OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,222
- 103,827
Tuhuma za Yanga kutupia majini wachezaji wake imenikumbusha nyuma kidogo. Imenikumbusha nyakati kina Ngasa, Ajibu, Domayo, Niyonzima (orodha ni ndefu) wakati wanaondoka Yanga.
Wakiwa kwenye piki wakataka kwenda kwingine kutafuta maisha mazuri zaidi ya waliyopata Yanga. Wote hawa walitamani kuondoka kwa amani kwani waliisaidia Yanga kufikia mafanikio na walitamani kuondoka kwa heshima. Ajabu hali ilikiwa tofauti kwani uongozi haukuwa tayari kuwaacha kwa wema. Hata pale walipolazimisha hatimaye waliondoka kwa chuki na kisununu, wakilaaniwa na kauli za "tutaona kama utatoboa"
Haya yalifanyika nyakati za Ajib kuja Simba, kina Ngasa na Domayo kwenda Azam. Hali hiyo imejirudia kwa Feitoto na Mayele. Uondokaji wa watu hawa ulifichwa sana kwa sababu za husda tu huku viongozi wakiamini vitisho vitasaidia.
Kipindi Niyonzima anakuja Simba, wana Yanga mpaka wakachoma jezi kumlaani. Hiyo ni roho ya kawaida kweli. Si ujini huo. Kumbuka kina Bangala na Djuma walivyoondoka Yanga.
Kwa hali hii hata kama ni kweli hawafugi majini, lakini kumbania mtu maisha ni zaidi ya kumtupia majini. Tazama suala ya Fei mpaka Rais wa nchi anaingilia kati, Hiyo roho ni zaidi ya jini. Nafikiri hata jini lenyewe lilishangaa. Fei sio kichaa mpaka aseme ili abaki Yanga basi Hersi aondoke.
Hizi tabia za kishwahili zinatakiwa kukemewa sio tu na wanasoka bali kina mpenda maendeleo.
Wakiwa kwenye piki wakataka kwenda kwingine kutafuta maisha mazuri zaidi ya waliyopata Yanga. Wote hawa walitamani kuondoka kwa amani kwani waliisaidia Yanga kufikia mafanikio na walitamani kuondoka kwa heshima. Ajabu hali ilikiwa tofauti kwani uongozi haukuwa tayari kuwaacha kwa wema. Hata pale walipolazimisha hatimaye waliondoka kwa chuki na kisununu, wakilaaniwa na kauli za "tutaona kama utatoboa"
Haya yalifanyika nyakati za Ajib kuja Simba, kina Ngasa na Domayo kwenda Azam. Hali hiyo imejirudia kwa Feitoto na Mayele. Uondokaji wa watu hawa ulifichwa sana kwa sababu za husda tu huku viongozi wakiamini vitisho vitasaidia.
Kipindi Niyonzima anakuja Simba, wana Yanga mpaka wakachoma jezi kumlaani. Hiyo ni roho ya kawaida kweli. Si ujini huo. Kumbuka kina Bangala na Djuma walivyoondoka Yanga.
Kwa hali hii hata kama ni kweli hawafugi majini, lakini kumbania mtu maisha ni zaidi ya kumtupia majini. Tazama suala ya Fei mpaka Rais wa nchi anaingilia kati, Hiyo roho ni zaidi ya jini. Nafikiri hata jini lenyewe lilishangaa. Fei sio kichaa mpaka aseme ili abaki Yanga basi Hersi aondoke.
Hizi tabia za kishwahili zinatakiwa kukemewa sio tu na wanasoka bali kina mpenda maendeleo.