Ipi ni comeback ya kibabe zaidi: Simba vs Mufulira Wanderers au hii ya Yanga vs CR Belouizdad

SAYVILLE

JF-Expert Member
Mar 25, 2010
5,129
7,898
Mwaka 1979 kulitokea maajabu ya soka ambayo mpaka leo bado hayajaweza kurudiwa katika historia ya soka la Afrika.

Simba ilicheza mchezo wa Klabu Bingwa Afrika na timu ya Mufulira Wanderers ya Zambia. Mufulira ilikuwa moja ya timu bora Afrika kipindi hicho. Katika mechi ya kwanza iliyofanyika Tanzania, Simba ilikung'utwa 0-4. Katika hali ya kawaida, hapo timu inaenda mechi ya marudiano ugenini kukamilisha tu ratiba ila katika hali ya kushangaza, Simba ilipindua matokeo kwa kushinda 5-0 mbele ya Rais wa Zambia Keneth Kaunda na hivyo kuvuka hadi hatua inayofuata.

Msimu huu wa 2023-2024, Yanga ilienda kucheza na CR Belouizdad katika mzunguko wa pili wa makundi huku ikiwa imeshafungwa 0-3 katika mechi ya kwanza. Kutokana na kanuni za CAF zilivyo na msimamo wa kundi lao, Yanga ilihitaji ushindi wa goli 4-0 ili automatically iwe imefuzu. Ushindi wowote tofauti na huo ingeilazimu Yanga kwenda kutafuta kufuzu katika mechi ya mwisho dhidi ya Al Ahly. Mpira una maajabu yake, Yanga ikafanikiwa kupata huo ushindi wa 4-0 dhidi ya CRB na hivyo kufuzu hadi hatua ya robo fainali.

Kwa mtazamo wako, ipi kati ya hizi comeback mbili ni kali zaidi? Tukumbuke Simba ilipata ushindi wa 5-0 katika ardhi ya ugenini na ni rekodi ambayo bado haijafikiwa mpaka leo katika kumbukumbu za CAF.
 
20240229_145450.jpg
 
Umechanganya madesa, Yanga alikuwa anatafuta point afu magoli tofauti na Simba ilikuwa magoli kwanza na wala sio point
Nadhani wewe madesa ndo yamekuchanganya. Simba ilikuwa ni lazima ishinde (ipate point zote za mchezo) na ili ivuke automatically ilihitaji huo ushindi wa 5-0.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Mwaka 1979 kulitokea maajabu ya soka ambayo mpaka leo bado hayajaweza kurudiwa katika historia ya soka la Afrika.

Simba ilicheza mchezo wa Klabu Bingwa Afrika na timu ya Mufulira Wanderers ya Zambia. Mufulira ilikuwa moja ya timu bora Afrika kipindi hicho. Katika mechi ya kwanza iliyofanyika Tanzania, Simba ilikung'utwa 0-4. Katika hali ya kawaida, hapo timu inaenda mechi ya marudiano ugenini kukamilisha tu ratiba ila katika hali ya kushangaza, Simba ilipindua matokeo kwa kushinda 5-0 mbele ya Rais wa Zambia Keneth Kaunda na hivyo kuvuka hadi hatua inayofuata.

Msimu huu wa 2023-2024, Yanga ilienda kucheza na CR Belouizdad katika mzunguko wa pili wa makundi huku ikiwa imeshafungwa 0-3 katika mechi ya kwanza. Kutokana na kanuni za CAF zilivyo na msimamo wa kundi lao, Yanga ilihitaji ushindi wa goli 4-0 ili automatically iwe imefuzu. Ushindi wowote tofauti na huo ingeilazimu Yanga kwenda kutafuta kufuzu katika mechi ya mwisho dhidi ya Al Ahly. Mpira una maajabu yake, Yanga ikafanikiwa kupata huo ushindi wa 4-0 dhidi ya CRB na hivyo kufuzu hadi hatua ya robo fainali.

Kwa mtazamo wako, ipi kati ya hizi comeback mbili ni kali zaidi? Tukumbuke Simba ilipata ushindi wa 5-0 katika ardhi ya ugenini na ni rekodi ambayo bado haijafikiwa mpaka leo katika kumbukumbu za CAF.
Watu wa simba wataisifia ya kwao na wa yanga wataisifia ya kwao tena watasema hii wameiona
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom