Yametimia, ndege ya ATCL, Dash8-Q400 angani

Yametimia, ndege ya ATCL, Dash8-Q400 angani

Mimi hofu yangu ni muda wa safari kuwa mrefu hivyo kushindwa kushindana na Fastest katika same root na hivyo kukosa faida na kushindwa kukua kibiashara. Sio mikoa yote ina idadi kubwa ya wananchi wanaweza kumudu kupanda ndege. Jamaa waumize kichwa na kufanya restructuring ya shirika sasa


kwa taarifa yako fast jet wanataka kuagiza na wao bombaider ili waendane na soko kwani wameshaona wamepigwa bao

ikumbukwe airbus hazitui maeneo korofi ambapo viwanja vyetu asilimia 80 ni viwanja korofi
 
Hivi Kenya Airways na Ethiopia Airline wana ndege ngapi ili tujipime nao!
Ethiopian wana ndege 78, kenya wana ndege 45 na rwandair wana ndege 8. Ila wote hao pia wanatumia ndege kama hizi za magu for short haul flights. Kenya hutumia jambo jet shirika dogo la kq.
1472576581722.jpg
1472576599681.jpg
1472576608458.jpg
1472576615929.jpg
1472576624358.jpg
 
Hivi ndege na "hedikopta" zina tofauti gani jameni?😀😀😀😀😀
 
Ndege ya ATCL angani ikipasua anga na mawingu kwa ajili ya Test Flight. Sasa ni tayari kwa safari ya kuja nyumbani.

Alama ya Twiga wetu inaenda kuruka na kutambaa katika milima na mabonde ya Tanzania. Tunarudi tena katika anga la Tanzania. Nia ya dhati iliyotumika kulifufua shirika hili, itumike pia kutuweka watanzania kama wamoja, kwa chuki na uhasama wa "kuminywa demokrasia", turudishwe na tuwe wamoja.

Tunaenda hatua kwa hatua,kwa ile kanuni yetu ya "JF be the first to know", welcome back home.

The Wings of the Kilimanjaro

View attachment 390071
Ndege ya ATCL angani ikipasua anga na mawingu kwa ajili ya Test Flight. Sasa ni tayari kwa safari ya kuja nyumbani.

Alama ya Twiga wetu inaenda kuruka na kutambaa katika milima na mabonde ya Tanzania. Tunarudi tena katika anga la Tanzania. Nia ya dhati iliyotumika kulifufua shirika hili, itumike pia kutuweka watanzania kama wamoja, kwa chuki na uhasama wa "kuminywa demokrasia", turudishwe na tuwe wamoja.

Tunaenda hatua kwa hatua,kwa ile kanuni yetu ya "JF be the first to know", welcome back home.

The Wings of the Kilimanjaro

View attachment 390071
Mkuu barafu ni kweli kwamba hizo ndege ni model ya kabla ya uhuru wa Tanganyika ?
 
Hivi ndege na "hedikopta" zina tofauti gani jameni?😀😀😀😀😀
Hedikopta sijawahi kusikia kitu hiyo. Labda helikopta. Zote ni ndege. Airplane huwa zinatua kwa matairi na huruka kwa kukimbia. Pia hizi zinakuwa na uwezo wa kuruka juu sana. Helikopta inatua kwa mapanga na haiwezi kwenda juu sana kwani haina oxygen system. Wengine wataongeza.
 
karibu home kabajaj ketu ka taifa,wabongo wanaongea sana ujue watakuteta wakiwa humo humo umewabeba,usikasirike tu ukapitiliza kiwanja na kutua shambani km mwenzio yuleee wa zamani alivyofanya kigoma.
Nakweli aisee hichi kibaji tunachokipigia promo ndio kitakuja zalisha ma boeng nakuwazidi hata wakina fast jet na prediction
 
Baada ya miaka 50+ tuko kwenye kuleteana picha ya ndege inayopaa tukiambiwa kwamba inakuja Tanzania!!

Mpaka Rwanda...ethiopia...kenya wametushinda!

by upepo wa pesa
 
Inapendeza sana kama mtu anajadili mada kama hizi,awe na ABC ya usafiri wa anga na changamoto zake.
Fastjet tunaenda kukimbiza sana sana.Kwa sbb yeye anatumia ndege aina ya A319 inayobeba abiria 156.
Sisi tunaenda kuwa na Dash8-400 abiria 78.Safari ya Mwanza to Dsm,ATCL inatumia saa 1.20 hadi 25 wakati Fastjet anatumia saa 1.10 hadi 15.ATCL anatumia tani 1.2 kwa safari hiyo,wakati fastjet anatumia tani 3.1 za mafuta JET A1 kwenda Mwanza.

ATCL anatuwa viwanja vyote Tz vyenye lami na vile vya vumbi,wakati Fastjet anatuwa viwanja vitano tu Tz kwa maana ya Mwanza,KIA,Dsm,Znz na Mbeya.Huku ATCL akituwa Kigoma,Tbr,Mbeya,Lindi,Mtwara,Arusha,Iringa,Songea,Musoma,Dodoma,Mpanda nk

Ili fastjet atuwe na kuruka,Runway ya kiwanja inatakiwa iwe km 2.3 wakati ATCL anatuwa kwenye kiwanja chenye 1.2 km,ambavyo ndo viwanja vingi vilivyopo Tanzania.

Kwa kulitambua hili,Fastjet ameamua kuanza kuuza ndege zake zooote,ili anunue walau E190 aendane na ushindani wa soko.Kuepuka ghalama za mafuta na vipuri.

Sasa hapo ni nani anamtishia mwenzake?Muwe mnafanya utafiti kabla ya kutoa mchango
Asante sana mkuu barafu.

Toa elimu, we lack knowledge ndio maana unaona watu wakihoji, ndege ipo kwenye 'test flight' kwa nini haifungi 'landing gears'?

Watu wanahoji kuhusu kununua Boeing au Airbus wakati hawajafuatilia na kujua running costs za aina hizo kwa local market.

Hata aina za engines watu wanahoji, ni kama nchi imejaa 'flight service engineers', na kila mtu anajua ABC zake.

Hili linanikumbusha BRT, kulizuka 'structural engineers' humu balaa, watu wakahoji upana wa barabara, vituo vya basi, 'milango itakuwa kushoto huku vituo vipo kulia', kupanda na kushuka kutakuwa na ngazi na mengine mengi ambayo ni BS tu.

Huwa nasema, 'always seek knowledge'.!! Hakuna kitu muhimu kama kujisomea ili kupata maarifa, bahati mbaya wengi wetu hata pages mbili hatuwezi kusoma.
 
Mkuu barafu ni kweli kwamba hizo ndege ni model ya kabla ya uhuru wa Tanganyika ?
Kampuni yenyewe haijaanzishwa kabla ya Uhuru,sasa itakuwaje ndege inayozalishwa na hiyo kampuni iwe ni "model" ya kabla ya Uhuru?

Ni sawa na kusema mtoto alizaliwa kabla ya Wazazi....Tafuta maarifa kwanza,tetesi sio uhakika,bali chanzo cha kuutafuta uhakika
 
kwa taarifa yako fast jet wanataka kuagiza na wao bombaider ili waendane na soko kwani wameshaona wamepigwa bao

ikumbukwe airbus hazitui maeneo korofi ambapo viwanja vyetu asilimia 80 ni viwanja korofi
Mkuu unamaanisha nini maeneo korofi? Eneo gani korofi lina abiria 132 WA kupanda ndege kila siku?
 
Ifike Tz haraka nipige nayo picha, Kama kupanda nimeshindwa kupiga picha napo nishindwe!
 
Inawauma sana hizi ndege mbili tena mpya,Ni nyie wapinzani mtakuwa wa kwanza kutumia ndege hizi kuendea kwenye operesheni zenu
Wapinzani wana hela ya kununulia tiketi za ndege?
Wapinzani hawalipi kodi? Je wanalipa kodi za miamala?
Wewe mpiga debe wa fisiem utaendelea kuisoma namba tu mpaka akili zikurudie. Fisiem mbele kwa mbele.
 
Tumefikia hatua nzuri sana
Hatua nzuri sana. Tumenunua ndege ya mapangaboi itakayofanya kazi mbili kwa mpigo. Kusafirisha abiria na pia kuwa machinjio ya ndege wanaojitia kihere here cha kustaajabia mapangaboi.
 
Nauhakika nitakuwa mtu wa kwanza kabisa kuipanda ndege yetu
 
Back
Top Bottom