Elections 2010 Yanayojiri huko Shinyanga

kuna ndugu zetu huko hatuna raha mtujuze,ccm wameamua kuua ila mwisho wao unakaribia

Sasa hivi shy na vitongoji vyake vyote pako shwari kuanzia maeneo ya stendi mpya ya Ibinzamata, Katikati ya mji maeneo ya soko kuu.., majengo... ngokolo ..mwasele rubaga nk mpaka kolandoto.., ila tu ni kwamba walitangaza matokeo jana usiku na kumtangaza mtu wa ccm kwamba ameshinda kitu ambacho kilileta tena balaa jingine..kifupi ni kwamba jamaa walishindwa majimbo haya mawili ya Bukombe na Shinyanga mjini sasa wakawa wanaona fadhaa kuyaachia yote...Ila tushukuru mungu anazidi kutuonyesha aina ya viongozi tulionao..Mwakilishi wa NEC Mkoani hapa huenda akajiuzulu.
 
Nilijaribu kufuatilia mambo yaliyojiri huko shinyanga ambapo inasemekana kuwa Chadema wameshinda bali mheshimiwa akawaambia wabadili matokeo ndipo mgombea wa CCM alipotangazwa kiasi ambacho kimesababisha vurugu jengo la Manispaa nasikia limechomwa moto

Huu uchakachuaji sasa hata aibu hakuna. ("...Shelembi ambaye aliongoza kwenye kata 17, aliamua kutokubali matokeo hayo akidai kuwa hayaendani na rekodi walizonazo mawakala wa chama chake...". From mwananchi.co.tz)

Kwani kuna kata ngapi huko Shinyanga?
 
...Ila tushukuru mungu anazidi kutuonyesha aina ya viongozi tulionao..Mwakilishi wa NEC Mkoani hapa huenda akajiuzulu.

Anajiuzulu baada ya kupokea maagizo ya kishetani, na kuyatekeleza!! Angeziulu baada ya kukataa kutangaza uongo, akatangaza ukweli, na hivyo kuonyesha kutofautiana na mwajiri wake!!
 
Napata habari hapa kuwa Shinyanga mambo sio shwari. Eti kwanza mkurugenzi alitangaza matokeo kuwa Chadema wameshinda. Alafu akapotea na polisi wakatangaza ccm kushinda na kuchoma masanduku moto.

hii habari ni kweli?
 
Mambo yameanza kuiva na ndio inavyotakiwa mpaka kieleweke,,Go go go Hongera Dk .Slaaa kwa msimamo huu.
Wednesday, 03 November 2010 05:18
Dk Willbrod Slaa
MGOMBEA urais kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo, (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema, atayakataa matokeo ya urais yatakayotangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC) kwa kuwa kumefanyika wizi mkubwa wa kura.Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Dk Slaa alisema, kama NEC inaitakia mema nchi hii, ifute matokeo yote ya urais na uchaguzi urudiwe upya.

Dk Slaa ambaye pia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, alisema wamekuwa wakifuatilia matokeo ya nchi nzima kwa umakini mkubwa na wamegundua kuna wizi mkubwa wa kura kwenye nafasi za urais na ubunge.

"Kuna uchakachuaji mkubwa wa kura na kazi hiyo inafanywa na usalama wa taifa,"alisema Dk Slaa.
Chanzo:Mwananchi:Gazeti la habari za kiswahili la kila siku Tanzania, linaongoza
 
Slaa tuite nasi tutakuitikia, wote tuna haki sawa katika nchi hii, kama sisi tumeshinda tuachiwe tutawale sio kutuibia kura. CCM someni alama za nyakati, walikuwepo akina Mobutu wakatoka sembuse nyie CCM tena wezi wa kura!!
 
Safi ila mkuu zipo threads nyingi zinaongelea hilihili. Mods nadhani mambo yamekuwa mengi kwenu ndo maana inakuwa hivi!
 
Watu wa CHADEMA walipoenda ofisini kwake kudai atangaze matokeo...akasema mgombea wa CHADEMA Kashinda..Baadae wa CCM alivyoenda akawaambia wa CCM Kashinda tena kwa tofauti ya Kura Moja.. Kisha akatoka na kufunga Ofisi akachukua familia na mizigo akatokomea kusikojulikana......
Watu wenye Hasira wakachoma moto kimjengo hicho.... Fujo Fujo zikaendela vurugu tele Bahati nzuri Mashabiki wa Chadema wakawa wamekusanya data toka vituo vyote vya kupigia Kura! Data Wanazo akina Marando na Dr. Slaa ..tusubiri kitakakacho endelea.....
Habari kwa hisani ya Mwanausalama mmoja aliyepo Shinyanga
 
huwawezi CCM wana matambo wewe! hii yote ni shauri ya babu Mwalimu JK ....alijenga mfumo tata wa kulinda chama ,kiwe ni kama serikali !

kila mtu anaogopa serikali isiyo ya CCM ..wakitishiana kua itavuruga nchi ..maana CCM ndio nchi ya Ahadi !
 
Huyo msimamizi kama ningekuwa mimi namkamata nampa adhabu ya kujikwaa kwenye jiwe. yaani ajikwae tuuu kwa masaa 2 halafu tuone kama hajasema ukweli nani kashinda
 
malipo ya dhulma hayo. na hatatulia kamwe, atazunguka huku na huko na kukosa amani.
 
Na Wananchi wengi wa Shinyanga Mjini HAWAMTAKI Mbunge mteule bwana Stephen, Na inasemekana Ametishiwa kuwa akionekana mitaani watamfanyia Kitu Mbaya.... Ni Hasira ...Chuki ...dhidi ya DHULUMA!
 
Watu wa CHADEMA walipoenda ofisini kwake kudai atangaze matokeo...akasema mgombea wa CHADEMA Kashinda..Baadae wa CCM alivyoenda akawaambia wa CCM Kashinda tena kwa tofauti ya Kura Moja.. Kisha akatoka na kufunga Ofisi....

Nina mashaka sana na habari yako mkuu. Labda nina matatizo. Kwamba, mwanzo kabisa alikuwa peke yake ofisini and then wagombea/wafuasi wa CHADEMA na CCM wakawa wanamfuata kila mtu kwa wakati wake!??
 
Nina mashaka sana na habari yako mkuu. Labda nina matatizo. Kwamba, mwanzo kabisa alikuwa peke yake ofisini and then wagombea/wafuasi wa CHADEMA na CCM wakawa wanamfuata kila mtu kwa wakati wake!??

Acha mashaka hii habari ni ya kweli kila mtu anaijua so acha ubishi wakati msimamizi wa uchaguzi alipo waambia chadema wameshinda makundi ya wana chadema wakaanza kusherekea ushindi kwa maandamano kuelekea mjini umbali wa km 2 kutoka hapo walipokua wanahesabia kura. Kumbe huku nyuma msimamizi akatangaza kua ccm imeshinda ndipo hapo watu wakaanza kuchoma moto majengo.
 
Na Wananchi wengi wa Shinyanga Mjini HAWAMTAKI Mbunge mteule bwana Stephen, Na inasemekana Ametishiwa kuwa akionekana mitaani watamfanyia Kitu Mbaya.... Ni Hasira ...Chuki ...dhidi ya DHULUMA!

Zitaisha na kutulia. Tufanye kazi tupate mlo wetu wa kila siku. Tuachane na wanasiasa wapige domo wao wanalipwa wakati sisi tunaacha kazi zetu za kila siku za kutafuta mkate wetu na familia zetu
 
watashinda kwa staili hii siku zote lakini hawatashinda vita ambayo Baba wa taifa aliitangaza,Isipokuwa Mwnamume mmoja tu Dk Slaa asiye na woga wa kukumbatia marafiki waovu na wezi , anaye weza kutoa muongozo (vision) na anayeweza kumonitor na kuevaluate kazi iliyofanyika sio kuchez mdako na mchafu koge ,halafu unakimbia jioni kulala ,hujui hata kesho utavaa nini kwenda shule, THINK BIG NA PATA SHIDA KWA TAIFA LAKO
 
Zitaisha na kutulia. Tufanye kazi tupate mlo wetu wa kila siku. Tuachane na wanasiasa wapige domo wao wanalipwa wakati sisi tunaacha kazi zetu za kila siku za kutafuta mkate wetu na familia zetu

Yaani wewe inaonekana uko mbali sana,unafikiri siasa ni mambo ya wanasiasa tu.Hujui kuwa sera zinazo ongoza ufanyaji kazi wako ikiwa ni pamoja na mshahara, kodi,marupurupu na kila kitu ambacho unakiita mkate kinapangwa na wanasiasa.
Funguka,dunia hii kila kitu ni siasa,haijalishi umesoma kiasi gani,utakuwa chini ya wanasiasa,ndiyo maana tunawachagua maana siasa ni kwa wote.Ole wako uchague wanasiasa wabovu,utabakia masikini pamoja na kukaa kwenye mkoa unaotoa madini kwa wingi.
 
Back
Top Bottom