mtwa mkulu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2013
- 8,098
- 9,994
HABARI ZA MOJA KWA MOJA KUTOKA MEDANI YA KIVITA TEL AVIV NA GAZA PALESTINE
Kombora likilipuka eneo la Gaza usiku wa jumapili
09 Oct 2023
Wakuu heshima kwenu.
Habari Za hivi punde kutoka uwanja wa kivita zinadokeza kuwa watu 700 wameuliwa upende wa Israeli huku watu 400 wakithibitika kuuliwa upande wa Palestine. Hospitali za mjini Gaza zimefurika maelefu ya majeruhi. Mpaka kufikia asubuhi ya Leo tayari zaidi ya wapalestina laki moja wamekimbia makazi yao.
KUTOKA TEHRAN HIVI LEO
Iran "haikuhusika" katika shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa Hamas kusini mwa Israel, ujumbe wake katika Umoja wa Mataifa umesema.
"Tunasimama kwa nguvu katika kuunga mkono Palestina; hata hivyo, hatuhusiki katika shambulio la Palestina, kwani linatekelezwa na Palestina yenyewe," ilisema katika taarifa ya Jumapili, kulingana na Reuters
MELI YA KIVITA KUTOKA MAREKANI IMEWASILI KARIBU NA ISRAELI LEO
Meli ya kubeba ndege ya USS Gerald R. Ford inaelekea eneo hiloImage caption:
Marekani inasema inahamisha shehena ya ndege, meli na jeti hadi mashariki mwa Mediterania na pia itaipa Israel vifaa na risasi zaidi.
Hii inafuatia shambulio la Hamas kusini mwa Israel, ambalo Rais Biden aliliita "shambulio lisilokuwa na kifani na la kutisha".
Marekani pia ilikuwa ikifanya kazi ya kuthibitisha ripoti kwamba raia wake walikuwa miongoni mwa waliouawa na kuchukuliwa mateka, Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken amesema.
Israel inasema zaidi ya watu 700 wameuawa na 100 kutekwa nyara.
Mjini Gaza, zaidi ya watu 400 wameuawa kufuatia mashambulizi ya anga ya kulipiza kisasi ya Israel, kulingana na maafisa wa Palestina.
Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alisema meli ya kubeba ndege ya USS Gerald R. Ford, meli ya kubebea makombora na zana za kuharibu makombora vimepelekwa katika eneo hilo. Ndege za kivita za Marekani pia zinapelekwa Gaza.
Misaada zaidi ya kijeshi kwa Israel itatumwa katika siku zijazo, Ikulu ya White House ilisema.
Rais wa Iran Ebrahim Raisi ameeleza kuunga mkono shambulio la Hamas akisema Israel inapaswa kuwajibika kwa kuhatarisha eneo hilo.
October 11, 2023
Umeme ulikatika leo baada ya kituo pekee cha umeme katika eneo hilo kukosa mafuta. Hospitali, ambazo zimejaa maelfu ya majeruhi, zinasema zinakosa dawa.
Umoja wa Mataifa unasema watu nusu milioni wa Gaza hawajapata mgao wao wa chakula tangu Jumamosi. Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuanzishwa eneo la kibinadamu. Afisa mmoja wa Misri aliiambia BBC kwamba serikali mjini Cairo ilikuwa katika majadiliano na pande zote kujaribu kuruhusu msaada kuingia Gaza kupitia Misri hata kama ni kwa saa chache tu.
Wakati huo huo, kuna matarajio makubwa kwamba Israel hivi karibuni itaimarisha zaidi operesheni yake kwa mashambulizi ya ardhini.
Msemaji wa Israel alisema vikosi, ikiwa ni pamoja na askari wa akiba 300,000, walikuwa karibu na mpaka wakijitayarisha kwa kwa mashambulizi, ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na "mwisho wa vita hivi Hamas hawana tena uwezo wowote wa kijeshi".
Kwa idadi ya watu waliouawa na Hamas mwishoni mwa juma ambayo sasa inajulikana kuwa zaidi ya 1,200, ujumbe huo utakuwa na uungwaji mkono mkubwa wa umma wa Israeli
Kombora likilipuka eneo la Gaza usiku wa jumapili
09 Oct 2023
Wakuu heshima kwenu.
Habari Za hivi punde kutoka uwanja wa kivita zinadokeza kuwa watu 700 wameuliwa upende wa Israeli huku watu 400 wakithibitika kuuliwa upande wa Palestine. Hospitali za mjini Gaza zimefurika maelefu ya majeruhi. Mpaka kufikia asubuhi ya Leo tayari zaidi ya wapalestina laki moja wamekimbia makazi yao.
KUTOKA TEHRAN HIVI LEO
Iran "haikuhusika" katika shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa Hamas kusini mwa Israel, ujumbe wake katika Umoja wa Mataifa umesema.
"Tunasimama kwa nguvu katika kuunga mkono Palestina; hata hivyo, hatuhusiki katika shambulio la Palestina, kwani linatekelezwa na Palestina yenyewe," ilisema katika taarifa ya Jumapili, kulingana na Reuters
MELI YA KIVITA KUTOKA MAREKANI IMEWASILI KARIBU NA ISRAELI LEO
Meli ya kubeba ndege ya USS Gerald R. Ford inaelekea eneo hiloImage caption:
Marekani inasema inahamisha shehena ya ndege, meli na jeti hadi mashariki mwa Mediterania na pia itaipa Israel vifaa na risasi zaidi.
Hii inafuatia shambulio la Hamas kusini mwa Israel, ambalo Rais Biden aliliita "shambulio lisilokuwa na kifani na la kutisha".
Marekani pia ilikuwa ikifanya kazi ya kuthibitisha ripoti kwamba raia wake walikuwa miongoni mwa waliouawa na kuchukuliwa mateka, Waziri wa Mambo ya Nje Antony Blinken amesema.
Israel inasema zaidi ya watu 700 wameuawa na 100 kutekwa nyara.
Mjini Gaza, zaidi ya watu 400 wameuawa kufuatia mashambulizi ya anga ya kulipiza kisasi ya Israel, kulingana na maafisa wa Palestina.
Waziri wa ulinzi wa Marekani Lloyd Austin alisema meli ya kubeba ndege ya USS Gerald R. Ford, meli ya kubebea makombora na zana za kuharibu makombora vimepelekwa katika eneo hilo. Ndege za kivita za Marekani pia zinapelekwa Gaza.
Misaada zaidi ya kijeshi kwa Israel itatumwa katika siku zijazo, Ikulu ya White House ilisema.
Rais wa Iran Ebrahim Raisi ameeleza kuunga mkono shambulio la Hamas akisema Israel inapaswa kuwajibika kwa kuhatarisha eneo hilo.
October 11, 2023
Hali ya kibinadamu ya Gaza inazidi kuwa mbaya, huku Israel ikitarajiwa kuanza mashambulizi ya ardhini
Huku Gaza sasa ikiwa imezingirwa kikamilifu na wanajeshi wa Israel na baada ya siku tano za mashambulizi ya mabomu, hali ya kibinadamu inazidi kuwa mbaya.Umeme ulikatika leo baada ya kituo pekee cha umeme katika eneo hilo kukosa mafuta. Hospitali, ambazo zimejaa maelfu ya majeruhi, zinasema zinakosa dawa.
Umoja wa Mataifa unasema watu nusu milioni wa Gaza hawajapata mgao wao wa chakula tangu Jumamosi. Umoja wa Mataifa umetoa wito wa kuanzishwa eneo la kibinadamu. Afisa mmoja wa Misri aliiambia BBC kwamba serikali mjini Cairo ilikuwa katika majadiliano na pande zote kujaribu kuruhusu msaada kuingia Gaza kupitia Misri hata kama ni kwa saa chache tu.
Wakati huo huo, kuna matarajio makubwa kwamba Israel hivi karibuni itaimarisha zaidi operesheni yake kwa mashambulizi ya ardhini.
Msemaji wa Israel alisema vikosi, ikiwa ni pamoja na askari wa akiba 300,000, walikuwa karibu na mpaka wakijitayarisha kwa kwa mashambulizi, ili kuhakikisha kwamba kunakuwa na "mwisho wa vita hivi Hamas hawana tena uwezo wowote wa kijeshi".
Kwa idadi ya watu waliouawa na Hamas mwishoni mwa juma ambayo sasa inajulikana kuwa zaidi ya 1,200, ujumbe huo utakuwa na uungwaji mkono mkubwa wa umma wa Israeli