Yamenikuta mwenzenu naombeni ushauri

Yamenikuta mwenzenu naombeni ushauri

mambo ya nyumba za kupanga hayo tena hasa wapangaji wengi mkikutana wanawake loh utajuta, mwingine ugomvi ndo tabia yake na atakutafuta kila awezavyo mpaka lengo lake litimie, cha msingi we kuwa kimya tu usimjibu wala kumuuliza chochote na salam endelea kumpa kama kawaida mwisho ataacha
 
Poleeeeeee mapito tu hayo ata marehemu kanumba aki act move moja unaitwa my angel alielekeza kuwa huwa kunakuwa na kipindi cha mpito pia
 
Achana nae....kaa kimya mwisho wa siku atajiona mjinga yeye.ukute hawara mwenyewe hana A wala Z af anakutia nuksi mama wa watu...akuaachee upumue .

Mama S unaakaunti mbili JF?
 
.we miss chagga. wewe!!! maneno hayang'ati eeh?..kumbuka Mungu aliumba mbingu na nchi kwa neno, na nakuhakikishia ukiambiwa maneno mabayaaaa/mabovuuuuu tena kutoka kwa mtu wa karibu waweza tamani dunia ipasuke na kukumeza, huyu mpangaji dawa ni apelekwe vyombo husika vinginevyo mwajei atakuwa na kesi ya kujibu siku si nyingi.

sawa mkuu
 
Habari za leo wana JF.

Mimi ni mama wa mtoto mmoja, nimeajiriwa.

Tatizo ambalo ninalo ni kuhusu mpangaji mwanzangu (ke) kaambiwa natoka kimapenzi na hawara yake lakini ukweli huyo hawara yake hata salamu hatusalimiani, sasa ananikosesha raha na maneno maneno yako. Nimeshindwa kuvumilia nikamwambia mwenye nyumba amwite na amwite na aliyemwambia kaniona mimi na hawara yake lakini amekuwa mkali kama pili pili anasisitiza ni kweli na huyo mwanaume anakujaga kwangu. Note: Naishi na wadogo zangu wakiume 2 na vyumba ni viwili.

Sasa nimeshindwa kumwelewa anataka nini au nimweleze vipi anielewe maana mi si mtu wa maneno na ni short temper nahisi akiendelea kuniletea mdomo nitakuwa na keshi ya kujibu.

Hekima zenu zinahitajika.

Ahsanteni.
Mama S.


hebu sema unatoka nae kivipi bana!!!

sipendi watu wanaomung'unya maneno!!

kwamba anakugegeda ama unamgegeda wewe? kuna mawili hapo!!
 
hebu sema unatoka nae kivipi bana!!!

sipendi watu wanaomung'unya maneno!!

kwamba anakugegeda ama unamgegeda wewe? kuna mawili hapo!!

we nae........kamung'unya nini hapo? na hujaelewa nini hapo? embu mpe ushauri acha hizoo banaaa!

hujambo lakini?

mama s mpuuze huyo mwanamke, mbona hayo ya kawaida sanaaaa
 
we nae........kamung'unya nini hapo? na hujaelewa nini hapo? embu mpe ushauri acha hizoo banaaa!

hujambo lakini?

mama s mpuuze huyo mwanamke, mbona hayo ya kawaida sanaaaa

hahahaaaa!!! Palomaaaaa!!! aisee nilikuwa nampiga biti mpangaji!!

mie mzima bana, nashangaa unazidi kunizingua bana..! nataka nipange moyoni mwako. lols!

pole sana mwajei.. kama vipi, hicho kidada kivute kando mkiwa wawili, kidunde ngumi za kutosha!! kitakuheshimu tu!!
 
Last edited by a moderator:
Achana nae....kaa kimya mwisho wa siku atajiona mjinga yeye.ukute hawara mwenyewe hana A wala Z af anakutia nuksi mama wa watu...akuaachee upumue .

Mama S unaakaunti mbili JF?

Hapana nina account moja.

Nimeshampuuzia sana sasa anaona nimenyamaza kaanza chokochoko.
 
hebu sema unatoka nae kivipi bana!!!

sipendi watu wanaomung'unya maneno!!

kwamba anakugegeda ama unamgegeda wewe? kuna mawili hapo!!

Sijamung'unya maneno.

Huyo hawara ni mwanaume. Anamaanisha nagegedana naye.
 
mambo ya nyumba za kupanga hayo tena hasa wapangaji wengi mkikutana wanawake loh utajuta, mwingine ugomvi ndo tabia yake na atakutafuta kila awezavyo mpaka lengo lake litimie, cha msingi we kuwa kimya tu usimjibu wala kumuuliza chochote na salam endelea kumpa kama kawaida mwisho ataacha

Nimejitahidi kumwepuka lkn mmmh. Ukipita mara anafonza mimi huwa nacheka sasa sijui kwavile nacheka simsemeshi anakereka.
 
Pole sana
Kawaida nyinyi ke kuoneana wivu, nina hakika kuna kawivu fulani ndio maana anakutafutia shari
 
Sijamung'unya maneno.

Huyo hawara ni mwanaume. Anamaanisha nagegedana naye.
nakupa mbinu za medani sasa!
tafuta muda ambao uko private na huyo mbaya wako! hakikisha umekula na umeshiba kabisa!

sasa cha kufanya, kachape makofi ya kutosha, kaambie kaache mazoea ya kifala na wewe!!

otherwise, muite mumewe, mwambie athibitishe mbele yake kuwa hajawahi kuona wala kula tunda lako!

plan three.. if 0ne and two has failed, report abuse kwa polisi jamii.
 
Ahsanteni kwa ushauri. Nitaufanyia kazi.

Mbekeche: Sina tabia ya kubadili wanaume najiheshimu sana na naheshimu familia yangu siwezi waonyesha wadogo zangu picha mbaya ila kinachomchanganya anaona maisha yangu tofauti na yake. Mi nafanya kazi ila yeye sijui anajishughulisha na nini pia kipindi cha nyuma tulikuwa tunasalimiana vzr akawa ananiambia tutoke twende Disco nikawa namkatalia. Sa sijui alichofikiria.

Pili huyo mwanaume ni mume wa Mtu alikuwa mpangaji hapo hapo nilipo sa sijui kwa vile ye kamchukulia mwenzake anadhani na mm nitamchukua.

Jifunze kumpuuza...
Ukianza kuchukua vijihatua, au kumuuliza ujue ndio utakuza hayo mambo akilini mwako...

Jibu mahususi kwa -------- ni silence

Ni hayo tu kwa sasa
 
nakupa mbinu za medani sasa!
tafuta muda ambao uko private na huyo mbaya wako! hakikisha umekula na umeshiba kabisa!

sasa cha kufanya, kachape makofi ya kutosha, kaambie kaache mazoea ya kifala na wewe!!

otherwise, muite mumewe, mwambie athibitishe mbele yake kuwa hajawahi kuona wala kula tunda lako!

plan three.. if 0ne and two has failed, report abuse kwa polisi jamii.

Ahsante kwa ushauri wako.

Kwa sababu anataka ugomvi mi nimeamua kumpuuzia maana sitakuwa na muda wakukimbizana posili na kesi.

Note. huyo si mume wake ni mume wa mtu.
 
Watu wa hivyo dawa yao ni ndogo sana;
Kodi ikiisha hama hapo na uhakikishe unatembea kweli na huyo sijui hawara sijui nani wake.

Kwa sasa mpuuze na achana naye;
ila jitahidi kuweka viwaro hadi aumie na apasuke.
 
Wivu tu unamsumbua,mdharau na mwisho wa siku atajiona mjinga tu
 
Mh, pole hayo yalishawahi kunikuta, tena bora wewe maneno matupu mimi nilishikiwa hadi kisu. Ila mwisho wa siku yule dada alinipigia magoti na kuniomba msamaha.
We mnyamazie, zizuie hasira zako maana kukaa kimya ni jibu la mjinga ila ukiona hakomi mchukue kweli huyo bwana ake lolz.
Teh teh hapo kwenye red ndilo lilikuwa wazo lako, huko kwingine ulikuwa unazunguka tu.
 
hama nyumba uachane naye kabisa km ukiona kuendelea kukaa hapo ni tatizo kwako na huwez kumvumilia. jiepushe na shari mdada
 
weka urafiki na mke wa huyo jamaa kisha mwambie kila kitu, kisha uwe unamkaribisha kwako, huyo mbaya wako kila akimuona atakuwa kama mbwa mkia nyuma.
 
Back
Top Bottom