Yanayojiri mkutano wa NCCR - Disemba 17, 2011

Status
Not open for further replies.
Mkosamali karibu CDM na utarudi tu mjengoni,hata Kafulila utasamehewa makosa yako kama utakuwa umejirekebisha,atawahangaisha sana huyo kibaraka wa CCM,na kama leo kaleta wajumbe feki hakikisheni mnamuumbua kabisa

Eheeeee! yaani wewe umeifanya CDM kuwa sehemu ya kupokea na kulea puppets kama Mkosamali na Kafulila. These pple cant stand on their own. They are virus that CDM can not entertain. Labda waende CCM B
 
Du nimesubiri sana kujuzwa yaliyojili mpaka nimechoka,hata repoter wetu haonekani tena,sijui ndio keshalishwa ban na Mambatia?
 
Kikao kinaendelea hoja iliyopo mezani ni kuwavua uanachama akina Kafulila, Rungwe,Bwana, Mkosamali.Au waombe radhi moto Mkali!
 
Kwenye Mgogoro huu inaonekana dhahiri kuwa Wajumbe wamegawanyika sana, hivi karibuni Msaidizi wa Mwenyekiti Danda Juju ameonekana akimukandia sana Mbatia na Moses Machali kwasababu , MBATIA alimushawishi DANDA amuunge mkono ili amupitishe Kwenye nafasi ya kugombea Ubunge Afrika Mashariki.

Taarifa zinaonyesha kuwa Mbatia aliambiwa na CCM baada ya kushindwa Ubunge Kawe kuwa amufungulie kesi Halima Mdee wa Chadema ili ushindi wa Halima Mdee Utengiuliwe na ukirudiwa CCM itatumia Nguvu zote na kunyakua Jimbo hilo.

Mkataba huo ulikuwa CCM wamupe Ubunge Jemus Mbatia kupitia Afrika Mashariki Kwa hiyo Mbatia anajua kuwa yeye ni Mbunge tayari kupitia Afrika Mashariki, lakini ni lazima ashinde kesi ya Kawe. Gharama zote za kuendesha Kesi hiyo zinatoka CCM na sio NCCR!

Ndani ya NCCR Danda Juju ana jina kubwa Kugombea Ubunge Afrika Mashariki lakini Hawezi kupita kama Mbatia hamuungi Mkono!!!

Danda alifanya Kampeni Mbaya dhidi ya Mbatia kuwambia Wajumbe wa NEC kuwa endapo Mbatia ambaye ni mwenyekiti wa NCCR atakuwa Mbunge kupita Afrika mashariki basi NCCR itakufa kwakuwa watu watasema ni CCM-B.

Mbatia aliposikia njama hizo akakaa kikao na Dr Mvungi wakapatana kwamba ni bora Dr Mvungi au katibu Mkuu Samuel Ruhuza Wakagombea Ubunge Afrika Mashariki na si Danda JUJU.

Huu ndio umafia wa Mbatia na kundi lake na Danda juju anajua hivyo amenoa upanga kumukata Mbatia leo!!!
Hapa ndipo mahali palipo mfanya Mbatia kuagiza watu wanaoitwa Mabonce Kutoka CCM Jeshi ambalo halipo kwenye katiba ya NCCR.

Ndani ya Katiba ya CUF kuna kitengo cha Blue Guard, na Katiba ya CDM kuna kitengo cha Red Brigade na CCM wana Green Gud lakini Ndani ya NCCR hakuna kitengo cha Mabounce lakini kuna kitengo cha VIBARAKA wa CCM wanaofahamika na kulipwa na MBATIA.

Ma-bouncer hao wanalipwa na Mbatia na si NCCR na pesa zote zinatoka CCM.

Sasa kama Kafulila wamevunja katiba kwa kuongea nje ya vikao iweje mtu ambaye amevunja katiba na kuitisha jeshi kutisha mkutano wa Halmashauri kuu?

Hivi unaweza kuwa na Uhuru kulindwa na mtu usiyemjua? Hapa hoja hii naacha kwenu!

Kwa nini asiite polisi?

Mnaosubiri Mbatia ang'olewe uenyekiti NCCR imekula kwenu kwani jamaa huyu Hashikiki wala hakamatiki ndani ya chama chake. Alimfanyizia Marando nguli wa mageuzi na shushushu aliyebobea sembuse Sisimizi Kafulila na viroboto wenzake.

Nyuma ya Mbatia kuna CCM na usalama wa taifa .Mpaka sasa anayemmudu Mbatia ni Halima Mdee binti Chadema.
 
Kwa kuwa Mbatia kapita kuendelea na Uenyekiti sasa amekaa anaongoza kikao kwa ujasiri akitaka kulisulubu kundi la pili!Msuguano ni Mkali!
 
Mnaosubiri Mbatia ang'olewe uenyekiti NCCR imekula kwenu kwani jamaa huyu Hashikiki wala hakamatiki ndani ya chama chake. Alimfanyizia Marando nguli wa mageuzi na shushushu aliyebobea sembuse Sisimizi Kafulila na viroboto wenzake.

Nyuma ya Mbatia kuna CCM na usalama wa taifa .Mpaka sasa anayemmudu Mbatia ni Halima Mdee binti Chadema.
Jina lako wewe sio zuri ijapo unaweza kuwa na hoja nzuri!
 
Kuna mgogoro mkubwa unaoashiria Mapigano eneo Ada Estate karibu na ofisi za TCD zamani.

Kikao kinashindwa kuanza Mbatia kaleta Majeshi na wajumbe feki 25.

Mbatia hajawahi kuwa Mwanachama wa NCCR Mageuzi moyoni mwake!
 
Siasa ni mchezo mchafu ambao kila nikifikiria naumia sana moyoni kama leo asubuhi tumesikia kwenye vyombo vya habari kuwa kiongozi wa nchi yetu amewateua wale waliokuwa mawaziri ambao walishindwa kwenye ubunge mwaka 2010 kama vile Dk.Batilda Buriani,Philip Marmo,Deodoras Kamala na wengine aliowateua kipindi cha nyuma kidogo kama vile Basil Mramba na wengine akawapa ukuu wa mikoa kama vile Joel Bendera,Mwantumu Mahiza na wengineo,hivi uongozi ni kuwa CCM au ni kuwa na uwezo wa kuongoza?mbona kiongozi wetu anawabeba watu wake kwa sababu tu ni CCM?haoni kama anataka kusababisha maandamano kama yale ya Misri,Libya na nyinginezo?jamani wana Jamii Forum naombeni mnisaidie kwa hili.
 
Maskini Mbatia, huu ndo mwanzo wa mwisho wake. Kwa heri nyota kwaheri!
 
Jamani tunaomba taarifa sahihi basi. Naona kila mtu anapiga makelele tu. Aaaaaaaaarrrrrrrgggghhhhhh
 
yaani hii thread nimeifuatilia kwa muda mrefu lakini haina updates kabisa.sijui kama muanzisha thread ni mzima au la.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom