kwa sababu Al Ahly bado hawako vizuri na wataendelea kuwakosa baadhi ya wachezaji wake muhimu kutokana na majeraha. Vilevile changamoto za hitilafu za ndege yao na uchovu wa safari unaweza ukawaathiri kwa kiasi fulani Al Ahly.

Matokeo ya mechi hizo mbili yakienda kama nilivyosema, kitakachobaki ni katika mechi za mwisho kwa Yanga kuiombea Medeama itoe sare dhidi ya CRB huku yenyewe haihitaji kupata sare wala ushindi kwenye mechi yake dhidi ya Al Ahly.

Kwenye head to head, Yanga ina faida mbele ya Medeama kwa hiyo ikitokea wamelingana points, Yanga anafuzu.
 
Wengi mmejikuta mnaangalia hatma ya Yanga kwa kuangalia tu mechi mbili za Yanga dhidi ya CRB na ile ya mwisho dhidi ya Al Ahly. Hakuna ambaye amewaza ni jinsi gani Medeama anaweza kuwa msaada mkubwa kwa Yanga.

Ukweli ni kuwa Yanga ni ngumu sana kuvuka kwa kutumia njia hiyo maana kama ambavyo tumeshajadili sana inahitaji amfunge CRB kwa tofauti ya goli 4 jambo ambalo ni gumu sana ingawa kwenye mpira lolote linaweza kutokea. Ikipata ushindi tofauti na huo Yanga inahitaji kupata angalau sare dhidi ya Al Ahly jambo ambalo nalo lina ugumu fulani.

Njia iliyo rahisi zaidi kwa Yanga ni kwa Yanga kumfunga CRB kwa ushindi wowote ule huku wakiombea Medeama ipate ushindi leo dhidi ya Al Ahly. Medeama ana nafasi kubwa ya kushinda leo kwa sababu Al Ahly bado hawako vizuri na wataendelea kuwakosa baadhi ya wachezaji wake muhimu kutokana na majeraha. Vilevile changamoto za hitilafu za ndege yao na uchovu wa safari unaweza ukawaathiri kwa kiasi fulani Al Ahly.

Matokeo ya mechi hizo mbili yakienda kama nilivyosema, kitakachobaki ni katika mechi za mwisho kwa Yanga kuiombea Medeama itoe sare dhidi ya CRB huku yenyewe haihitaji kupata sare wala ushindi kwenye mechi yake dhidi ya Al Ahly.

Kwenye head to head, Yanga ina faida mbele ya Medeama kwa hiyo ikitokea wamelingana points, Yanga anafuzu.
Hallelujah hallelujah hallelujah 🙏
 
Siioni Al Ahly ikiendelea kuwa na makali hasa nikitazama ile mechi yao dhidi ya CRB, walicheza mpira wa kawaida sana.

Yanga ana uwezo wa kukomaa kule Misri na akato sare, kikubwa kesho apate ushindi mzuri kama unavyosema, sare Yanga ana uwezo wa kuipata kule Cairo kama akienda kwa nidhamu.

Aucho, Mudathir, Pacome, Maxi ni viungo ila wanajua haswa kukaba pia.
 
Siioni Al Ahly ikiendelea kuwa na makali hasa nikitazama ile mechi yao dhidi ya CRB, walicheza mpira wa kawaida sana.

Yanga ana uwezo wa kukomaa kule Misri na akato sare, kikubwa kesho apate ushindi mzuri kama unavyosema, sare Yanga ana uwezo wa kuipata kule Cairo kama akienda kwa nidhamu.

Aucho, Mudathir, Pacome, Maxi ni viungo ila wanajua haswa kukaba pia.
Ni kweli wakikaza sare wanaweza kuipata Misri ila kesho kushinda 4-0 au 5-1 ni mtihani mkubwa ndiyo maana hayo mahesabu yanakuwa magumu zaidi.
 
Umeandika gazeti lote hili kuwashauri utopolo, baadae muanze kulalamika Mangungu hafai, Hivi mbumbumbu kwann huwa mnapoteza Muda mwingi kwa ajili ya sisi utopolo ili hali nyie mnayo matatizo kibao tu zaidi yetu
Leo malaika wa heri kaamka na nyie
 
Siioni Al Ahly ikiendelea kuwa na makali hasa nikitazama ile mechi yao dhidi ya CRB, walicheza mpira wa kawaida sana.

Yanga ana uwezo wa kukomaa kule Misri na akato sare, kikubwa kesho apate ushindi mzuri kama unavyosema, sare Yanga ana uwezo wa kuipata kule Cairo kama akienda kwa nidhamu.

Aucho, Mudathir, Pacome, Maxi ni viungo ila wanajua haswa kukaba pia.
"Yanga ana uwezo wa kukomaa kule Misri na akatoa sare"
upo usingizini unaota amka upesi...
 
Ni kweli wakikaza sare wanaweza kuipata Misri ila kesho kushinda 4-0 au 5-1 ni mtihani mkubwa ndiyo maana hayo mahesabu yanakuwa magumu zaidi.
Hivi nyie mbumbumbu habari za goli 4 mnazitoa wapi? Yanga hahitaji kushinda goli nyingi cha msingi ashinde hata goli moja then atafte sare away , itamsaidia nini akishinda goli 5 then apoteze mechi ya mwisho?
 
Labda kama umetoka kwenu buseresere juzi Yanga kasha toa sare hapo Cairo , washa pelekana matuta na Al Ahly, washa cheza hadi extra time
Da hizi habari ulipata wapi?yanga alifungwa goli moja bila ,kwa sababu nyubani alishinda moja bila wakaenda matuta .Kabla ya kuandika fahamu uachoandika ,yanga hajawahi kutoa sare cairo.
 
Wengi mmejikuta mnaangalia hatma ya Yanga kwa kuangalia tu mechi mbili za Yanga dhidi ya CRB na ile ya mwisho dhidi ya Al Ahly. Hakuna ambaye amewaza ni jinsi gani Medeama anaweza kuwa msaada mkubwa kwa Yanga.

Ukweli ni kuwa Yanga ni ngumu sana kuvuka kwa kucheza mechi zake pekee maana kama ambavyo tumejadili sana inahitaji amfunge CRB kwa tofauti ya goli 4 jambo ambalo ni gumu sana ingawa kwenye mpira lolote linaweza kutokea. Ikipata ushindi tofauti na huo Yanga inahitaji kupata angalau sare dhidi ya Al Ahly jambo ambalo nalo lina ugumu fulani.

Njia iliyo rahisi zaidi kwa Yanga ni kwa Yanga kumfunga CRB kwa ushindi wowote ule huku wakiombea Medeama ipate ushindi leo dhidi ya Al Ahly. Medeama ana nafasi kubwa ya kushinda leo kwa sababu Al Ahly bado hawako vizuri na wataendelea kuwakosa baadhi ya wachezaji wake muhimu kutokana na majeraha. Vilevile changamoto za hitilafu za ndege yao na uchovu wa safari unaweza ukawaathiri kwa kiasi fulani Al Ahly.

Matokeo ya mechi hizo mbili yakienda kama nilivyosema, kitakachobaki ni katika mechi za mwisho kwa Yanga kuiombea Medeama itoe sare dhidi ya CRB huku yenyewe haihitaji kupata sare wala ushindi kwenye mechi yake dhidi ya Al Ahly.

Kwenye head to head, Yanga ina faida mbele ya Medeama kwa hiyo ikitokea wamelingana points, Yanga anafuzu.
Unawaza ujinga usiokuwa na faida kwa unayemuwazia.

Kuelekea mechi ya mwisho, matokeo mazuri kwa Yanga ni Al Ahly ashinde dhidi ya Medeama.
Al Ahly akishinda leo anakuwa amefuzu kwa kufikisha point tisa hivyo mechi ya mwisho itakuwa ngumu ila haitokuwa ngumu kama Al Ahly angetafuta nafasi ya kufuzu.
Kesho Yanga anatakiwa ashinde ushindi wowote ule, ila kama atashinda goli nne basi atakuwa ameshafuzu moja kwa moja kama Al Ahly atashinda leo
 
Medeama akimfunga Al Ahly, itamlazimu Yanga ashinde mechi yake ya Mwisho kama Yanga itapata ushindi dhidi ya CRB kesho
 
Da hizi habari ulipata wapi?yanga alifungwa goli moja bila ,kwa sababu nyubani alishinda moja bila wakaenda matuta .Kabla ya kuandika fahamu uachoandika ,yanga hajawahi kutoa sare cairo.
Na kipindi kile wame enda extra time ilikuaje?
 
Al ahly ni kama Baba mwenye Nyumba hata akiludi saa 8 usiku lazima tu mfungue mlango...kwahiyo mtoeni kabisa kwenye hayo mahesabu ya Tuki waki,

Al ahly hilo kundi Vyura watake wasitake lazima aongoze.
 
Back
Top Bottom