Yanga bingwa 2022/2023 Simba tujikite CAF na mwakani

bulabo

JF-Expert Member
Aug 20, 2015
620
759
Kwa hali ilivyo Jana Yanga kushinda mechi Ngumu dhidi ya IHEFU ambapo haikuwa na nyota wao wengi hii imefuta ndoto za SImba kuwa bingwa Msimu huu. Yanga wana mechi Tatu za Ugenini Singida ambapo ni timu nyepesi sana kwa Yanga. Wana Mbeya CIty na Prison mechi hizi hawawezi kupoteza mechi zote.

Simba tulijichanganya mechi ya Azam kupoteza na mechi ya Kagera KMC(2-2) pia. Simba kwa sasa tuwekeze Nguvu mashindano ya CAF na mechi ya Simba Vs Yanga kulipa kisasi. Ligi tujiandae vizuri mwakani.

Simba kama OKRAH anaondoka aondoke tulete Fei Toto. Tujipange Next Season mwaka huu labda FA azam ndio kombe ambalo tukijipanga tunaweza kuchukua.

Pia tununue beki msimu ujao Onyango amechoka jamani!!

NAWASILISHA.
 
Kumbe simba bado mnazo ndoto za kuwa bingwa🤣🤣🤣 kujipa matumaini ni vizuri lakini kiuhalisia mlishapotea njia gape la point 6 sio dogo kwenye ligi yenye ushindani.

Na hili simba wawe mabingwa inatakiwa yanga ipoteze mechi mbili na simba ishinde zote zilizobaki jambo ambalo ni sawa na ngamia kupenya kwenye tundu la sindano,.

Bado simba ana mechi na yanga pia na azam, yanga keshamalizana na azam kwa kumpa kichapo ivyo vita ya kugombea nafasi ya pili imebaki kwa simba na azam, Na bado yanga kabakisha mechi 3 tu mikoani ambazo ni ngumu kwa yanga hii kupoteza kirahisi, mechi zilizobaki ni kwa mkapa nafikiri jibu unalo
 
Yanga ni BINGWA Kwa Miaka mitatu mfululizo.

Mwaka I 2023-2024 UBINGWA ungeenda Azamu ila wamesha zingua, Kuna mambo machache wanaweza kurekebisha.
 
Kwa hali ilivyo Jana Yanga kushinda mechi Ngumu dhidi ya IHEFU ambapo haikuwa na nyota wao wengi hii imefuta ndoto za SImba kuwa bingwa Msimu huu. Yanga wana mechi Tatu za Ugenini Singida ambapo ni timu nyepesi sana kwa Yanga. Wana Mbeya CIty na Prison mechi hizi hawawezi kupoteza mechi zote.

Simba tulijichanganya mechi ya Azam kupoteza na mechi ya Kagera KMC(2-2) pia. Simba kwa sasa tuwekeze Nguvu mashindano ya CAF na mechi ya Simba Vs Yanga kulipa kisasi. Ligi tujiandae vizuri mwakani.

Simba kama OKRAH anaondoka aondoke tulete Fei Toto. Tujipange Next Season mwaka huu labda FA azam ndio kombe ambalo tukijipanga tunaweza kuchukua.

Pia tununue beki msimu ujao Onyango amechoka jamani!!

NAWASILISHA.
Mpira unasimuliwaga? Mechi ya Simba na Yanga nani atakuwa mwenyeji?
 
Back
Top Bottom